Hapa nadhani ni jukumu la vyama vya upinzani, mashirika huru, na wanaharakati mbalimbali kufanya mikakati ya kuwafikishia wananchi habari sahihi kuhusu nchi yao. Wananchi wakishapata habari hizo, itawapa uwezo wa kuamua na kutenda ipasavyo pale watakapohitajika kufanya hivyo, kwa mfano katika upigaji kura.
Kwenye hili, wa kulaumiwa ni sisi wananchi kwamba kwa nini wananchi hawana elimu ya siasa tuliyonayo JF, sio kosa la CCM.
Mabibi na Mabwana najitokeza kuuliza swali ambalo nimekuwa nikijiuliza mara kwa mara kuhusu mustakabali wa nchi yangu Kisiasa hususani kwa wananchi waishio Vijijini ambako upatikanaji wa taarifa ni adimu.
Ukweli ni kuwa Tanzania inahitaji mapinduzi makubwa sana kisiasa ili kuweza kujenga jamii yenye maendeleo hasa kutokana na mauzauza ya Ufisadi yaliyoanza kufichuka na yanayoendelea kufichuka. Lakini je, Watanzania wote wana mwamko kuhusu hali nzima ya nchi yetu na ubabaishaji wa viongozi wetu waliopo madarakani? Je wale waliopo vijijini ambao kuna baadhi inasemekana mpaka leo wanajua kuwa rais wa Tanzania ni Nyerere na ndiyo wanaoipatia kura CCM bila kujijua kwa kigezo kuwa 'tunampigia kura Nyerere' wana mwamko huu tulio nao wana JF?
Manake nimeona maoni yenye matumaini kutoka kwa wadau mbali mbali ndani na nje ya JF kuwa 2010 CCM (JK) itakiona cha mtema kuni, itawezekana kweli?
Wadau naomba tufumbuane macho kuhusu huu utata ili nami niweze kufahamu mikakati pamoja na maendeleo katika suala zima la kuleta mabadiliko kwenye nchi yetu.
"Ukweli ni kuwa Tanzania inahitaji mapinduzi makubwa sana kisiasa ili kuweza kujenga jamii yenye maendeleo hasa kutokana na mauzauza ya Ufisadi yaliyoanza kufichuka na yanayoendelea kufichuka."
Na mie nifumbulie fumbo- Mwamko wa kisiasa nchini na habari adimu vijijini-Huu ni utata au?
Hiyo hapo juu bai ze wei
My take-mapinduzi ya siasa yapo na tumeendelea kuliko Nchi nyingi barani Afrika. Ukweli tunahitaji mapinduzi makubwa Kiuchumi na sio Kisiasa.
Nafikiri itakuwa sahihi kusema chimbuko la Ufisadi nchini-Ufisadi wa habari vijijini-na mwamko wa Kiuchumi na Habari Vijijini."Mwamko wa Kisiasa" ilishapitwa na enzi
Inatisha-"Chukua Chako Mapema" ni mwamko mzuri wa kiuchumi-haina siasa sasa.
Kijarida cha Jamboforums, kisichofungamana na chama chochote, kitakachosambazwa nchi nzima, kitakachotoa elimu ya siasa ama kwa bure au kwa bei ya chini kabisa, kitakachosambazwa nchi nzima na kuchapishwa kila baada ya wiki mbili.
Makala za uwakilishi zitaandikwa hapa, kuchujwa umakini, kupigiwa kura halafu kuchapishwa.
Funds zitatoka kwa members hapa na watutakiao mema.Tayari tuna waandishi wa habari na watu wa media wenye uzoefu na uchapishaji.Ikibidi hata kutengeneza soft copy itakayosambazwa bure kwa email kwa wawakilishi tofauti nchini kote halafu wawakilishi waweze ku print, kama wataweza kufanya huduma bure au kuuza kwa bei nafuu ili kurudisha gharama za uchapishaji yote ni sawa.
In any case Jamboforums need a newsletter, period.
Angalau na watu wa vijijini wapate mwamko wa kujua nini kinaendelea.Tunaweza kuweka habari za kisiasa, maendeleo ya bunge, wabunge na performance zao, ahadi za serikali kuu na utekelezwaji wake, data za kiuchumi nk.
Kwa sasa huu ndio mchango wangu.