Mwan mpambanaji
JF-Expert Member
- Apr 3, 2008
- 482
- 131
Ndugu wanaJf
nimetafakari hali ya giza na tanesco,na kutoka na uamuzi huu
Sita na mwakyembe hawawezi kamwe kutoka kwenye hili zigo na daima watanzania na wapenda ukweli hatutawasamehe na histori itawahukumu,mtakumbuka kuwa mwakyembe kwa makusudi kabisa alificha ukweli kuhusu kampuni hewa ya richmond kwa kuhofia serikali kuanguka,alidiriki hata kutamka hadharani eti kama angesema yote serikali ingeanguka,ukweli hauwi nusu na kwa mwakyembe kuuficha ukweli amekosa uadilifu na hivyo kupelekea leo taifa kuingia gizani
Sita akiwa spika hakuwatendea haki watanzania kwa kukubali ripoti nusu iliyoficha ukweli na kukubali kufunga mjadala wa richmond
hawa wawili walikuwa na nafasi ya kutosha kuutetea ukweli na leo hii taifa tusingekuwa gizani na uzalishaji ungeendelea
Hawa ni wanafiki,na wahujumu uchumi,na kwakuwa walishindwa kuutetea ukweli nao ni sehemu ya uovu,vinginevyo watuombe radhi
nimetafakari hali ya giza na tanesco,na kutoka na uamuzi huu
Sita na mwakyembe hawawezi kamwe kutoka kwenye hili zigo na daima watanzania na wapenda ukweli hatutawasamehe na histori itawahukumu,mtakumbuka kuwa mwakyembe kwa makusudi kabisa alificha ukweli kuhusu kampuni hewa ya richmond kwa kuhofia serikali kuanguka,alidiriki hata kutamka hadharani eti kama angesema yote serikali ingeanguka,ukweli hauwi nusu na kwa mwakyembe kuuficha ukweli amekosa uadilifu na hivyo kupelekea leo taifa kuingia gizani
Sita akiwa spika hakuwatendea haki watanzania kwa kukubali ripoti nusu iliyoficha ukweli na kukubali kufunga mjadala wa richmond
hawa wawili walikuwa na nafasi ya kutosha kuutetea ukweli na leo hii taifa tusingekuwa gizani na uzalishaji ungeendelea
Hawa ni wanafiki,na wahujumu uchumi,na kwakuwa walishindwa kuutetea ukweli nao ni sehemu ya uovu,vinginevyo watuombe radhi