Mwalimu Nyerere (RIP): Matukio Muhimu Mpaka Kutuaga Watanzania

Apr 27, 2006
26,588
10,375
Wakuu ninaomba kutoa heshima kwa wananchi wote hapa forum, in the wake ya yanayotutokea sasa hivi kisiasa nchini, kwa unyeyekevu mkubwa ninaomba tumkumbuke Rais wetu wa kwanza Baba wa taifa Mwalimu Nyerere(RIP).

Ninaomba kuyafikisha kwenu matukio muhimu yaliyotokea katika kuelekea kwenye kututoka kwake, nilikuwa ninapitia maktaba yangu nikayakuta haya magazeti ya mwaka October, 1999, ya wiki ambazo zilielekeza mwisho wa Mwalimu, baba wa taifa, mwisho ambao wengi wetu tunaamini kuwa ndio uliokuwa mwanzo wa yanayotukuta sasa hivi katika taifa letu kisisasa.

Tumefikia mahali as taifa hatuelewani tena, kuna wanaonekana kuwa ni wamiliki wa nchi yetu, na sisi wananchi kuwa kama wageni, umoja wetu upo mashakani, mshikamano wetu upo njia panda, Mungu atunusuru na hili balaa tunalotaka kuletewa na wenzetu wachache wenye tamaa za utajiri wa haraka na madaraka yasiyokuwa na mipaka.

Reconciliation inaweza kuwa ni pamoja na kumkumbuka Mwalimu
Baba yetu alivyotutoka.

Ahsanteni Wakuu!
 
Salute mzee

Tuko kwenye hali mbaya sana hivi sasa.
 
ISSN 0856-5775 NO. 0885 Ijumaaa October 1, 1999.

Agosti 1998:-

Mwalimu agundulika ana kansa ya damu, lakini aendelea na shughuli zake za kutafuta suluhu kwa taifa la Burundi.

Agosti 26&27, 1999:-

Media ya Tanzania, kwa mara ya kwanza inasema wazi kwa public kuwa hali ya Mwalimu sio nzuri, lakini wasaidizi wake wanaota kigugumizi kusema ukweli, kwa kusingizia kuwa wao sio madakitari.

Septemba, Mosi 1999:-

Mwalimu, akisindikizwa na mkewe, Mama Maria na daktari wake, David Mwakyusa, wanaondoka nchini kuelekea Uingereza, kuchekiwa afya yake, na familia ya Mwalimu wanawaaambia waandishi wa haabri kuwa angerudi tarehe 28, Septemba, 1999.

Septemba, 22 1999:-

Rasi wetu Mkapa, atangaza rasmi akizungumza na CNN, na kutangaza rasmi kuwa hali ya Mwalimu kule Uingereza "sio nzuri".

Septemba, 24 1999:-

Mwalimu anazidiwa akiwa huko Uingereza, na kukimbizwa hospitali ya Mtakatifu Thomas, ambako analazwa akiwa "Hoi".

Septemba, 25:-

Rais Mkapa, anamtembelea Mwalimu huko hospitalini London na kumpelekea salam za pole kutoka kwa rais Jimmy Carter, na siku hiyo usiku kwa sauti yenye kutetemeka na majonzi, rais Mkapa, anaitangazia rasmi dunia kuwa Mwalimu anaumwa kansa ya damu.


......Itaendelea...........
 
FM heshima yako mkuu,
Miiko yote viongozi wetu walishaivunja, sasa hivi naona wameshanogewa na kula nyama ya mtu. Kama mzee Warioba alivyosema, walianza kuchafuana wao kwa wao sasa hivi dhambi imeshaanza kuota mapembe. Lakini kama taifa lazima tujiulize, huko ndiko tunakotaka kwenda?
 
Septemba, 26 1999:-

Rais Thabo Mbeki, anapitia london mapaka hospitali kumuona Mwalimu, na kumpa salam za pole Rais Mkapa.

Septemba, 27 1999:-

Gazeti la Alasiri kwa kutumia vyanzo vyake, linabaini kuwa hali ya Mwalimu ni mbaya mno, na anawekwa chini ya mitambo ya kusaidiwa kupumua.

Septemba 28 1999:-

1. Mkewe Mama Maria, na wanawe Anna na Rose, wanaanza kumuangalia Mwalimu kwa masaa 24, huku Ikulu yetu ikisema uongo kuwa hali yake inaendelea kuwa nzuri kidogo, huku ikimtuma Waziri wa Tawala Za Mikoa, Kingunge Ngombale Mwiru, kwenda huko London kusimaia utoaji wa habari za ugonjwa na hali ya Mwalimu kwa ujumla.

2. Siku hiyo hiyo, Simba wa vita Rashid Kawawa, alitaka taifa kumuombea Mwalimu, apone haraka huku akionyesha kusikitishwa sana na hali ya Mwalimu kuzorota sana kwa kasi ya ghafla, akisema"...Tunamuhitaji zaidi Mwalimu kuliko wakati wowote mwingine uliopita...."

3. Ikulu yatangaza kuwa Mwalimu amepatwa na ugonjwa mwingine ambao ni sawa na ugonjwa wa homa ya manjano, lakini madaktari wake huko London wasema hali yake ni ya kawaida.

Septemba 30 1999:-

Ikulu yasema hali ya Mwalimu ni njema, na ameanza kukubali matibabu, anageuka mwenyewe kitandani kwa mara ya kwanza tangu alazwe, na anaanza kula kidogo kidogo kwa kutumia mpira maalum.

Oktoba Mosi, 1999:-

1. Ikulu yatoa kauli mbili tofauti zikisema hali ya Mwalimu, inabadilika kila wakati ila inakuwa mbaya zaidi na kwamba amekosa tena kauli na kuhamishiwa chumab cha wagonjwa mahututi.

2. Madaktari wasema kuwa wanapigana kiume kuyanusuru maisha ya Baba wa taifa letu.

3. Rais Mkapa, awataka wananchi kuendelea kumuombea duwa Baba wa taifa.

......Itaendelea.....
 
"...Tunamuhitaji zaidi Mwalimu kuliko wakati wowote mwingine uliopita...

sielewi nianzie wapi lakini kwa ufupi hali ya kila ki2 Nyumbani kwa sasa ni mbaya sana na kama Nyerere angekuwepo sijui kama ingekuaje... lakini me nadhani nina solution au pendekezo
 
Kumbukumbu inanionyesha kwamba baada ya Mwl. Kung'atuka urais 1984 aliendelea kua mwenyekiti wa chama hadi mwaka 1999 ndio akaachia Uenyekiti kwa bwana Mwinyi, baada ya hapo ndo kwanza na azimio la Arusha likahifadhiwa katika nyumba ya milele(likazikwa)na hapo matatizo yalipoanzia, Me nadhani kuna haja kabisa ya hawa waumini wenzangu wa CCM kukubali kutenganisha Uenyekiti wa Chama na Urais ili angalau Rais na Watendaji wake wawe na Mtu au sehem ya kuwakemea, nadhani kashfa zinazoendelea sasa hivi ilitakiwa watu wawajibishwe kwani mie naona mambo yako wazi sana na kila mwananchi anona.

Naomba unikosoe mkuu ili nijifunze toka kwako
 
ISSN 0856-4973 TOLEO NA. 313 ALHAMISI, OKTOBA 11-21, 1999 RAI

Kauli nyingi za Mwalimu, kabla ya kuondoka Butiama kwa wanakijiji hicho, zilikuwa zinaashiria kwamba asingerudi. Jack Nyamwanga, ambaye amekuwa mtu wa karibu sana na Mwalimu kijijini Butiama, kwa muda mrefu, ameimabia Rai kwamba katika hali isiyokuwa ya kawaida, Mwalimu aliacha maagizo mengi yasiyokuwa na uwezekano wa kutekelezeka.

Aliacha maagizo ya kupanua mashamba, kwa kiwango ambacho kilikuwa ni nje ya uwezo wa kijiji hicho, "...Butiama hakuna uwezo wa kupoanua mashamba kwa kiwango alichokuwa anaagiza yeye.." alisema Mzee Nyamwanga. " Alituambia mambo mengi sana sasa ndio ninagundua kuwa inawezekana alijua kuwa hatarudi akiwa salama...".

Kwa kawaida haikuwa tabia ya Mwalimu kutuambia siku za kurudi safari zake kwa sababu za kusalama, lakini alituambia anakwenda kwa matibabu Ulaya, na atarudi kwenye mwezi Septemba au Oktoba mwanzoni.

......Itaendelea........!
 
Mwalimu you're simply the best, better than all rest the better than anyone. Thanks for your dedication, ethics and love to our beloved country. We wish we had another Mwalimu. Rest in peace Baba yetu wa taifa.

Umetuachia wezi, wala rushwa wanafiki wanaopenda kujilimbikizia mali na kuweka maslahi yao mbele badala ya yale ya Taifa. We wish you were still here with us. Rest in peace our beloved leader and we will always love you.
http://www.youtube.com/watch?v=fM1ujosaDTE
 
"Nitakuwa sio mkweli kama sitaeleza bayana juu ya kutoridhika kwangu kwa majadiliano mliyokuwa mnayafanya kwa kipindi cha wiki mbili zilizopita, mmekuwa mkipoteza fedha na matumaini ya amani.."

"..Tumepoteza wiki mbili hizo kwa kuwa mafundi wa kutoa taarifa za kushutumiana kwenye vyombo vya habari, huku hali ya utulivu katika majadiliano haya imetibuliwa kabisa, wengine mnatumia visingizio vya kutokuwapo baadhi ya vikundi katika majadiliano haya na wengine mnatumia mapigano yanayoendelea chini Burundi kama ndiyo sababu za kutoendelea kufanya mazungumzo"

"Kwa kweli sielewi na kwa kutumia visingizio hivyo ni sawa na kutowajibika kwa upande wa wajumbe wa mkutano huu."

Hii ilikuwa ni mara ya kwanza tangu Mwalimu awe mpatanishi wa Warundi hao, kuzungumza kwa sauti ya juu na kwa ukali sana na ya kuhudhunisha sana dhidi ya vikundi vyote vinavyopambana Burundi,

na kwa bahati mbaya hiyo ndiyo iliyokuwa mara yake ya mwisho kukutana nao pamoja.

......Itaendelea.......!
 
Field Marshall ES unajua ku-'entice'

Njia ya kuenzi yote mazuri aliyotuachia Mwalimu ni kwa kila mtu aliyeamini/anayeamini kujitahidi kutekeleza aliyotufundisha katika nyakati hizi mpya. Tusikate tamaa.
The best we can do to 'enzi' Mwalimu, ni ku-play our part diligently wherever we are, for our beloved Tanzania.

Ninaimani hata Kikwete moyo unamuuma kivyake kwa mambo yanavyokwenda kinyume na matarajio ya waTanzania katika miaka hii miwili. Atajitahidi kupambana. I hope!
 
Rais Mkapa, Ametangaza Rasmi Kifo Cha Mwalimu Baba WETU WA TAIFA Kilichotokea Leo Katika Hospitali Ya Mtakatifu Thomas Huko London, Uingereza. Ametangaza Kuutuma Ujumbe Mzito Wa Viongozi Wetu Wakiongozwa Na Makamu Wa Rais Dr. Omari Juma, Kwenda Huko Kuurudisha Mwili Wa Mwalimu Nyumbani.

Buriani Mwalimu, Mungu Akuweke Mahali Pema Peponi,

Amina!
 
Mwalimu Kwa Watz Ilikuwa Ni Zawadi Ya Pekee Ambayo Watz Inatupasa Kujivunia Japo Katutoka.
Na Hawa Viongozi Tuliona Walipaswa Kuwa Waadilifu Kama Mwalium Alivyokuwa Japo Ata Kwa 1/3.
Mungu Ibariki Tz Mungu Aibariki Africa
 
As we are heading towards the 14 of October lets commemorate some tributes to JK from all over the world.

"A great loss to, not only the people of Tanzania, but the whole of Africa and the whole world. A champion of peace and a true Pan-Africanist. May his soul rest in peace.
Chris Chilufya Kalyamba, Zambia

We have lost a leader who tried his best to unite the people of Africa and the region of Great Lakes. He also showed example to Africa leaders that it is good to retire and play yet very important political roles. His contribution will be hard to replace.
Moses Rotich, South Africa

It is very sad that Tanzania and indeed Africa has lost a statesman, a great son of Africa, a father of our nation ... I can not think of a suitable expression, which can exhaustively describe Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Mwalimu Nyerere will be remembered for his dedication to serve his people by educating them and showing the way. We will always cherish all qualities he had during his lifetime.
Gideon Kalokola, Tanzania

I grew up listening to you. The more I listened the you, the more I wanted to be you. I will always miss you Mzee. Thanks for installing Africanism in me.
Kaunda Matoke, Kenya

God bless the Mualimu. The African leaders must work harder the road to better Africa is long enough that the Mualimu could not complete.
Abdi, Kenyan

He was indeed one of the greatest sons of Africa. He shall be remembered by all those who knew and read about him. May he rest in peace.
M J Baatshwana, Botswana

I feel like I have lost my own father. May god bless his soul, amen!
William Peter Lika, Tanzania

Being one of he first African Presidents to willingly step down from power, I hope your high standard will be emulated by many more. We shall solely miss your advice to Africa. Rest in Peace Mwalimu.
Nancy Kula, The Netherlands

Dr.Nyerere's regime was kind to my tribe (Igbos) during the Nigeria/Biafra civil war. May his soul rest in peace.
Nduwuisi A . Akandu, Nigeria

Your relentless involvement in the struggle to liberate Uganda from dictatorial regimes will never be forgotten.
Rachel Mukwaya, Uganda

He was the man of the Great Lakes Region. The death has taken him at the moment when we, all, needed his solutions to African problems.
Julien Bucyabahiga, Rwanda

He was one of the best leaders to Africans and to Tanzanians that we as Africans lost in the worst crisis in African time. Let God accept him in his heaven.
K.GEBRETSADIK, CANADA

The world has lost a true Hero. May God rest his soul in eternal peace. AMEN
Lusako, USA

As the Executive-Director of the Council for African affairs as well as a Nigerian and an Africanist who has been greatly influenced by Nyerere's dedication to Africa in particular, we are going to miss this great son of Africa. One remembers the greatness and the inspirations that pours from his ideas and his vision there is only one of such unique African leader alive now, Nelson Mandela and we have lost Nyerere as he joins others like him, Kwame Nkrumah and Senghor.
Dr Bamidele A Ojo, United States

The death of Mwalimu Nyerere is indeed a blow to Africa. He stands out as an example of what a people's leader should be. At a time that other African leaders were embezzling their country's wealth, Nyerere stood above all that and remained his people's teacher. His policy of Ujama may have had some shortcomings but his intention was altruistic. He ranks with people like Mandela in the annals of African history. It will be a good thing if present leaders of the continent would emulate these two great leaders.
Amandi Esonwanne, Nigerian in Canada

Nyerere, you were a source of hope to the Central African region. Nobody can replace you. MYSRP
Gift Sikaundi, Zambia

A great man has passed that we Africans are proud of I wish I could say the same for 95%of our African leaders, who without a doubt love their sweethearts more than they love their countries. God I pray you bring him back for we are running short of Prophets.
Kobina Harleston , Sierra Leone

It was such a big shock for us. I believe that this pain will be in our hearts for century. Loosing Mwalimu Nyerere is very big loss not only for Tanzania itself but this is a big loss of whole Africa. May God put his soul in peace. Amen
MSHENGA ABDY NASSEB, ZANZIBAR- TANZANIA.

It is with great sorrow that I have learned of the loss of one of the most outstanding African leaders. He was a great teacher and inspiration to many Africans including Eritreans on the principles of freedom, hard work and self-reliance. May his soul rest in peace.
Debesay Tesfagaber, Eritrea

Mwalimu is not dead and Mwalimu will never die. His influence on politics, African identity, pan-Africanism will live on for ages. A salute to you Mwalimu, your dream will carry. As you join Nkrumah, Lumumba, Biko, Sankara, Nasser, Kenyatta in the land of our ancestors, rejoice for we the children of Africa will carry on with NYEREREISM. Accept my regards for your very positive contribution to African linguistics. Sleep well Mwalimu, Lala Salama Mwalimu. Africa loves you Mwalimu. A true African son, statesman, philosopher.
Mungai Mutonya, Kenya

Dr. Nyerere is truly a big loss for the entire Africa. Africans need to see in him a highly political role model to follow, a model of love, service and compassion. May he repose in peace around The Almighty. I will pray for his soul.
Matthieu w. Yangambi., Democratic Congolese in USA

I never look at Nyerere as a president, but a great teacher. This is very sad to me, I hope that Tanzanian leaders will follow his leadership. And I am sure God will rest his soul in greatest peace.
Allan Shoo TANZANIAN

Nyerere was as true pan African, a man who cared for all Africans and always tried to find ways and means to protect them. May his soul rest in peace.
Judithbusingye, Uganda

It is a pity that while Africa continues to lose the few heroes she has, the satanic military are the faces we see like recurring decimals on the African political scene. May his humble and gentle soul rest in Peace.
Dr. Victor A. Obajuluwa, Gary, Indiana, USA.


Tanzania has lost a great son; Africa, a great influential figure and the world a great human being. Sleep well my friend.
Althea Campbell, Jamaica

Dr. Nyerere was one of the greatest leadesr Post Colonial Africa has ever produced. He will be remember for his vision and determination. He was able to unite this nation, a task which we should all accomplish as respect for him.
Conrad Msoma, Tanzania

Dr. Julius Kambarage Nyerere means so much to me, Tanzanians as well as for all Africa. I can't find words to describe his character. He is truly 'the man of the people', and will remain the father of the nation. He was not only the leader of Tanzania but also, Africa in general. Though he left us, we are sure that one day we will be together with him. We Tanzanians promise to follow your foot steps forever, peace and unity will prevail . Amen
Kenneth Gibussa, Tanzania


Adieu! Nwalimu, the great African patriot.
O. Oduwole, Nigeria

A great pan-African giant has fallen! This is a loss not only to those who knew him, but to generations of Africans who continue to benefit from his legacies. As a co-founder of the OAU, as a champion for the entrenchment of democracy in Africa, for his efforts to free Africa from colonialism and apartheid, he has earned the title "father of Africa"! May God grant him eternal rest!
Beatrice A. Hamza, New York, USA

Credit for the current democracy, peace and stability in Tanzania goes to the late President Nyerere. Tanzania is one of the few African counties exercising democratic political process. We Africans have to learn from Nyerere's legacy. History is always a fair judge. Let him rest in peace.
Alemayehu Daba, United States

We have to believe that he is dead, but his spirit and his thoughts are still with us. May the great teacher's soul rest in peace.
Abdallah Liguo, Tanzania

Our dear "Mwalimu" is gone at 77years and may his gentle soul rest in perfect peace. While there is a tendency to highlight the economic difficulties which his rule foisted on Tanzania, it is pertinent to point out that he pointed the country in the right direction in many other respects. Tanzania was spared the consumer society which characterised many post-independence African states thereby drastically reducing social problems. The simple and ascetic lifestyle of Mwalimu was always a reference point for Tanzanians. It is hoped that despite the embracing of market economics by the present rulers of Tanzania, they will not jettison all that is noble and edifying in the teachings of Mwalimu. While I wish our teacher, Nyerere, a peaceful rest, I also wish all Tanzanians and indeed all Africans and humanity a more positive and responsible social direction as envisaged by Mwalimu.
Efosa Aruede, Nigeria

A true humanist, a great communicator and unifier - an African of the highest intellect. He made mistakes, but who doesn't? I admire him.
Christian Sorensen, Denmark

We Africans are victims of many tragedies, most of them unfortunately self-inflicted. Dr Julius Nyerere, Mwalimu remained as a shining inspiration to many of us. An inspiration that reminded us that we can rid our continent of all these tragedies. He helped us defeat apartheid. He taught us integrity, he taught us to serve our fellow citizens, he taught to know that the measure of a leader is not how many Mercedes Benz cars he has or how many wives he has. He taught us that a leader can relinquish power and still remain influential. He taught to listen to one another. He brought respect to a continent that, more often than not, fails to respect the rights of its people. Mwalimu will be missed but not forgotten. Be at peace Mwalimu with yourself, you have done more than was expected of you for Africa.
Mziwakhe John Tsabedze, Swaziland

He was indeed a great man who set a very good but rare example of voluntarily stepping down to pave way for younger leaders. May his Soul Rest In eternal Peace
George Mwale, Malawi

It is difficult to believe that the father of our nation is dead. Left are the memories of the good things he did to his nation and the world at large during his life time. Tanzanians will always remember him. May God rest your soul in peace. Amen!
Frank Mathew, Tanzania

We will never forget what you did to our country and the rest of Africa. People of your type occur once in century... Rest In Piece and help us from wherever you are now!
Primus Dias Nkwera, Tanzania

A great loss!! He had fully accomplished his mission and his spirit will forever live within Tanzanians and all other peace-keepers.
Betilda C Ngeleja, Tanzania

My condolences go out to all Tanzanians, both at home and away. For myself, having spent most of my formative years in Tanzania, I got to see the influence that Baba Taifa Nyerere had on everyone. His guidance was well respected and honoured by Tanzanians. He showed true leadership when he stepped down to make way for Ali Hassan Mwinyi. This was a single act of mature leadership and it is something rarely seen in many of the worlds governments especially in Africa and Asia. I can say this much that his presence will be well missed and our prayers are with the family and nation at this time.
Hansel Ramathal, India/USA

Nyrere was one of the very few who worked for Africa to be self-dependent, there is a lot to be learned from him.
Ted Andemichael, USA

Mwalimu, you made Tanzania a great neighbour to Malawi. Your efforts to unite the turbulent continent of Africa will be greatly missed.
Joshua Lichakala, Malawi

It is a sad day for the world because a great statesman is gone and I therefor send my condolences to the people of Tanzania and the family of ex-president Nyerere.
Magnus Svensson, Sweden

In the desert wastelands of Botswana Mwalimu was an icon, a motivator and mentor Fairwell Mwalimu. Dusk has approached too soon
Bobana Badisang, Botswana

My heartfelt condolence to all Tanzanians and fellow Africans who mourn Nyerere. We lost a great son of Africa.
Ephrem Hunde, Ethiopia

I find it difficult to get the best words that explains him well. However as one of the most influential statesmen history has ever produced on the continent his name will live above all others. He remains a fallen hero of his generation.
Shekania Bisanda, United Kingdom

Tanzania will not be the same again. However the strong foundations of unity and love in Tanzania will live forever.
Ngahyoma, Tanzania

My sincerest condolences at the loss of our pillar. You will be remembered for your honest, flexibility and good leadership. Rest in peace Mwalimu..
Denford Madenyika, Zimbabwe

The world has truly lost a true giant; the conscience of Africa.
Henry O, USA

There are many Norwegians here who are saddened by the news of the death of Mwalimu J.K.Nyerere. He was very respected and loved.
Bjorg Evjen Olsen, Norway

Nyerere our brave man, you won so many battles and you fought for so many, today we have not been able to fight for you on this single war, now you lay there helpless, nature has taken over beyond us, doctors have tried and failed, may almighty God rest your soul in peace, amen. May God retain the great wall of peace which you built for us, stone by stone.
James Mhagama, Tanzania

"Mwalimu" Julius Kambarage Nyerere has gone down this day as a true and admirable citizen of the world. If he erred, that was only because he was human -- not because he meant any harm to humanity. Yes, "mzee" was wise, honest and, I strongly believe, abhorred corruption. Did you come too early or too late for Africa? Where shall we get a replacement for this modern time Colossus? No we must create one out of his ideals. Is there any greater honour? To Tanzania "I mourn with you with all my heart". RIP Baba.
George Were, Sudan

The loss of Mwalimu Julius Nyerere goes beyond the borders of Tanzania. The story of today's freedom in the region cannot be complete without the mention of Nyerere. He set standards his contemporaries could not match, standards which the present generation of leaders is struggling to emulate. He deserves a peaceful rest
Gracian Tukula, Malawi

We as Africans have lost one of the best figures in the turn of the century .Let us be strong in this time of grief and sorrow. Be strong and follow his steps.
Michael Mbagu, USA

If tears are expression of extreme grief and sorrow, then let the tears flow in all corners of africa for with the death of Mwalimu, Africa has lost its shinning star.
I. O. Mensa-Bonsu, Switzerland

Mwalimu will be missed by all peace loving democrats in the world. He was a shining example of a leader. He prepared his political successors. Even in death he lingered on to prepare his people. The man has died but his good legacy begins to live. RIP Mwalimu.
Henry Kafwembe, Zambia

Africa will remember Dr Nyerere as a great statesman who lived up to his principles. African leaders should emulate the late Dr Nyerere's attributes.
Patrick Ruzinda, The Netherlands

He was a wonderful African statesman and his death is an irreparable loss to thousands of African people. May the Lord rest his soul in peace.
Phillip Maiyo, Kenya

As a teacher of social and political thought, I included his ujuma ideology in my course syllabus to enrich our class discussions and provoke students to explore other ideologies.
Noel Servigon, Philippines

It is a sad moment for Africa. It would be a proper tribute to Nyrere if some of the African leaders who are clinging to power for so long by manipulating the political systems of their countries could borrow a page from Nyrere's life and opt for a smooth transition of power.
Gebre Gebremariam, USA/Ethiopia

Rest in Peace Julius Kambarage Nyerere. You did many good things to Tanzania and Africa. Your name and fame will last forever.
Shadrack E. Ndosi, Sweden

Man of dignity, courage and honesty, Nyerere was an example for Africa, especially for African Heads of States who stick to power, are afraid of Democracy and only care about themselves.
Sindou Diarrassouba, USA

Africa has lost a father. We thank you for the work you have done for us and the generations to come. The best tribute Africans and especially the leaders have to give Mwalimu is to emulate his example and to work hard for the African Unity. Then the work he began would be accomplished. May the Lord bless his soul and he rests in everlasting peace. Amen.
Evelyn Mukasa, Belgium

Africa and the free world will miss you Mwalimu. Humble, intelligent and always ready to fight for freedom of the black man. Rest in peace.
Sigombe Paul , Uganda

What a great lose to Africa as a whole. Mwalimu Nyerere must be remembered by all, and in fact the current African leaders need to complete the work started by him. They must now seek ways to bring peace in D R Congo and many other volatile countries.
Dr. J. K. Lonyangapuo, Kenya

There is no doubt that Dr. Julius Nyerere is one of the most influential leaders of this century. He was certainly the most respected in Africa. Many Africans see him as the advocate of democracy, decency and the rule of law in Africa. I wish to send my condolences to his family, friends and all Tanzanians and acknowledge that Dr. Nyerere will remembered by many and emulated by many.
Zakariya Suleyman, Australia

The world is a poorer place today. My heart felt sympathy to the people of Tanzania and the family of Mwalimu. If only more world leaders would demonstrate his compassion, humility and the wisdom to admit when they get things wrong.
Joy Clancy, Netherlands

Mwalimu J.K.Nyerer it is hard to accept the truth that you are gone. You will always be remembered for your guidance honest dedication and wisdom. Tanzania enjoyed peace, freedom of religion and national unity throughout because of you. Father may God Rest you in Peace.
O.Mongi & E.Mosha, Tanzania

May his soul rest in peace. In his greatness, he was humble. Africa will not forget him.
Aida Kiangi, Tanzania

Mwalimu will be greatly missed as a true world leader. His legacy is the unity and peace of Tanzania in a troubled continent.
Tony Janes, UK

To me Mwalimu was more than a father but also God's messenger of his days, I won't forget free education, free water supply services, electricity, and the like. I won't forget the peace we are enjoying this moment, unity among Tanzanians, sense of humility which was given to us through his wisdom, love and co-operation - all these are the result of his leadership.
Alex Maira, Tanzania

It is a big loss for Tanzania, Africa and the world that, Mwalimu has left us! His wisdom and contribution towards the liberation of Africa as a whole will be remembered for ever. With great sorrow I say ''Kwaheri Mwalimu''!. May God rest his soul in eternal peace!
Tobias Mufuruki, Tanzania

Mwalimu Nyerere was the most honest, dedicated, and charismatic African leader. I, and my family share Tanzania's grief, and send our condolences to his family.
Said H S Al Dhahry, Sultanate Of Oman

Hamba Kahle Julius Nyerere. A towering African philosopher and politician. A man of rare integrity, would that there were more like him.
Carole Andrew, South Africa

Rest in Peace. You led Tanzania with dignity, and when the time came you stepped down and gave way to others who had new ideas in the running of your country. I hope other leaders in Africa will emulate you, instead of holding on to the myth of life leadership. Africa needs more Nyereres. If there is magic on how to do this effectively on the other side please send us some. Africa badly needs it.
Esther Kasalu-Coffin, Cote D'Ivoire

Mwalimu your teachings and principles will remain in our hearts forever.
Hiten Pandya, United kingdom

Africa and Tanzania in particular has not only lost, a leader but a wise man whose efforts and love for humanity may take another century to come across May God the almighty rest his soul in eternal peace amen.
Leo Mazigo, Tanzania

We believe that you are the one that had led us where we are. You are the farther of our nation. For many, many years to come your name shall be remembered, because you were "a god of small people"
Shedrack Mziray, Tanzania

He was a Great Philosopher. The Tanzanian government should consider establishing a Nyerere memorial centre in Tanzania to honour his greatness
Makundi Emmanuel, University of Bergen, Norway

Not only Tanzania has lost, Africa as a whole has lost. He has played a vital role in the liberalisation of the people of Africa and the world at large. May his soul rest in peace.
Ishmael lekwape, Botswana

Other East African leaders should take opportunity of his death, to reflect on their own popularity and performance. He was still popular 14 years since he left power, because he led by example, he preached Ujama and practised it, in other words "he preached water and drank water". He remains the most honest leader East Africa has ever produced. God bless Africa with another Nyerere, his type is all we ever needed.
Joshua Odeny, Kenya

A true statesman, our country will miss your outstanding wisdom!
George S. Kivaria, Tanzania.

This is the saddest moment in the history of Tanzania. Rest in Peace Mwalimu Julius Nyerere. Amen
Laurent Ndalichako, Tanzania

Mwalimu was a great man, ahead of his time, a visionary whose vision for Africa is accepted as the norm today, but whose vision of rural Africa was not right for the time. He had the confidence in his people and himself to hand over leadership to a new generation - something his brothers in most other African countries have never had. He was a great man, the father not only of Tanzania but of much of post-colonial Africa. He will be missed.
Mike Bess, UK

Almighty God, give us another person similar to Mwalimu J.K. Nyerere. In the name of Jesus we pray - AMEN
Wildard Lwiza, Tanzania

This is truly a patriot Africa has lost... His non corruption stand should server as a good example to many leaders...His is an honourable exit...
Abel, Kenya

When someone you've known all your life dies, it sure is a tragedy. Mwalimu Nyerere is as close to the people of Uganda as to the people of Tanzania. He has been one of the fathers of the liberation of our nation. Truly, he was a great man, and should be recognised by friend and foe, even as we go into the millennium.
Anne Lydia Sekandi, Uganda

I extend my heartfelt condolences to the people of Tanzania at the loss of this great man, Dr. Nyrere, the Teacher and the leader. I feel the loss is also shared by all Africans for Dr. Nyrere was one of the few early founders of Africa.
Habte Asfaha, USA

The death of "Mwalimu" Nyerere is indeed saddening especially to all of us who saw him as a man with a vision of a united and peaceful continent of Africa. We share this grief with our brothers and sisters in Tanzania and hope to build upon his vision in securing unity and peace in this region. May God rest his soul in eternal peace.
E. Kinyangi, Kenya

Africa has lost a great leader! A leader who left power without force. He will always be remembered as "The Father Of Africa" May Dr Nyerere rest in peace.
Yusufu-Shaft Kayima, Uganda - Sweden

Long live Mwalimu the great teacher. Your great works are your immortality. Thank you for teaching African leaders that there is life after power.
Ronald Goredema, Zimbabwe

May our memory of you live forever.
Razia Alibhai, Belgium

Our father of the nation has gone. Mwalimu Nyerere, you will be remembered by all of us for cultivating peace and solidarity among Tanzanians and African as a whole.
Charles Mhagama, Tanzania"
 
Ni jambo la kushangaza sana kuona ya kuwa karibu viongozi wote walioko serikalini na katika nyadhifa za juu wamefanya kazi na Mwalimu kwa karibu sana lakini ndio wanashindwa kuenzi matendo yake zaidi ya kutumia jina lake kujinufaisha kisiasa.

Ni ajabu sana kuona Mzee kama Kingunge amejisahau hadi kutetea ufisadi uliopo sasa serikalini,Mtu kama JSM alishatungiwa hadi kitabu kuonyesha jinsi alivyo mshauri mbaya kwa Rais jambo ambalo linaweza kuhatarisha ustawi wa taifa leo hii Chama kilekile alichokiasisi Mwl. kinamtumia kama baba wa ushauri.Bungeni JSM akisimama kusema kitu ni kama kafunga mjadala.Katika sakata la Zitto hali hiyo ilijitokeza baada ya Spika kumtaka Zitto ajitete kabla ya kumwita JSM kuhitimisha.

Msururu ni mrefu,Kuenzi matendo ya mwalimu sasa imekuwa kama HEKAYA ZA ABUNUASI ambazo watoto wakihadithiwa wanadhani ni kweli.Kusema kuwa Mwl alihitajika zaidi wakati huu kuliko wakati mwingine,ni kuingilia mipango ya MUNGU. Wapo wengi wenye dhamira ya kweli,uadilifu na chuki dhidi ya ufisadi ambao WaTZ tulipaswa kuonyesha nia ya kuwaunga mkono, lakini kwa sababu ya ujinga wa kuona Vyama ni muhimu kuliko Tanzania tunasahau wajibu wetu. Nisingeshangaa kama viongozi wakuu wangekuwa wanamfahamu Mwl kwa kumsoma vitabuni na magazetini kama wengi wetu,lakini kufanya nae kazi kisha unamtaja kama backup yako kisiasa huku ukifanya yale aliyoyapinga maisha yake yote! huu ni UHAYAWANI mkubwa.

Mungu airehemu roho ya Mwl.Nyerere na atuhurumie sisi kwa kuwajaza hekima hawa viongozi wetu wajue kuwa njia wanayoyuelekeza kufuata siyo na kama kutumbukia shimoni hata wao watatumbukia nasi,furaha yao na familia zao itatumbukiwa nyongo.
 
Mzee Ibrahim Mohamed Kaduma,
Ni mmoja wa Watanzania wachache wenye uchungu wa kweli na nchi yetu, nani anayetambua kwa vitendo mchango wa huyu mzee?
 
Makamu wa Rais Dr. Omar Juma, akiongoza ujumbe mzito wa kitaifa ameondoka jijini jana kwenda London, Uingereza kuuchukua mwili wa Baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere. Dr. Omar na ujumbe wake wa watu 10 wanatarajiwa kurejea kesho wakiwa na mwili huo.

Waliopo kwenye ujumbe huo ni Mkewe Dr. Omar, Mama Salma Omar, Waziri wa Ujenzi Bi. Anna Abdallah, Makamu Wa Mwenyekiti wa CCM Bara Dr. John Malecela, Naibu Kiongozi Wa Upinzani Bungeni, Bw John Cheyo, Kiongozi wa Upinzani Bungeni Bi. Fatuma Maghimbi, Mwenyekiti wa Vijana CCM Bw. Emmanuel Nchimbi, Naibu wa serikali ya mapinduzi Zanzibar, Bw. Omar Mapuri, Mbunge wa Musoma Vijijini Blozi Paul Ndhobo, Abbasi Mhunzi na Bw. Haji Mkema wabunge wa CUF, na Bw. Hamadi Fadau pia mbunge wa CUf.

Ujumbe huo uliondoka kwa ndege maalum ya Boeing 737, saaa 3:14 na inategemewa kugeuza leo jioni na kuwasili Jijini Jumatatu asubuhi. Ujumbe huo uliagwa na mawaziri akiwemo waziri wa nje Bw. Jakay Kikwete, Naibu waziri wa mawasiliano Dr. Maua Daftari, na pia balozi wa Uingereza nchini BW. Bruce Dinwiy.

.......Itaendelea........
 
naomba nimnukuu marehem Chachage S. L Chachage katika kitabu chake cha makuadi wa soko huria ukurasa wa 82

"Nawasihi wale ambao wamezoea kudai ushahidi kwa kila jambo, ushahidi wa kupimika kwenye mizani ya sheria unaoishia katika upendeleo kwa wazandiki na mabaradhuli na kuwanyima haki wanyoofu na wanyonge, wasithubutu kuninyoshea kidole"

Bubu ataka kuongea nilitaka tu hawa wezi niwapanue kimawazo maana hawa wezi walikuwepo toka enzi za Mwl Nyerere wamejitokeza waziwazi baada za mtu mzima kututoka.

Enzi za Nyerere watu hawa waliwajibishwa ipasavyo ili kusafisha jina la Serikali kama unakumbuka Waziri mkuu J.S Warioba alijiuzulu kwa influence ya nyerere baada ya mawaziri wengi kukumbwa na kashfa ya Rushwa hivyo ikaonekana serikali ya mwinyi yote imejaa rushwa. Mwl. alimshauri mwinyi avunje baraza lake lakini baada ya WArioba Kujiuzuru japo baada ya kuunda Baraza jipya alimrudisha tena Warioba.

Hapa nilitaka nitoe kumbukumbu kwa serikali hii ya Majangiri wapunguze ushkaji la sivyo watatupeleka kubaya.

Naomba Kuwasilisha
 
Mwalimu alifariki Oktoba 14, 1999, huko London, Uingereza na tangu siku hiyo hadi sasa hivi taifa letu zima limo katika simanzi kubwa.

Tunamsindikiza Baba yetu kwenda katika nyumba yake ya milele, huku tukijiuliza maswali chungu nzima. Giza limetanda katika mioyo yetu na fikra zetu kwa sababu hatuna uhakika nini kitatokea baada ya kumaliza kumlaza mzee wetu. Ni wazi katika kipindi hiki kuwa na tafakuri ya kiyakinifu kuhusu hali ya mambo na mustakabali wa taifa letu ni kazi nzito sana.
Lakini tunapokwenda kumlaza Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, katika nyumba yake hiyo ya milele, pia tukumbuke kwamba tunayo majukumu makubwa kwa taifa letu.

Buriani Baba wa Taifa letu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mwenyezi Mungu aipokee roho yako na kuilaza mahali pema milele,

Amina.
 
Back
Top Bottom