Mwakyembe anasikitisha! Walaaniwe wanaohusika!

Mwakyembe anasikitisha! Walaaniwe wanaohusika!

kama ni kweli amekuwa poisoned god will pay them.
Siyo rahisi kwisha bure itawarudia.
Mkweli amekuwa mbaya ng mbaya amekuwa mzuri.aibu kwao.
 
Na kama walivyokataa kuwa na
Mungu katika fahamu zao,
Mungu aliwaacha wafuate akili
zao zisizofaa, wayafanye
yasiyowapasa.
Warumi 1:28.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Ugua pole Mwakyembe. Siasa za bongo zina shaka sana. Naamini mwenye kutoa uhai na kuuchukua ni mungu pekee. Haya nayo yatapita
 
mwakyembe anateseka sana juu ya wahuni wachache waliomchezea mchezo mchafu-naomba apate nguvu na arud as normal na ataje hao wahusika wote,ila kama ni noma iwe noma tu-vengance lazima ifanyike juu ya hao wabaya wa mwakyembe
 
Kwa hili la Mwakyembe ni kuapply sheria za torati tuu.Jino kwa jino,jicho kwa jicho,poison kwa poison kusubiri Mungu awaadhibu watatamba sana.
 
ninachojua huyu bwana harudi kama alivyokwenda.......ana bahati maana hata ile dawa ya meno aliyopelekewa kama zawadi huko india hakuitumia maana tungekwa tunaongea mengine kabisa mda huu.....shukrani ziwaendee vjana wanaomtakia memo waliofikisha habari kabala box la dawa hiyo halijafika

Mkuu hapana. JF hatuendi hivyo. Hii imekaa kinadharia/ndoto zaidi.
 
He will not die..not this time he will live to the full of his age ili atangaze matendo makuu Mungu aliyomtendea na pia ku expose kazi za ibilisi kupitia agents wake. For this wala sina hata wasi wasi maana najua yule alyeniita kamwe hawezi nidanganya kwani hajawahi fanya hivyo.
 
Kwa sababu tumesimama upande wa haki tutashinda. Neno la Mungu linasema punje isipodondoka kwenye mchanga kufa na kuoza, haiwezi kuzaa kitu. Mwakyembe anaweza kuwa punje

Kafara aliyotoa Yesu pale msalabani inajitosheleza na Mwakyembe ni beneficiary so kwaajili ta Taifa hili na kwakua kwanafasi yake alitenda kwa wema basi sisi tumeomba na kwaajili ya sisi hatakufa ataishi ili furaha yetu iwe tele.
 
Kama ni kweli ni sumu, wahusika wanajulikana. Kwa nini hawaguswi?

Wewe umejuaje wahusika wanajulikana?
Kama unawajua wataje hapa nasi tujue. Halafu, is it really confirmed ya kwamba amepewa sumu? Tena sumu hizo hapo juu au ni tetesi tuu hizi?

Tujuzane kiukweli jamani
 
wakuu mwenyekuweza kuweka picha basi hata kama kupiga picha ktk hilo gazeti kwa simu tafadhali
wakuu huku moshi hatujapata magazeti hajui ni kwa nini wauza magazeti walikuwa wanauza ijumaa tafadhali tuwekeeni tuione
 
Wewe umejuaje wahusika wanajulikana?
Kama unawajua wataje hapa nasi tujue. Halafu, is it really confirmed ya kwamba amepewa sumu? Tena sumu hizo hapo juu au ni tetesi tuu hizi?

Tujuzane kiukweli jamani

hebu soma thread yote vizuri utapata uchunguzi mzima
 
Mungu wetu ni mkubwa,anaweza yote yeye ni mponyaji. Haki na ukweli wake unadumu milele. Watesi wa watu wake atawalipa staili yao hapa duniani na hata mbinguni. Yeye ni Mungu wa haki na ufalme wake unadumu milele.
 
Wewe umejuaje wahusika wanajulikana?
Kama unawajua wataje hapa nasi tujue. Halafu, is it really confirmed ya kwamba amepewa sumu? Tena sumu hizo hapo juu au ni tetesi tuu hizi?

Tujuzane kiukweli jamani

Kwa hiyo wewe kwa hali unaiyoina kwenye picha unadhani anaumwa malaria??!!!!. Fanya utafiti kwa watu walikaribu na wewe au jirani zako kama yupo anayeonekana kama Mwakyembe kwa jinsi alivyoonekana kwa sasa. Kwa utafiti huu mdogo tu kabla wa kidaktari ndio utajua Mwakyembe kapewa sumu. Kinachotafutwa hapa ni kujua ni sumu ya aina gani na nani hasa aliinitiate hiyo move. Ukifuata series ya matukio toka Mwakyembe alivyolalamika polisi kuwa kuna kikundi kinampango wa kumuuwa, haipaswi kuwa mganga wa kienyeji ndio upate kujua kuwa Mwakyembe kapewa sumu
 
Nilisema awali na kutoa mifano ya Daud Ballali. Alitoa vitisho na kutengeneza video, na kugawa copies kwa watu at least wanne. Haya hatimaye yakutokea, yakatokea na sasa yeye yuko six feet under. Wenye nakala za video wanakula bata, pasi na shaka. Mchezo ni ule ule.

Kuna msemo wa mitaani, nikanyage kwa bahati mbaya nikulipue kwa makusudi. Naona kuna watu wamekanyagwa kwa bahati mbaya, sasa wanafanya kweli.
 
Inasikitisha sana jamani! watu wanakosa utu na hofu ya Mungu kwa ajili ya madaraka! ni maombi yangu kwa Mungu kuwa apone na arejeshewe afya yake,wenye hila waaibishwe,Mungu anafanya njia pasipo na njia namuombea uponyaji.
 
Jamani Yesu anaponya tumuombee kwa iman atapona kama Lazaro alikufa na akarudishiwa uhai iweje mheshimiwa mh!!! Kweli madaraka matamu ukiwaona kwny nyumba za ibada wanavyonyenyekea huwadhanii kama ni wauwaji wakubwa na je how many people do they going to kill?
 
<div style="display:none;"> <img src="//pixel.quantserve.com/pixel/p-95EVqn2X8Y6XI.gif" border="0" height="1" width="1" alt="Quantcast"/> </div>




<div style="display:none;"> <img src="//pixel.quantserve.com/pixel/p-95EVqn2X8Y6XI.gif" border="0" height="1" width="1" alt="Quantcast"/> </div>
 
Back
Top Bottom