Mwakyembe: Sikusinzia...

Edson,

Usisahau kuwa huyu ni kiongozi wa watu na siyo Prof wa Chuo Kikuu anayefanya kazi yake kimya kimya. Huyu ana watu wakingoja kuona, kusikia na kutiwa moyo kuwa matatizo yao yanashughulikiwa. Maneno ya kutia moyo yanahitajika sana na wa-Tz, lakini pia yakifuatiwa na vitendo vilivyobeba dhamira ya kweli kuwatumikia na kuwathamini.

Hata wewe ukiwa kiongozi watu watataka kukuona unavyotenda na unavyozungumza pia.. Halafu baada ya muda watapima maneno yako na matendo yako kama vinafanana.

Naomba tumpe nafasi kwanza hata kama tunachuki naye kwa sababu zozote zile ....
 


hivi ni utafiti gani unafanyika ukiwa ndani ya tren na wakati huo huo unatafiti hali ya usafiri huku unatafiti pia maeneo treni inakopita na kuona namna watu wa maeneo hayo wakiishi? ...hivi tren hiyo safari mda gani na kufika dodoma mda gani..kama ni usiku vipi aiwezaje kutafiti maisha ya wakazi huko njian? ..alifanya hivyo trni ilipofika kituoni? VUTA-NKUVUTE naomba unisadie kitu mkuu maana uliambatana na mh huko njia...humo ndan ya trni ulimuona zaidi zaidi akijishughulisha na nini huyu mh katika tafiti zake....alitembelea mabehewa yote?..kuna lolote alikemea? ..ulikuwa nae beneti mkuu....yaani safari yenu yote toka dar mpaka dom wewe ulimuuliza/kuulizwa swali hilo tu kuwa ''kwa nini hukulala... kwa nini hakutaja walau kwa uchache yale aliyoyaona huko njian na ndani ya tren??!!.....

bado sana kuna wakati waziri Nundu nae alipanda dala dala tena akiwa amesimama kashika chuma....hivi nae aliwahi kutoa majibu ya huo utafiti au usafiri wa dala dala umeboreshwa???...
 
Nilijuwa kuwa unaweza kuhoji hilo .... lakini si topic ya hii thread. Hata hivyo EN Lowasa ndivyo anavyoitwa. Ndani ya Bunge, vyombo vya habari na serikali. Sasa mimi sijatunga hilo. Mimi pia ninahoji kama wewe, lakini bado heshima hiyo anapewa na huwezi kumpokonya kwa sasa labda uende mahakamani.
 
mkuu naomba utoe hiyo avatar ina to lure tufikiri kwamba unabusara kumbe zero, mwakyembe hajafanya ziara kama za kina lowassa au kikwete yeye kajihusisha kabisa alitaka ayafeel matatizo kabisa. ni kama waziri wakilimo aamue kulima kwa jembe la mkono, ajitafutie mbolea na soko bila shaka atakuja na plan nzuri ya kumkomboa mkulima sasa we ni kubisha hata mtu afanyaje. please badilisha avatar
 
Cha msingi azuie mizigo kuanzia tani 10 ipandishwe kwenye treni ili kulinda barabara lakini hilo litawezekana?!!! maana malori yoote ni ya hao hao mawaziri na WABUNGE!!
 

Wewe unawajibika kumpa heshima hiyo kwa mujibu wa sheria gani? Hii sio heshima ni upotoshaji wa wazi kabisa, ni moja ya namna lugha ya kiswahili inatumika vibaya kwa manufaa ya kisiasa. tuachane na haya. Ila ujue kwamba mategemeo yangu ya kuona ufanisi wa safari ya mwakyembe yanaanzia kwenye bajeti ya wizara yake atakayosoma uko dodoma. usidhani nitapoteza muda wangu kusubiri two years ili kuona matokeo. Hata kama budget zao haziaminiki na hazitekelezeki, lakini nitaitumia kama benchmark ya faida ya safari hiyo.
 
ingeweza kuwa positive, kama asingetoa taarifa, ili aweze kupata hali halisi ya usafiri huo wa wananchi wa kipato cha chini, lakini kwa matangazo aliyofanya sidhani ataweza kuzipata zile kero za muda mrefu.
 
ingeweza kuwa positive, kama asingetoa taarifa, ili aweze kupata hali halisi ya usafiri huo wa wananchi wa walio wengi, lakini kwa matangazo aliyofanya sidhani ataweza kuzipata zile kero za muda mrefu.
 


mkuu tangu umfahamu huyu jamaa hujawahi kupima maneno yake na matendo yake? tangu aanze siasa nchi hii!!!! gimme a break!!!! matatizo yanayowakabili wananchi wakiwa ndani ya treni wanasafiri ni sehemu ndogo sana ya mambo/matatizo yanaoyoikabili sekta hiyo.....labda kama alikuwa anaongeza geographia yake kichwani maana njia ya treni inapita porin na mijin pia...
 
Sangarara, mimi nashangaa hii topic ni outlier ya main topi iliyopo hapa. Siwajibiki kumpa au kumnyang'anya heshima yake anayopewa na watu wengi au wachache. Na sijuwi ni sheria gani inayolazimisha apewe hiyo heshima. Lakini anapewa na watu, tena kila mara vyombo vya habari vinatangaza, na Bungeni pia wanampa, na serikalini pia wanampa...

Kama hukubaliani na hilo tafuta wakili akusaidie kufungua kesi ya zuio la mtu kupewa heshima asiyostahili. Utatusaidia wengi. Lakini utakapokuwa ukikemea watu hapa JF sidhani kama itawafikia walengwa wakubwa, yaani wananchi wanaompa hishima hiyo. Hata hivyo sikuvunji moyo, endelea kujaribu ...
 


sasa wewe mbona unalaumu kabla ya kusikia maelezo ya utafiti wake?
 

Angalia huyu. Kwa hiyo huyu Mwakyembe toka azaliwe hajawahi kupanda treni? Kwamba siku hiyo ndiyo aliyafeel matatizo ya usafiri wa treni? wewe ndio unahoji credibility ya busara zangu? Sasa naamini JF members wengine ni majini.
 
Kwa anayeijua sumu aliyonyweshwa mwakyembe tafadhari, mawaziri wengine wapewe hiyo sumu!
 
Kila research ina limitations ... narrowed down for the sake of achievability
 
sasa wewe mbona unalaumu kabla ya kusikia maelezo ya utafiti wake?
Yaani mimi sangarara nikae kusubiri report ya matatizo ya usafiri wa treni na ugumu wa maisha ya watanzania wanaoishi jirani na reli? kwa raha zipi nilizonazo? kwamba nimekuwa natumia usafiri wa ndege maisha yangu yote? tusitake kuvunjiana heshima, au unadhani mimi ndondocha.
 
kila jambo lina mwanzo wake hakuna ubaya kwa mwakyembe kujiridhisha na mambo yanayoendelea wizarani kwake, ninacho kiona kwako ni hasira zako dhidi yake bila sababu.KAKUKOSEA NINI HATA UMSHUKIE KIHIVYO? naona uhasama wa richmond unaendelea.
 
Tunaamini Dk. Mwakyembe atatushirikisha yote aliyoyaona katika utafiti wake wa Dar es Salaam hadi Dodoma kwa treni.
Asafiri tena kwa treni hadi Moshi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…