Mwakyembe anvyowahadaa Watanzania

ili tuendelee tumuhitaji sana Mwakyembe. Kama wewe humpendi jiunge na wenzako mkamtafutie sumu nyingine
 
Pole mkuu,ila hasira zako peleka hukohuko,Katumia sh ngapi Tanga kwani!Vipi nauli ya VIP ya mtu mmoja kwenda london na kurudi haijatosha kuhudumia kikao hicho!Hivi bandari iko DSM tu!Mie ningeshangaa kama kazindulia Dodoma!Acha utoto yaani umejiunga juzi humu baada ya kufukuzwa kazi bandarini ili upate pa kusemea!maana tarehe za kuja kwako ni kipindi cha timua timua ya mwakyembe!Kalghabaho
 
Nipisheni naona chuki binafsi dhidi ya Mwakyembe haikwepeki kwenye kauli zako.
Vp, kwani kuna ubaya gani ukijiongezea nauli kisha usafiri na business class?

Tatizo la binadamu ni ubinafsi tu. Hakuna tofauti yoyote kati ya Business Class na Economy. Halafu kama mtumishi kama abiria mwingine ataweza kuongezea nauli kutoka Economy na kuwa Business class kwani Dr. Mwakyembe amekataa? Tabu ni pale unapotaka kuibebesha Serikali mzigo bila sababu. Kama hujawahi panda ndege nikufahamishe tu kuwa baada ya Rubani inafuata First Class ambayo mara nyingi huwa ni kagorofa kanakuwa juu harafu inafuata Business then Economy lakini wote mnapanda kwa pamoja, mnashuka kwa pamoja na ndani ya ndege mnahudumiwa kwa pamoja.

Kwamfano; Tofauti ya Business Class na Economy kwa route moja inaweza kuanzaia Tshs. 150,000/= hadi Tshs. 400,000 japo inapanda kulinga na Destination.
 
Mh, Mwakyembe anajitahidi kuwa mbunifu lkn anachokifanya kinategemea zaidi huruma ya wananchi na yupo kisiasa zaidi kuliko utendaji, na hapo ndipo anapoweza kuingia mgogoro wa chinichini na wasaidizi wake wizarani na kuonekana kuwa amri yake imepuuzwa au amedharauliwa.

Maana kuna ngazi na madaraja ya watumishi hadhi zao za usafiri zinatofautiana kati ya vyeo na vyeo mf; si kila kiongozi anatembelea landcruiser GX kama alilonalo yeye MWAKYEMBE na ndiyo maana amri ya waziri mkuu imepuuzwa kwa kuwa hadhi ile iko kisheria , hivyo nia nzuri ya mh, Mwakyembe asimamie marekebisho ya sheria kwanza ,vinginevyo ataingia mgogoro na wasaidizi wake, kisha aje kwa wananchi kutaka huruma yetu jiulize lile suala la askari wa kova liliishia wapi? si alimpa amri kova ,ilitekelezwa?

Jamani, tusishabikie matamko ya kisiasa.

MWISHO: ATC itafufuka? tuelezwe ukweli nawadokeza tu, ina madeni ya kufa mtu, maneno ya kisiasa yanapendeza masikioni lkn maneno ya watendaji utatamani ulie.
 
Waziri huyu ambae amekua na tabia ya kujipatia misifa,hivi karibuni amezuia watumishi waliopo chini ya wizara hiyo wasipande daraja la kwanza wanapo safiri na ndege kwa tafsiri kwamba watanzania wengi bado ni maskini.

Mwakyembe angekua mkweli wa kutaka kusaidia watanzania asingekwenda kuzindua bodi yake mkoani Tanga.Akae atafakari ni kiasi gani cha fedha kingeokolewa kama kazi hiyo ingefanyika Dar es salaam.Gharama iliyotumika kuzindua bodi yake ingetosha kabisa kununulia madawa ya zahanati tatu katika jimbo lake na badala yake anatoa amri za kitoto kwa watanzania kwamba yeye ni mzalendo.

:pop2: :laser:wewe una matatizo ya akili na inaonekana unachuki binafsi na Mwakyembe....aidha wewe ni miongoni mwa wale wanaoguswa na mpiganaji huyu... sasa usiwachafue wa Tanzania.... WATANZANIA walio wengi siku hizi hawadanganyiki.... wanaelewa mbivu na mbichi.... unapoongea tumia busara na utafakari unaongea nini......kwani wanaowafahamu viongozi watendaji wazuri wa nchi hii ni wachache......mmoja wao ni Mwakyembe..... mwache afanye kazi za kutumikia wananchi...
:majani7: :target::A S 100: :cheer2:
 
waziri huyu ambae amekua na tabia ya kujipatia misifa,hivi karibuni amezuia watumishi waliopo chini ya wizara hiyo wasipande daraja la kwanza wanapo safiri na ndege kwa tafsiri kwamba watanzania wengi bado ni maskini.

Mwakyembe angekua mkweli wa kutaka kusaidia watanzania asingekwenda kuzindua bodi yake mkoani tanga.akae atafakari ni kiasi gani cha fedha kingeokolewa kama kazi hiyo ingefanyika dar es salaam.gharama iliyotumika kuzindua bodi yake ingetosha kabisa kununulia madawa ya zahanati tatu katika jimbo lake na badala yake anatoa amri za kitoto kwa watanzania kwamba yeye ni mzalendo.

kafie mbali
 
kweli kuna kila dalili za chuki binafsi; kuna watu kweli wanafafanya kazi ambazo tunaziona; lini ulitegemea kuona usafiri wa train dsm; watu wanaoweza kufanya maamuzi sahihi ni adimu na ndio tunaowahitaji tz hii bila kujali itikadi zetu; kama unaongelea habari ya madawa ya hospitali, unaijua bajeti ya wizara ya afya ww, kwanini wao hawajafanya hivo kama umeona kuna mapungufu; na kama kweli kuna mapungufu huku wizara ya afya kwanini wao wasiombe kwa wizara ambazo zina ahueni; pia wajua waliohudhuria huo uzinduzi wanatokea wapi; je waufahamu kiasi gani na bandari zingine ikiwemo hiyo ya tanga ambako uzindizi ulifanyika? tuache fitina tujadili masuala yanayoweza kututoa hapa kwenda mbele zaidi
 
Amewabana sasa Mnabwabwaja tu kama vichaa, na bado Mwakyembe atawanyoosha mpaka mtie akili, kwani kwenda Tanga shida iko wapi?!! Tanga sio Tanzania au?!! nani asiejua matatizo ya mji wa Dar hasa usafiri, so Tanga ilichaguliwa ili mkutano uwe na Utulivu...
 
Huna hoja. Labda uliandika kwa haraka. Jipange halafu rudi hapa na maelezo yaliyonyooka.
 
Amewabana sasa Mnabwabwaja tu kama vichaa, na bado Mwakyembe atawanyoosha mpaka mtie akili, kwani kwenda Tanga shida iko wapi?!! Tanga sio Tanzania au?!! nani asiejua matatizo ya mji wa Dar hasa usafiri, so Tanga ilichaguliwa ili mkutano uwe na Utulivu...

Mwakembe hajawahi kuwa mpambanaji.Ni opportunist 100% nothing else.
 
wazee wa bandari mmebanwa mbavu lazma nyumba ndogo ziwakimbie safari hii
 
Lazima mkae safari hii!Tatizo wabongo mnapenda sana starehe kuliko kazi yaani kwani ukikaa daraja la 3 hutafika?
Mbona sasa hivi garimoshi kuelekea/kutoka Kigoma ni daraja la TATU tuu wakati kabla ya RITES palikuwa na madaraja ya PILI na KWANZA vilevile garimoshi la Mwanza lilikuwepo!:confused2::confused2:
 
Lazima mkae safari hii!Tatizo wabongo mnapenda sana starehe kuliko kazi yaani kwani ukikaa daraja la 3 hutafika?

Mandingo me sijawah kupanda ndege,kwani daraja la 3 wanakaa kwenye tela?,wanapigwa na jua?ni siti ya mwisho?,wanakaa kwenye mabawa ya ndege?,wanakaa ndani ya injini au?hao wanaong'ang'ania la kwanza nani kawaambia kuwa wao ni spesho kwa la kwanza?,na je wao wanawah kufika?,wanaruhusiwa kwenda kuchimba dawa?,wanafungua madisrisha?,au?????
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom