Mwakyembe: Maisha yangu yapo hatarini

Status
Not open for further replies.
Kama aliwahi kukana PhD yake hamna namna tumpuuze tu
 
Kuna kitu kinakuja kikubwa,na watanzania tulivyo litatubeba sana
 
Dada yang Joyce, usiichoshe akili yako kwa ajili ya mtu huyu.

Black & white ya bwana huyu ni hii:

Ametoa madai hayo kwa sababu ameshabaini kuwa umma wa Watanzania haupo naye hivyo ameshadharauliwa na amechukiwa sana.

Na hiyo ni kutokana na vitendo vyake vya kinafiki na uzandiki kwa kuusaliti na kuupuza umma.

Hivyo anataka kupata huruma ya wananchi kwa kuamini kuwa akizua hilo alilozua watu watamuonea huruma kama kipindi kile alichodai kupewa sumu.

Ambacho hajiku ni kwamba, wananchi wana akili ya kupambanua mambo na kwamba sio wajinga kama anavyofikiria.

Asituumize Vichwa.
 
" Kwenye serikali yangu, sitaweka wazee.. maana wazee ndo wametufikisha hapa tulipo"..... kuna muda ni bora kunyamaza kuliko kutoa speech
 
Sasa Serikali Yenyewe inaogopa na Mwananchi wa Kaida atasemaje Sasa au Maisha Yake yapo hatarini kivipi c zaidi ya Mwakyembe Sasa?
 
Tusidharau kauli kama hizi kwani mwanzo wa ngoma ni lele na tukumbuke yalishamkuta huyu huyu na akapigania roho yake hakuna aliyejua kama atapona.......huyu ni mtu mkubwa Serikalini hawezi kueleza hovyo hovyo tu jambo kama hili, kifupi hakuna aliye salama kwa sasa.
 
He trying to attract sympathy when all that he has from the people is hate caused by his hypocrisy
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…