NIWA
Wana JF nianze kwa kumba samahani kuchelewa kuchangia tangia jana kwa matatizo niliyojitakia mwenyewe kwa kukbali kuajiriwa badala ya kujiajiri. Muda ulikuwa kiduchu hivyo niendeleze thread hii mpaka leo. Nilipokuwa nafundishwa elimu ya dini ya Kikatoliki maarufu kama Kateksimu nilifundishwa kuwa anayejua mengi ataulizwa mengi. Naamini Mwampambwa anajua mengi maana amesoma mpaka ngazi ya chuo kikuu. Anapoamua kuandika kitu ni vizuri kiahakisi uelewa wake na kama anataka kuelezea ubaya wa kitu afanye hivyo kuonyesha ni kwa jinsi gani kile anachomtuhumu kimefanya jamii idhurike, iteseke na isononeke. Halafu aonyeshe pasipo shaka na jinsi yeye alivyodhurika na tuhuma hizo. Failure to show the magnitude of damage at individual and communal level makes the whole criticism a means to explode vendetta. Nimesoma majibu ya Mwampambwa yamekosa umakini wa uelewa na jinsi jamii au chama kilivyodhurika na tuhuma ya kukopa within the party. Na basi ili aonekane katumia chembe ya uelewa basi angetupatia na empirical study kuwa kiongozi wa jamii, taifa au chama fulani ndani na nje ya nchi aliwahi kufanya kinachofanana na hiki na akasababisha madhara. Lakini hakuna hata kitu cha aina hiyo. This is purely meeting trouble half way.
Pili haonyeshi ni lini kukopa pesa ndani ya chama imekuwa ni kosa la kulinganisha na ufisadi. Analalamikia taratibu, sheria na kanuni zisizokuwepo. Sasa malalamiko ya nini yasiyokuwa na basis. Bila basis in place everybody can fabricate things as long as the aim is implicate another person and put one's integrity in question. Ni ajabu tena kuona mtu wa aina hii mwenye kuibuka na vitu visivyokuwa na basis anapata mashabiki.Bado tunaweza kupoteza muda kwa kushabikia visivyokuwepo na tukaacha vikubwa ambavyo vimekosa mtu wa kuvisema the likes of EPA, Richmond, Rada ya kuongozea ndege, ununuzi wa ndege ya rais, waarabu wa Loliondo, mikataba ya madini, uchimbaji wa uranium, mikata ya gesi na bomba la gesi toka mtwara (nite majibu kwa wanamtwara hayajapatikana), Buzwagi, Meremeta na mengine.
Tatu, matatizo ya vyama huanzia ndani ya vikao rasmi vya vyama. Ni lini Mwampamba alipeleka dukuduku lake lijadiliwe ndani ya vikao vya vyama. Alete ushahidi kimaandishi ili tupime bila shaka kuwa alitenda kisomi na kiulewa ili hoja ikazimwa. Ilipozimwa alifanya nini. Kuna appeal organs. je alifanya hivyo. Maana kama kuna ufujaji wa pesa za ruzuku angeweza kwenda kwa CAG ili mahesabu ya CDM yakaguliwa au kwa msajiri ili CDM iwajibike. Alete ushahidi humu jamnvini na tutasema mengine. Short of that all said is a reflection of vendetta and power monger
Nne na ushauri huu nilimpa hata dada Shonza kuwa ukiwa umedhurika na maamuzi ya jamii au chama, kabla hujaenda public kujitetea kwanza fanya mambo manne;-
1. Mwombe Mungu akupe unyenyekevu katika utetezi wako- Lugha chafu, matusi na kejeli hata kwa mtu mdogo kiumri na kiutawala haina neema ya Mungu. Mwampama umekosa hofu ya Mungu. Kajute saa bado ipo.
2.Wakati na nyakati- Ulipaswa ujipe muda na ukajithathmini na uone kuwa mlichokuwa mnakifanya kiko sahii katika kanuni ya demokrasia ya magharibi yaani collective responsibility. Hii inataka mwende kwenye vikao vya ndani mbishane lakini mkitoka nje you are one hata kama mawazo yako hayakukukubaliwa au hukubaliana na mawazoya wengine. Hii ni kanuni ya demokrasia. Ukiona huiwezi basi wewe siasa si mahali pako tafuta kwingine. Hujajipa muda tangu ufukuzwe na sasa unaibuka na tuhuma. Watu makini hawawezi kukuelewa na chama makini hakiwezi kukuchukua nna kukupa madaraka nyeti maana wanajua hata kesho ukitoka utawatukana wakati maamuzi yalikuwa ni ya pamoja. Tena nakushauri kuwa better satan you know thean God you don't. Ni afadhali ukakaa kwanza halafu kesho ukaenda kwa wale voingozi wa CDM uliowatuhumu na kuwatukana ukaomba msamaha kuliko chama kingine maana huaminiki tena.
3. Maandishi (documentation) ni muhimu tena zenye rejea inayoweza kuwa accessed na watu wote na si za kughushi. All said by you and your compatriots are short of documenation hence they lack good trck records and remin to be outdate lies and fabrications.