Inkoskaz
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 6,372
- 2,374
Wengi wapo kizani katika kiza kinene
Ukiwakuta mtaani wanapigana vijembe
katiba ya zamani huijui mpya waitakaje
wewe mungu kakubariki, umewajuza wangapi?
Humu JF hatukosi kujadili mada na hoja motomoto za kisiasa,kuelimishana na kukosoana pale tunapokuwa tumepotoka,lakini jambo jema zaidi ni kuwa wengi wetu humu jamvini japo si haba lakini tuna ufahamu wa nini kinachoendelea hadi kufikia kukijadili humu
Hoja yangu ama swali langu kwako mwana JF mwenzangu je nje ya ulingo huu umefanya jitihada gani au kiasi gani kuwafumbua waliopo usingizini?
Mahali pako pa kazi,nyumbani kwa wanafamilia,shuleni au Chuoni, katika sehemu za umma na usafiri wa umma,majirani na hata vijiwe vya burudani umejaribu kuwafumbua wangapi kwa kuwaeleza unachokijua ama unachojifunza humu?
Nimeshangaa kukuta vijana wakibishana mtaani kwa jazba walio wengi wakisema watz wanadai katiba mpya wakati ya zamani hawaijui!
hawajui kama wanaishi katika ubepari wakati katiba ni ya kijamaa!
hawajui tuna vyama vingi vya siasa wakati katiba inasupport chama kimoja!
ukiwapata wawili watatu kwa siku popote ulipo nina hakika tanzania ya kesho haitakuwa hii ya leo iliyojaa IGNORANCE
hebu jiulize umewafumbua wangapi??
Ukiwakuta mtaani wanapigana vijembe
katiba ya zamani huijui mpya waitakaje
wewe mungu kakubariki, umewajuza wangapi?
Humu JF hatukosi kujadili mada na hoja motomoto za kisiasa,kuelimishana na kukosoana pale tunapokuwa tumepotoka,lakini jambo jema zaidi ni kuwa wengi wetu humu jamvini japo si haba lakini tuna ufahamu wa nini kinachoendelea hadi kufikia kukijadili humu
Hoja yangu ama swali langu kwako mwana JF mwenzangu je nje ya ulingo huu umefanya jitihada gani au kiasi gani kuwafumbua waliopo usingizini?
Mahali pako pa kazi,nyumbani kwa wanafamilia,shuleni au Chuoni, katika sehemu za umma na usafiri wa umma,majirani na hata vijiwe vya burudani umejaribu kuwafumbua wangapi kwa kuwaeleza unachokijua ama unachojifunza humu?
Nimeshangaa kukuta vijana wakibishana mtaani kwa jazba walio wengi wakisema watz wanadai katiba mpya wakati ya zamani hawaijui!
hawajui kama wanaishi katika ubepari wakati katiba ni ya kijamaa!
hawajui tuna vyama vingi vya siasa wakati katiba inasupport chama kimoja!
ukiwapata wawili watatu kwa siku popote ulipo nina hakika tanzania ya kesho haitakuwa hii ya leo iliyojaa IGNORANCE
hebu jiulize umewafumbua wangapi??