Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,311
- 9,740
Ndugu zangu Watanzania,
Jamii forum ni kama familia, tena familia kubwa sana japo hatufahamiani wala kuonana lakini makala zetu na michango yetu humu jukwaani imetufanya tukafahamiana hata kwa itikadi za kisiasa.
Mimi binafsi kuna member nimekuwa nikiwafuatilia kwa muda mrefu sana na kupenda kusoma makala zao, mmoja wapo ni huyu member aitwaye Faizafoxy ambaye sijamuona kwa muda mrefu sana humu jukwaani.
Kama ni buheri wa afya angefanya hata kuja mara moja kusalimia na kutoa hata maoni yake juu ya miradi mikubwa miwili iliyoanza kazi na Kuitetemesha Tanzania na Duniani nzima kwa ujumla, kwa namna mama wa shoka Mama Samia alivyo imaliza kibabe na kihodari.
Miradi hii ni ule wa SGR pamoja na ule wa bwawa la mwalimu Nyerere ambapo mtambo namba Tisa umewashwa ambao unazalisha megawati 235 ambao ni zaidi ya vinu vyote vya bwawa la kidatu linalozalisha megawati 204 na Mtera megawati 80.
Ningemuomba mama huyu Faizafoxy kama anapitia humu aje atoe hata mchango wake juu ya historia ya kipekee kabisa iliyoandikwa katika Taifa letu hili la Tanzania.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
Jamii forum ni kama familia, tena familia kubwa sana japo hatufahamiani wala kuonana lakini makala zetu na michango yetu humu jukwaani imetufanya tukafahamiana hata kwa itikadi za kisiasa.
Mimi binafsi kuna member nimekuwa nikiwafuatilia kwa muda mrefu sana na kupenda kusoma makala zao, mmoja wapo ni huyu member aitwaye Faizafoxy ambaye sijamuona kwa muda mrefu sana humu jukwaani.
Kama ni buheri wa afya angefanya hata kuja mara moja kusalimia na kutoa hata maoni yake juu ya miradi mikubwa miwili iliyoanza kazi na Kuitetemesha Tanzania na Duniani nzima kwa ujumla, kwa namna mama wa shoka Mama Samia alivyo imaliza kibabe na kihodari.
Miradi hii ni ule wa SGR pamoja na ule wa bwawa la mwalimu Nyerere ambapo mtambo namba Tisa umewashwa ambao unazalisha megawati 235 ambao ni zaidi ya vinu vyote vya bwawa la kidatu linalozalisha megawati 204 na Mtera megawati 80.
Ningemuomba mama huyu Faizafoxy kama anapitia humu aje atoe hata mchango wake juu ya historia ya kipekee kabisa iliyoandikwa katika Taifa letu hili la Tanzania.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.