Congo
JF-Expert Member
- Mar 13, 2008
- 2,064
- 2,301
Luninga jana usiku na magazeti ya leo yametoa picha za Polisi walioua majambazi pale magomeni majuzi wakipongezwa hadharani.
Suala zima la kupongeza hao Polisi sio baya lakini nahofia pale jambo hilo linapofanyika hadharani tena kwa sherehe. Tujue kuwa jambo la kuua binadamu sio jema hata kama anayeuawa ni jambazi. Nazungumzia lile tendo la kuua binadamu. Sio suala la kutambia. Kama jeshi la Polisi limeua majambazi, basi, walioua wanatakiwa kutojulikana kabisa. Kama ni kupongezwa, ingetangazwa tu kuwa wamepongezwa lakini bila kujulikana kwa wananchi ni nani aliyepongezwa.
Tukumbuke kuwa hao waliouawa wana familia zao ambazo zinaweza kulipiza kisasi au kundi lile la majambazi linaweza kuwa na mtandao mkubwa zaidi ya wale waliouawa hivyo likalipiza kisasi baada ya kuwatambua wale waliohusika na mauaji ya wenzao.
Kwa wenzetu huwa naona Polisi wakiwa wamevaa "ninja" ili wasitambulike kirahisi.
Kwa wanajeshi (JWTZ), sikuwahi kusikia mwanajeshi akitamba kuwa wakati wa vita aliua watu kadhaa. Ndio maadaili yao. Kuua sio kuzuri hata kama ni lazima kufanya hivyo.
Tusiwaonyeshe vijana wetu hadharani pale wanapokuwa wametumia ujasiri wao kulinda usalama wa raia. Ndugu zao, majirani, Polisi wenzao, hata wakienda baa sasa wanajulikana "yule aliua jambazi".
Suala zima la kupongeza hao Polisi sio baya lakini nahofia pale jambo hilo linapofanyika hadharani tena kwa sherehe. Tujue kuwa jambo la kuua binadamu sio jema hata kama anayeuawa ni jambazi. Nazungumzia lile tendo la kuua binadamu. Sio suala la kutambia. Kama jeshi la Polisi limeua majambazi, basi, walioua wanatakiwa kutojulikana kabisa. Kama ni kupongezwa, ingetangazwa tu kuwa wamepongezwa lakini bila kujulikana kwa wananchi ni nani aliyepongezwa.
Tukumbuke kuwa hao waliouawa wana familia zao ambazo zinaweza kulipiza kisasi au kundi lile la majambazi linaweza kuwa na mtandao mkubwa zaidi ya wale waliouawa hivyo likalipiza kisasi baada ya kuwatambua wale waliohusika na mauaji ya wenzao.
Kwa wenzetu huwa naona Polisi wakiwa wamevaa "ninja" ili wasitambulike kirahisi.
Kwa wanajeshi (JWTZ), sikuwahi kusikia mwanajeshi akitamba kuwa wakati wa vita aliua watu kadhaa. Ndio maadaili yao. Kuua sio kuzuri hata kama ni lazima kufanya hivyo.
Tusiwaonyeshe vijana wetu hadharani pale wanapokuwa wametumia ujasiri wao kulinda usalama wa raia. Ndugu zao, majirani, Polisi wenzao, hata wakienda baa sasa wanajulikana "yule aliua jambazi".