Mwambieni Magufuli, Nimekasirika!

Mwambieni Magufuli, Nimekasirika!

Wewe soma ukijua unapanua upeo wa kufikiri ili kupambana na mazingira yanayokuzunguka. Neno kuajiriwa libadilishe liwe kujiajiri. Hata kama utaajiriwa bado wazo la kujiajiri ni muhimu .mitaala iwe inamuandaa mwanafunzi kujiajiri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kibarua hiki mnacholipwa kuandika upuuzi na propaganda dhaifu kama hizi mmeshafeli na mnazidi kukididimiza Chama Chenu. Watanzania wa sasa sio wale mliokuwa mnawahadaa kwa Operation na movements zisizo na faida
Naamini hujaandika kwa niaba ya Watanzania. Ni kwa niaba ya familia na chama chako.
 
Mimi ni nani? Mimi ni raia wa kuzaliwa na mzalendo kwa nchi yangu Tanzania, Na ninakiri kwamba pamoja na kwamba sio "wa chama kile" lakini nilimpigia kura yangu yangu kwa kuamini kwamba misimamo yake ya kusimamia katiba ingeisaidia hii nchi, (Nilikosea). Nimekasirika maana sikumchagua kufanya haya anayoyafanya sasa hivi ya kufanya neno lake ndio liwe katiba, Tafadhali Mwambieni.

Nimekasirika, kuona kwa sababu ya chuki zake binafsi na "Wawekezaji Wale" Watanzania wenzangu maelfu kwa maelfu wameachishwa kazi na kila kukicha makampuni yanaendelea kutangaaza kupunguza wafanyakazi na hata ambao bado wapo makazini hawajui kesho itakuwaje, Mwambieni sikumchagua kwa ajili ya kufanya hayo. Nilimpigia kura yangu ili aweke mazingira ya hao wenye nacho watengeneze ajira zaidi kwa watoto wetu, Nilimchagua atengeneze mazingira walau maisha yangu nami yainuke kidogo walau yawakaribie hao wenye nacho.

Nimekasirika, Binti yangu aliyesoma na kuhitimu chuo kikuu ualimu wa masomo ya arts na ambae nilimsomesha kwa mshahara wangu mdogo wa kazi yangu niliyoipoteza ya ulinzi kwenye kampuni la "Yule Mhindi" hajapata kazi tangu mwaka 2015. Wamerundikana mtaani na vyuoni bado wanaendelea kutengenezwa wengine, Nilimsomesha nikijua akimaliza ajira yake ni moja kwa moja serikalini na hivyo ndivyo ilivyokuwa, Si mngesema tangu awali kwamba ajira kwa hawa watu hazitakuwepo akasoma kitu kingine?

Mwambieni nimekasirika yeye kujifanya ndio Mungu, kuona kwamba yeye anajua kila kitu, Mwambieni kiongozi husikiliza, Nchi yetu hii ambayo watu wengi hawajui wanataka nini inahtaji kiongozi anayesikiliza maoni hata ya wachache wenye akili. Muulizeni kwanini anawachukia upinzani? Kama wanampa mawazo ya kujenga kwa nini anawachukia? Kwanini kuwakamata kamata kila siku kama vile wamekuwa maadui kisa tu wanaikosoa serikali? Nilitegemea angewasikiliza, na ambayo yanafaa angeyafanyia kazi kama hayafai angetoa majibu kwa hoja kwa nini hakubaliani na mawazo yao. Sio hivyo anavyofanya kuwachulia kama ni maadui wa serikali.

Mwambieni nimekasirika na mtaani kwetu watu wengi wana hasira. Mwambieni asipofanya jambo hawa watu anaofikiri hawana akili mwaka 2020 watamkataa, na akilazimisha ataelewa "Panya akikasirika anakuwaje". Mwambieni hajachelewa, akae ajitafakari upya, aanze upya.
Si mpaka awe na listening skills ndo aweze kusikiliza na àwe na Good communication skills ndo aweze jibu kwa hoja na kushawishi.Bàhati mbayà sàna amenyimwa uwezo wa kusikilizà,kushawishi na kujenga hoja zinazoeleweka si kwa kiingerezà wala kiswahili
 
kumbe ulipiga kura kwa ccm?

basi nakupa ''hi''
 
Mnapoandika upuuzi wenu, mue pia mnataja na vifungu vya sheria anavyovunja, kwa maana ya ibara. Na sio mtindo wenu wa kipuuzi wa ku generalise habari

Sent using Jamii Forums mobile app
Okay wataka tukutajie Ibara za kwenye Katiba yetu anazovunja Mkulu?

Ngoja nikutajie:-

1. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 3(1) inaeleza kuwa nchi yetu itakuwa ya mfumo wa vyama vingi na hakuna chombo kingine chochote kitakachokuwa na mamlaka ya kuingilia shughuli za vyama hivyo.

Sasa nikuulize wewe kada, huyo Mwenyekiti wako wa CCM Taifa, amepata wapi mamlaka ya kupiga marufuku mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani hadi mwaka 2020?

2.Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 18(1) inasema " Kila mwananchi atakuwa huru kutoa maoni yake yanayohusu nchi yake na hakuna chombo chochote kitakachokuwa na mamlaka ya kuingilia Uhuru huo wa kutoa maoni wa wananchi' mwisho wa kunukuu

Sasa swali kwako wewe kada wa Chama Cha Makinikia,hivi ni kwamlnini Jeshi letu la Polisi linawakamata watu wanaoyumia Uhuru wao wa kikatiba wa kutoa maoni yao na kuwaita ni wa wachochezi?

Usidhani wote tuliomo humu JF ni wapumbavu na malofa kama tunavyoitwa na watawala eetu , wengi wetu tunajielewa na tunazielewa haki zetu za kikatiba vizuri sana.....
 
Mnapoandika upuuzi wenu, mue pia mnataja na vifungu vya sheria anavyovunja, kwa maana ya ibara. Na sio mtindo wenu wa kipuuzi wa ku generalise habari

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahaaaa kasome sheria ya manunuzi ya serikali halafu uje utuambie umeona nini na yeye kafanya nini, kasome sheria na kanuni za utumish wa umma halafu uje utuambie umeona nini na yeye anafanya jini, kasome katiba katika kipengere cha haki za binadamu ukirudi pia utoe jibu yeye na wateule wake wanafanya nini, kasome sheria ya vyama vya siasa halafu urudo utoe jibu mjinga na mpumbavu wewe sheria zipo halafu hamsomi mnataka tuje tuwaletee sisi huku matokeo yake mmekuwa wasifiaji wa kila kitu kwa sababu hamna shule na sheria hamzijui, TULIPE DENI LA WATU.
 
Mikutano hamfanyi, Uhuru wa kutoa maoni, Kila siku mnaitisha media na kueleza hisia zenu, Kuna siku ambapo Mmekatazwa kuongea na vyombo vya habari.

Tatizo Uhuru huo mnautumia kifala, kutukana wenzenu, kuzua, kukashifu, haikubaliki popote pale duniani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mikutano hamfanyi, Uhuru wa kutoa maoni, Kila siku mnaitisha media na kueleza hisia zenu, Kuna siku ambapo Mmekatazwa kuongea na vyombo vya habari.

Tatizo Uhuru huo mnautumia kifala, kutukana wenzenu, kuzua, kukashifu, haikubaliki popote pale duniani

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni nani aliyepanda jukwaani akawaita wenzake WAPUMBAVU/MALOFA?

In white-collar crime, there are ink stains instead of bloodstains.
 
Utaambiwa hata hayo maandishi yako sijayasoma nenda kayaandike kitandani kwako ulalie na mkeo.

In white-collar crime, there are ink stains instead of bloodstains.


aisee.. mheshimiwa ana maneno ya shombo sana....
 
fanya kazi acha kulialia


Hivi ninyi mnaowaambiaga watu wafanye kazi waache kulialia mnaelewa mnachokisema? kazi ndio hizo zinafungwa kwa visasi, kazi yoyote duniani uandaliwa mazingira mazuri. Mbona hamtaki kwenda Zimbabwe kuomba au kutafuta kazi, kila mmoja anatamani aje huku USA kwa sababu kuna mazingira mazuri ya kazi. JPM anazidi kuharibu mazingira ya kazi mbalimbali nchini kwa kisingizio kuwa ni wapiga dili. Nani aliyewaambia kuwa watanzania hawataki kufanya kazi?
 
Back
Top Bottom