Mwakyembe hali tete Jimboni kwake Kyela

Mwakyembe hali tete Jimboni kwake Kyela

kilght

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2012
Posts
635
Reaction score
182
Mbuge wa Kyela bwana Harrison Mwakyembe mambo yanamwendea kombo jimboni kwake. Juzi alizuiwa kwa Mawe na magogo na wanaichi wa Kyela na gari yake kumwagiwa pombe huku wakipiga kelele kuwa hawamtaki tena kwa kushindwa kutekeleza hata robo ya ahadi alizozihaidi siku za kampeni .

Alihaidi kiwanda cha juisi za embe na chungwa, meli ,kiwanda cha kugred mchele,barabara ya lami toka Kyela hadi Matema.

Chanzo mimi mwenyewe
 
Amelaaniwa tayari sijui atajificha wapi. Hawa jamaa wana roho mbaya hawana huruma na maisha magumu kwa watanzania. Bila aibu wanakuja kuomba kura tena
 
one time niliendaga kyela...maneno nikiyoyasikia toka kwa wananchi kule....dah, mwakyembe ajipange sana 2015. Chadema wanafanya vizuri sana kule jimboni kwake
 
Wananchi walimuhurumia alipolishwa sumu, wakajua atajipambanua kumbe hakuna kitu
 
Duuu mwakyembe ana hali mbaya sana kyela yaani ukitamka mwakyembe au ccm lazima utukanwe na unaweza kupigwa niko kyela kwa wiki sasa
 
Hata mwaka 2010 alipata kura za ulaghai. Ilikuwa akiwa kwenye mikutano yake ya kampeni, wananchi wakimwuliza mfano "Sisi hapa tunatatizo la maji...." anachojibu ni kwamba, tayari ameshaongea na waziri wat maji na mradi wao ni kipaumbele cha serikali. Halfu anaweka simu kwenye laud speaker, anawaambia wasikilize akiongea moja kwa moja na waziri mwenye dhamana. Anaanza kusema, "Hallo mheshimiwa, niko hapa nyumbani, wananchi wangu wanaomba kufahamu suala la maji limefikia wapi, naomba useme moja kwa moja waskisikia", . Sauti ya upande wapili inasema, "waambie wasiwe na wasiwasi, tayari nnimeshatoa maelekezo na mkandarasi.....blah blah..... atakuwa hapo kuanzia tarehe.....", . Mwakyembe angesema mmesikia wenyewe? Wapiga kura wake wangeitikia "Ndiyooooooooo!:.

Sehemu moja sauti ya pili ilijibu "Tayari vifaa vya ujenzi wa hilo daraja vimeshapakiwa kwenye magari vinakuja...".

Mara waziri wa ujenzi angejibu kwenye hiyo simu " Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami uko katika budget yetu na mwezi wa kwanza unaanza rasmi huko".

Mwakyembe ni mafia. Safari hii atapanga mawaziri wa kwenye simu waseme nini tena? Mtaji wa uowongo wake umebuma kyela.
 
Siku ya uchaguzi nilipita Kyela mjini nikielekea Matema kikazi, jambo lilonishangaza pale mjini ni jina jipya alilobatizwa Mwakyembe na wana Kyela DALALI, kwao Mwakyembe ni dalali...Hawataki hata kumsikia...

Nilipita baadhi ya vijiji nikakuta mitaro ya kutandaza bomba za maji, nikawauliza swali chokonozi: Huyu mtu na chama chake wanawaletea maji ajabu hamumtaki hivi ni uungwana kweli !? Jibu: Hili ni changa la macho na hata maji yakitoka siku moja kabla ya uchaguzi bado hatudanganyiki...
KERO KUU:
1) Barabara ya njiapanda boda mpaka Itungi Port kujengwa chini ya kiwango
2) Barabara ya njia panda ya Ipinda 3km ilikamilika mwaka jana mwaka huu imebandikwa viraka...
3) Mtandao wa cm ktk vijiji vingi ni wa taabu...
4) Ametoa gari aina ya Noah kama ambulance hospitali ya wilaya...

Tanbihi:
Nimeeleza matatizo/kero walizokuwa wanazitoa baada ya uchaguzi

Tafakari...
 
Juzi kati kuna mtu alimzungumzia Mh.Mbowe kuwa nae hali yake si nzuri ktk Jimbo lake,ila watu wakaeleza kwamba yuko busy na kukijenga chama. sasa leo huyu Mh.Mwakyembe ambaye ni mbunge na ni waziri, ila kwa kua yeye ni ccm basi anaonekana ni walewale tu mafisadi tu.
 
Uwaziri huwa unapofusha Sana. Mwakyembe kabadilika!!!!! sikutegemea matusi aliyokuwa akitukana mafisadi Leo anaweza geuka na kuwa sehemu ya mafisadi pale BANDARINI......

Inawezekana kelele za akina mwakyembe na Sitta zilikuwa ni vilio vya WIVU tu.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom