ZILLAHENDER MPEMA
JF-Expert Member
- Apr 4, 2015
- 2,055
- 4,245
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]Boss wa Harmo Rapper.....kweli siasa mcheZo mchafu......leo Mwakyembe eti anawahudumu....bongo flava
Hii wizara ni kama shimo la Tewa , Nape chupuchupu kutolewa ubongo kwa bastola , Mwakyembe naye hati hati !
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe amesema maisha yake yapo hatarini, amesema "pamoja na kuwa hawezi kulinganisha miaka saba iliyopita na sasa lakini bado maisha yangu hayako salama."
Akizungmza na Gazeti la MWANAHALISI, Dk Mwakyembe amesema "Siwezi kuwa salama siwezi kuwa naweza kutumia uhuru wangu wa kwenda kokote nikakota au wakati wowote ninaotaka.
"kwamba naweza kutumia uhuru wangu huo kama unavyotakiwa na katiba bado nina hofu ya maisha yangu ingawa siyo kama ilivyokuwa miaka ya mitano iliyopita " ameeleza DK Mwakyembe.
DK Mwakyembe alikuwa ni mmoja wa watu waliotajwa kwenye orodha ya wanaotishiwa maisha.
wengine wanaotajwa kwenye orodhra hiyo ni pamoja na Dr Willibrod Slaa.
kauli ya Dk Mwakyembe imekuja siku tano baada ya watu wasiojulikana kumteka na kumtesa mwanamuziki Ibrahim Musa (Roma Mkatoliki).
Dk Mwakyembe aliwahi kuripoti Februari Mwaka 2011 kuwepo kwa hatari ya kutokomeza maisha yake.
MWANAHALISI
duuuuHii wizara ni kama shimo la Tewa , Nape chupuchupu kutolewa ubongo kwa bastola , Mwakyembe naye hati hati !
Huyu Mwakyembe ukweli wake ni kutiliwa shaka...
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe amesema maisha yake yapo hatarini, amesema "pamoja na kuwa hawezi kulinganisha miaka saba iliyopita na sasa lakini bado maisha yangu hayako salama."
Akizungmza na Gazeti la MWANAHALISI, Dk Mwakyembe amesema "Siwezi kuwa salama siwezi kuwa naweza kutumia uhuru wangu wa kwenda kokote nikakota au wakati wowote ninaotaka.
"kwamba naweza kutumia uhuru wangu huo kama unavyotakiwa na katiba bado nina hofu ya maisha yangu ingawa siyo kama ilivyokuwa miaka ya mitano iliyopita " ameeleza DK Mwakyembe.
DK Mwakyembe alikuwa ni mmoja wa watu waliotajwa kwenye orodha ya wanaotishiwa maisha.
wengine wanaotajwa kwenye orodhra hiyo ni pamoja na Dr Willibrod Slaa.
kauli ya Dk Mwakyembe imekuja siku tano baada ya watu wasiojulikana kumteka na kumtesa mwanamuziki Ibrahim Musa (Roma Mkatoliki).
Dk Mwakyembe aliwahi kuripoti Februari Mwaka 2011 kuwepo kwa hatari ya kutokomeza maisha yake.
MWANAHALISI
Ndiyo nini hiyo fent ford??????Anatafuta kiki huyo,,,,kama vip ajiteke kama Roma ili awe fent Ford mwaka mzima
Unaitwa Bazilio na wewe unakubali???Mwakyembe tunakumbuka na hilo kwa lipo kuwa na tahadhari saana hilo genge ndo lilikufanya uteseke na kuponea chupuchupu pengine ndo linaratibu ya haya mengine kuzichafua serikali nigenge lenye njia chafu sana
Muulize Mh.Six anajua zaidi nilimnukuu tuu moja ya kauli zakeKwani alishawahi pewa sumu? labda haikuklea
Kwa kweli inatisha! Hizi kauli zake hizi!Ile sumu ya KGB polium tayari imeshatafuna ubongo wa Mwakyembe na umeoza, amejaa funza tu kichwani.
Mkuu umeandika kwa uchungu sana nilijua nipo kwenye matatu nimuombe konda nishuke nichukue matatu nyingineWakati yeye ana hofu juu ya mambo yasiyooneka,hofu ya kusadikika,wenzake tupo kwenye hofu halisi,hofu ya kutojua hatima yetu,hofu inayoyaweka maisha yetu rehani.Hatuna uhakika kesho yetu itakuwaje,hofu ya ugumu wa maisha.
Mtu anayerishwa na kulindwa kwa kodi zetu yeye pamoja na familia yake,anapokuja na kutuambia kuwa maisha yake yapo hatarini ni dhihaka kwetu tunaomtunza na kumlinda kwa mapato ya jasho letu.
Yeye ni nani kwetu,fursa alizonazo katika nchi hii hazijawahi kuwa msaada wowote kwetu,alitangulizwa mbele katika sakata la Richmond,akafanikiwa kuuhadaa umma wa watanzania kuwa alikuwa anapigana kwa niaba yetu,kumbe alikuwa anapigana kwa niaba ya tumbo lake na la wale waliomtuma,ndiyo! Yalikuwa ni mapambano juu ya vyeo!
Miaka 9 baada ya yeye kutumika kupigania tumbo lake na la wale waliomtuma,ameuthibitisha unafiki wake pale alipoidharau lipoti ya Nnape iliyowasilishwa Na timu aliyoiunda ili kumchunguza "mwana mfalme" katika kadhia ya kuvamiwa kwa Clauds.Mwakyembe aliita ripoti ile kuwa ni ripoti ya upande mmoja na hivyo imepoteza sifa eti kwa sababu haikumuhoji mkuu wa mkoa,ingemuhoji vipi wakati timu ile ilipofika ofisini kwa mkuu wa mkoa,mkuu huyo aliitoroka timu ile kwa kupitia dirishani?
Hoja kwamba timu ya uchunguzi iliyoundwa na mtangulizi wake kuwa imekosa weledi kwa sababu haikumuhoji Makonda,ilikuwa ni kejeli kwetu.Akiwa Mwenyekiti wa kamati teule ya bunge iliyoundwa ili kuuchunguza mkataba tata wa Richmond,kamati yake ilisafiri hadi"Ulaya" kwenda kuutafuta ukweli kuhusu Richmond,lakini ilishindwa kwenda kumuhoji Mh.Lowassa aliyekuwa mita chache sana pale Magogoni DSM.
Hata kama kamati teule ilikuwa imechoka kutembelea magari yenye viyoyozi kwenda kumuhoji Mh.Lowassa,tulikuwa radhi kuwabeba mgongoni wajumbe wa kamati teule ili wafike Ofisi ya Waziri mkuu pale Magogoni wakamuhoji na kutuletea ukweli juu ya uhusika wake katika sakata la Richmond.Lakini kwa sababu anazozijuwa yeye na wale waliomtuma,hakwenda kumuhoji Mh.Lowassa,badala yake walitumia kodi zetu kwenda kuzurura Ulaya eti wanatafuta uhusika wa Mh.Lowassa katika sakata la Richmond.
Asijaribu kuuhadaa umma uliokwisha mpuuza,hofu yake juu ya usalama wake ni matokeo ya siasa zake chafu,ni zao la unafiki wake na kutumika kwake kuwaangusha wenzake.Aache kukikimbia kivuli chake,kivuli hakikimbiwi kitaenda naye sambamba kwa spidi ileile anayoitumia yeye kukikimbia kivuli chake.
Maisha yake kuwa hatarini ni hoja ya kipumbavu zaidi ya upumbavu wa kiwango cha PhD ya maganda ya korosho!Hatari ipi inayomnyemelea na kwa lipi hasa?Ni jambo gani alilolisimamia hadi astahiri huruma yetu?Kama alilikana hadi andiko lake mwenyewe lililompa Permanent head Disorder(PhD),tunaanzia wapi kumuamini mwanasiasa huyu mchumia tumbo mwenye rangi nyingi zaidi ya kinyonga?Hakuna atakayeishi milele,sote tutakufa hivyo kama "ananyemelewa na kifo" afe tu nasi tutamfuata pale zamu yetu itakapofika.Aache siasa za kipumbavu na kilaghai.