Mwalimu Mkuu adaiwa kumlawiti mwanafunzi Bunda

Hatari sana huyu mwalimu,siku hizi kuwa mwalimu mkuu/ mkuu wa shule hakuzingatii maadili ya mhusika bali ni kitita alichotoa mhusika kwa maafisa wa juu,sidhani kama huyu mwalimu alipitiwa na shetani kama ambavyo wengi hudai bali ni inaonekana anatabia hiyo tangu mwanzo na hapo ndo arobaini zake zimefika.

Akili za kijinga na kihuni,unabaka ,haitoshi unalawiti na hujaridhika unaamua kujaribu kutoa uhai wa mtoto wa mwenzio ,akili gani hizi.?
Bora angebaka pekeake kesho angembembeleza dogo na vizawadi asitoe Siri ila katatua Hadi rinda jamaa ni kichaa aisee.
 
Hatari Sana. Kama kweli.
Ninachojiuliza ni kwamba, huyo mtoto baada ya kubakwa na kulawitiwa, ilikuwaje arudi tena kwa mwalimu yuleyule na aanze utaratibu wa kumpa sumu. Yaani hiyo sumu alikuwa anambugiza kwa nguvu au alimwekea kwenye chakula?
Mtoto amebakwa na kulawitiwa, ameenda kwa mama yake kesho yake kusaidia kufukuza ndege then arudi tena kwa mbakaji katika mazingira yanayowezesha kulishwa sumu ?

Hili tukio inawezekana ni la kweli lakini mbona Kama Kuna utata wa mtiririko?
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara linamshikilia mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Masaunga wilayani Bunda, Vicent Nkunguu (39) kwa tuhuma za kumbaka na kumlawiti mwanafunzi wa darasa la sita shuleni hapo kisha kumnywesha sumu.

Akizungumza na Mwananchi kwa simu leo Machi 13, 2024, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Salum Morcase amesema vitendo vya ubakaji na ulawiti vilifanyika siku moja kabla ya kunyweshwa sumu siku iliyofuata lengo likiwa ni kupoteza ushahidi.

Kamanda Morcase amesema mwanafunzi huyo (16) alibakwa Machi 8, 2024 usiku akiwa amelala nyumbani kwa mtuhumiwa huyo Kijiji cha Kisorya alipokuwa amekwenda kwa ajili ya kuwapikia watoto wa mtuhumiwa baada ya kuombwa na mke wa mwalimu huyo aliyesafiri kwenda kwenye maombi katika Kijiji cha Igundu.

"Akiwa amelala na watoto chumbani, mwalimu huyo alikwenda kwenye chumba cha watoto na kumwambia mwanafunzi huyo kuwa, amekosa usingizi na kwenda naye kwenye chumba chake ambako alimbaka na kumlawiti," amesema.

Kamanda Morcase amesema baada ya kumaliza haja zake alimruhusu kurudi chumbani kwa watoto na siku iliyofuata mtoto huyo aliitwa na mama yake kwenda kufukuza ndege kwenye shamba lao la mpunga.
Hii habari ndio imeishia hapo?!
 
Mwanamke mpumbavu huiharibu nyumba yake mwenyewe. Huyo mama wa maombi ameshindwa kuomba akiwa kwake Hadi aende kwa wachungaji wa michongo?
Kibaya zaidi anamjua mumewe halafu anamletea asusa yeye mwenyewe.
Anakwenda kumkemea shetani Kijiji Cha pili huku akimuacha ibilisi nyumbani. Pumbavu Sana huyo.
 
Back
Top Bottom