Smiles
JF-Expert Member
- Aug 24, 2009
- 1,231
- 107
Na Hidaya Kivatwa
Mkazi wa Kimara Abduswamadu Shabani (25), mwalimu wa shule ya kiislwamu (madrasa) ya king'ong'o amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wilayani Kinondoni kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wake.
Awali alidaiwa kuwa Agosti 26, mwaka huu huko Kimara King'ong'o alimbaka mtoto ambaye jina limehifadhiwa.
Hati ya mashtaka ilieleza kuwa mtuhumiwa alitenda kitendo hicho wakati wa muda wa mapumziko, naye alitumia muda huo kumuita mtoto huyo na kumuingiza katika kibanda chake cha biashara na kuanza kumbaka na alipomaliza alimpa ubuyu na baada ya hapo alirudi darasani na kuwaruhusu wanafunzi waende nyumbani.
Mshtakiwa alikana shtaka hilo na yupo ndani kwa kukosa wadhamini hadi hapo kesi itakapotajwa tena Septemba 14, mwaka huu.
Source: Mwananchi
Sijui tunaelekea wapi jamani, inaumiza sana kuona mtu mzima anatenda kitendo kama hiki, imagine wewe kama ni mzazi wa huyu mtoto - hivi kweli?? nashindwa kuamini ukatili wa namna hii.....akifanyiwa mwanao??? hii ni laana au???
Mkazi wa Kimara Abduswamadu Shabani (25), mwalimu wa shule ya kiislwamu (madrasa) ya king'ong'o amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wilayani Kinondoni kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wake.
Awali alidaiwa kuwa Agosti 26, mwaka huu huko Kimara King'ong'o alimbaka mtoto ambaye jina limehifadhiwa.
Hati ya mashtaka ilieleza kuwa mtuhumiwa alitenda kitendo hicho wakati wa muda wa mapumziko, naye alitumia muda huo kumuita mtoto huyo na kumuingiza katika kibanda chake cha biashara na kuanza kumbaka na alipomaliza alimpa ubuyu na baada ya hapo alirudi darasani na kuwaruhusu wanafunzi waende nyumbani.
Mshtakiwa alikana shtaka hilo na yupo ndani kwa kukosa wadhamini hadi hapo kesi itakapotajwa tena Septemba 14, mwaka huu.
Source: Mwananchi
Sijui tunaelekea wapi jamani, inaumiza sana kuona mtu mzima anatenda kitendo kama hiki, imagine wewe kama ni mzazi wa huyu mtoto - hivi kweli?? nashindwa kuamini ukatili wa namna hii.....akifanyiwa mwanao??? hii ni laana au???