BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
MWALIMU WA KIKE APIGWA NA MWALIMU MKUU NA KUVUNJWA JINO MOROGORO VIJIJINI. WENZAKE WAMUOMBA ASKOFU MWAMAKULA ASAIDIE KUPAZA SAUTI ILI MAWAZIRI WENYE DHAMANA WASIKIE NA KUINGILIA KATI
Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Tunapenda kukujulisha tukio la kusikitisha lililomkuta mwalimu mwenzetu aitwaye Witness Makoti wa Shule ya Msingi Mkuyuni iliyopo Tarafa ya Mkuyuni katika Wilaya ya Morogoro Vijijini Mkoani Morogoro.
Siku ya Ijumaa, tarehe 15 Oktoba 2021 muda wa Saa 6 mchana, Mwalimu Witness Makoti ambaye ni mwanamke alikuwa akiongea na wanafunzi watatu darasani. Wakati akiongea na watoto wake, ghafla alishambuliwa na kuanza kupigwa na Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo ambaye ni mwanaume aitwaye Mussa Hasira. Alipigwa sana lakini aliokolewa na mwalimu mmoja.
Baada ya kushambuliwa na kupigwa, Witness alikwenda kuripoti katika Kituo cha Polisi cha Mkuyuni na kupewa PF3 ya kwenda Zahanati ya Mkuyuni na kupata matibabu ya awali. Baada ya hali kuendelea kuwa mbaya, leo Jumapili alikwenda Hospitali ya Nunge kwa matibabu zaidi ambapo imegundulika kuwa Witness ana vidonda mdomoni na pia amevunjwa jino.
Hali yake ya kiafya mpaka sasa siyo nzuri sana na inazidi sana na ameleza pia kuwa pressure imempanda. Hadi muda huu, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Vijijini na Mkuu wa Wilaya hawana taarifa.
Mwalimu Witness Makoti anahofia usalama wa maisha yake kwani ameelezwa kuwa Mwalimu Mkuu alimfuata mwalimu aliyemgombelezea Witness akaanza kumlaumu na kusema kuwa angelimuacha bila kumgombelezea ili amuue kabisa.
Mwalimu Witness Makoti ameomba asaidiwe katika kulipazia sauti jambo hili aweze kupata msaada kusudi haki iweze kutendeka lakini pia ili kuokoa maisha yake.
Tunaambatanisha picha ya Mwalimu Witness Makoti hapa chini.
Tunakushuru sana Baba Askofu Mwamakula kwa kutupokea na tunaamini kuwa kupitia sauti yako, Witness atapata msaada anaouhitaji.
Mpendwa Baba Askofu Mwamakula!
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Tunapenda kukujulisha tukio la kusikitisha lililomkuta mwalimu mwenzetu aitwaye Witness Makoti wa Shule ya Msingi Mkuyuni iliyopo Tarafa ya Mkuyuni katika Wilaya ya Morogoro Vijijini Mkoani Morogoro.
Siku ya Ijumaa, tarehe 15 Oktoba 2021 muda wa Saa 6 mchana, Mwalimu Witness Makoti ambaye ni mwanamke alikuwa akiongea na wanafunzi watatu darasani. Wakati akiongea na watoto wake, ghafla alishambuliwa na kuanza kupigwa na Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo ambaye ni mwanaume aitwaye Mussa Hasira. Alipigwa sana lakini aliokolewa na mwalimu mmoja.
Baada ya kushambuliwa na kupigwa, Witness alikwenda kuripoti katika Kituo cha Polisi cha Mkuyuni na kupewa PF3 ya kwenda Zahanati ya Mkuyuni na kupata matibabu ya awali. Baada ya hali kuendelea kuwa mbaya, leo Jumapili alikwenda Hospitali ya Nunge kwa matibabu zaidi ambapo imegundulika kuwa Witness ana vidonda mdomoni na pia amevunjwa jino.
Hali yake ya kiafya mpaka sasa siyo nzuri sana na inazidi sana na ameleza pia kuwa pressure imempanda. Hadi muda huu, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Vijijini na Mkuu wa Wilaya hawana taarifa.
Mwalimu Witness Makoti anahofia usalama wa maisha yake kwani ameelezwa kuwa Mwalimu Mkuu alimfuata mwalimu aliyemgombelezea Witness akaanza kumlaumu na kusema kuwa angelimuacha bila kumgombelezea ili amuue kabisa.
Mwalimu Witness Makoti ameomba asaidiwe katika kulipazia sauti jambo hili aweze kupata msaada kusudi haki iweze kutendeka lakini pia ili kuokoa maisha yake.
Tunaambatanisha picha ya Mwalimu Witness Makoti hapa chini.
Tunakushuru sana Baba Askofu Mwamakula kwa kutupokea na tunaamini kuwa kupitia sauti yako, Witness atapata msaada anaouhitaji.