Mwakyembe unaua bandari yetu

Shughuli ndo kwanza imeanza,tutaheshimiana mwaka huu na ujao! Si mlikua mnatusanifu na kutuona maboya! Zile nyumba zenu ambazo hazijaisha ndio msahau! Shwaini!
 

Nadhani huko sahihi mkuu wangu. Chini ya utawala huu sitarajii mageuzi yeyote ya maana huko bandarini. Watapigana vita wao kwa wao,mwisho huduma zitazidi kuwa mbovu zaidi. Mtu mmoja hawezi fanya mabadiliko bila ushirikiano na wenzake.
 
Huna lolote unawaita wenzio mbumbumbu kisa mirija Yako imezibwa mwaka huu mtasema yote
Naona lifestyle zimebadilika home unaulizwa nini?
 
Ameisha waambia kama mmeshindwa kazi muache na wote mtakaojaribu kuhujumu atawatimulia mbali.
 
K
wani utamfanyaje? au ni sumu tena?
 
Loading and unloading permit huandaliwa Na kupitishwa Kwenye mikono mitatu minne, kabla ya meli kuweka nanga bandarini..

Na kila anayeleta mzigo huweka foleni ya DIS yake mapema ili kuepuka inboard charges. Na this is a smooth method ambayo wala haina ucheleweshaji wowote wizarani. I am sure kuna viwavi wachache Kwa maksudi waliokuwa wanafaidika Na poll ambao wanaona mambo ya wizarani ni kunyimana mlo manake mlo umeondolewa kwao, au wale Wa wizarani nao wameamua kuyaweka pending mafaili husika wakiwangojea face-to-face walengwa ili nao wajipatie ugali ambao hapo awali mlifaidika nyie. What I advice mzee Mwakyembe asichoke, bado kuna vikunguni, viroboto vingi tu so aunde vijitume vya siri kubaini wacheleweshaji hawa Na kuwapatia Keki Yao inayostahili..
 
Bodi Mpya ya Mamlaka ya Bandari: Uteuzi wa Bodi Mpya ya Mamlaka ya Bandari iliyofanywa na Mhe. Mwakyembe ni tumaini jipya kwa uhai na ufanisi wa Bandari Tanzania. Ninawafahamu vizuri Bw. John Ulanga, Dr. Jabiri Bakari Kuwe na Dr. Shayo. Hongera sana Dr. Mwakyembe kwa uteuzi makini. Kumbe watenda kazi wanajulikana, kwanini wateuliwa wakati jahazi limeshazama?
 
Naona wengi mnaongelea "mirija" point yangu siyo hiyo, efficiency ya bandari popote duniani inategemea sana speed ya kuipokea meli kupakia/kupakua mizigo na kuondoka kwa upande mmoja na speed ya ku deliver mizigo kwa mteja kwa upande mwingine. Kwa TPA kama stevedore company inahusika moja kwa moja na speed ya kuipokea meli kupakia/kupakua mizigo na kuondoka kwa meli bandarini. sasa kama meli ziko nje na tayari zimeisha kamilisha paper work yote ya kuingia bandarini na kufanya kazi bandari iko wazi, yani hakuna meli ndani lakini meli haziingi kwa sababu kuna mkubwa mmoja wa wizara hajatoa go ahead, efficency itapatikana vipi? nani atakubali alete meli yake Dar es salaam, bandari ambayo akifika anakaa wiki nzima na zaidi nje bila kupakua mzigo wakati ana deadline ya kumeet kwenye bandari zingine? hii beauracracy nini?
 
Nadhani hapo kwennye red mdau alikuwa anamaanisha "acha watu tufanye ufisadi"
 
JK atakuwa anajuta kwanini aliwaweka wasomi humo kunakonuka ufisadi

Nimependa approach ya Dr. Mwakyembe. Anataka aangalie tofauti labda kama kutakuwa na inconvenience atabadili lakini tofauti itakuwa imeonekana
 

Nyie ndo wezi wakubwa wa makontainer yetu
 
Naona wengi mnaongelea "mirija" point yangu siyo hiyo, efficiency ya bandari popote duniani inategemea sana speed ya kuipokea meli kupakia/kupakua mizigo na kuondoka kwa upande mmoja na speed ya ku deliver mizigo kwa mteja kwa upande mwingine.
Mkuu, mbona nasikia nyie ndo mnakwamisha ili watu waweze kukata mkwanja?

Tumpe muda na hiyo approach yake. Wakati huo wewe utakuwa unarekodi demerits
 
Wela wela sitoi bil ya helaaaaaaa.............................kinanikumbusha kibwagizo cha Masanja enzi zile.
Vip mwakyembe kachomoa drip nini?
Jipange mwana kutoka sio lazima uwe bandarini tuu!
 
Mkuu, mbona nasikia nyie ndo mnakwamisha ili watu waweze kukata mkwanja?

Tumpe muda na hiyo approach yake. Wakati huo wewe utakuwa unarekodi demerits

Mkuu labda umuulize anamaanisha nini kusema bandari iko wazi? Gati zote zimekaa meli, huo uwazi anamaanisha nini?
 
Mkuu,

Mbona huo ucheleweshaji upo miaka yote hata kabla ya kuingia huyo mheshimiwa, huko nyuma meli hasa za mafuta zilicheleweshwa ili watu watengeneze ulaji kupitia adhabu ya kuchelewesha meli!!!!!

Watu hawaungani nawe kwa sababu karibu kila mtu hapa kaonja shubiri ya hapo bandarini, wengine tunampa muda kwani tunafahamu sio rahisi kurudisha ufanisi ndani ya siku moja hapo bandarini.

Badala ya kumwambia awaache muendele kufisadi nasi tunawashauri mpeni ushirikiano muwache kufisadi uchumi wetu.


 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…