DELETED ACCOUNT
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 9,805
- 15,470
Unahalalisha unafki wenu.Msimu uliopita baada ya Chadrack Boka kuwa majeruhi, Nickson Kibabage ndiyo alikuwa mbadala wake! jambo ambalo liliifanya Yanga kuwa dhaifu sana kwenye huo upande.
Upande wa kulia nao Yao Kwasi alipoumia, tulishuhudia Dennis Nkane naye akichezeshwa kwenye hiyo namba! Na yeye alikuwa ni uchochoro tu!
Hivyo kwa usajili wa beki mwenye nidhamu na uzoefu kama Mohamed Hussein (Zimbwe Jr), utakuwa ni msaada mkubwa sana kwa timu ya Wananchi.
Rai yangu kwa viongozi; wahakimishe Israel Mwenda naye anabaki ili kumpa changamoto Yao Kwasi aliyekuwa majeruhi kwa muda mrefu.
Natambua kuna watu watauponda huu usajili! Ila kwa sisi ambao tumewahi kucheza na pia kuwa makocha, tunatambua fika siri ya mafanikio ya Yanga kwa miaka kadhaa sasa imejificha kwenye eneo hili la kusajili wachezaji wa kujazia mapengo yaliyo jitokeza wakati wa msimu.
Hongereni sana uongozi wa timu ya wananchi Young Africans 💛💚💪
Nauona tena ubingwa msimu huu. Siyo kwa hiki kikosi mlicho kisuka.