nyampanaga
JF-Expert Member
- Nov 16, 2012
- 1,104
- 559
Hakuna kitu hapo,Slaa amekiri kukopa na kurudisha tatizo liko wapi..suala ibara nalo kwangu halina mashiko sana kwani naamini Dr.Kama binadamu wengine alikuwa na shida na pengine aliona chamani anaweza kupata mkopo kwa urahisi kuliko taasisi zingine, katiba siyo msahafu wakati mwingine busara na hekima vyaweza tumika kulingana na ishu jinsi ilivyokaa(principle of rather evil),Kudai idadi na majina ya viongozi wengine waliowahi kukopeshwa na chama toka napo naona ni pumba nyingine, wewe ulipaswa kuja hapa na majina ya viongozi amabao waliomba kukopa kama Slaa wakakataliwa hata kama ni wewe mwenyewe ungeeleweka zaidi...cha mno ungekuja hapa na ushahidi kuwa bado pesa hazijarudishwa kama alivyodai mkopaji pia ungeeleweka zaidi...Bado niko palepale hivi kesi inayo/iliyokuwa inawakabili Josephine na Dr kule Arusha ilitokana na makosa yao binafsi kama mme na mke au walikuwa kwenye harakati za kujenga chama?Jibu ni katika kujenga chama..sasa upi ubaya wa Josephine kulipiwa gharama za yaya na chama ilhali alipaswa kuhudhuria mahakamani na yeye..Na amini kabisa kama Josephine asingetakiwa na mahakama kuhudhuria basi hizo pesa zi singelipwa kwa maana si kweli kwamba dr huzunguka na mke kila anapokwenda,last time dr alinikuta kata ya Lwenzera Geita kwenye kampeni za diwani oktoba mwaka jana but hakuwa na Josephine na alikaa pale siku 2.All in all PM 7 jipangeni upya kisiasa kupitia vyama vingine...huku cdm kumegoma..lugha za matusi zinazidi kuwabomoa na si kuwajenga na bado kuondoka kwenu pengo halionekani chama ndo kinazidi kuimarika...kama mnaweza hebu anzeni kujibu mapigo kupitia siasa za majukwaani muachane na media kama hamtaishia kupopolewa mawe na chupa za maji kama kina Kinana,Pinda,Mangula nk.