Viol
JF-Expert Member
- Dec 15, 2009
- 25,419
- 18,368
Kiongozi wa Majeshi ya Kulinda Amani Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo(DRC), Meja Jenerali,James Mwakibolwa amesema kwa sasa wanasubiri amri ya Umoja wa Mataifa waweze kutekeleza majukumu yao Mashariki mwa nchi hiyo.
Majeshi ya kulinda amani ya Tanzania tayari yako kwenye mji wa Goma, Mashariki mwa DRC pamoja yale ya Afrika Kusini. Majeshi ya Malawi bado hayajaingia DRC chini ya mpango huo wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa, Monusco.
"Bataliani zote ziko tayari kwa mapambano, tumeshajipanga, zana zote ziko tayari, bado tu silaha ndogondogo...wanajeshi wote wako tayari kuanza kazi. Tunachosubiri ni amri ya UN tuanze kukabiliana na waasi," alisema Mwakibolwa akizungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza, BBC.
Alisema kuwa pamoja na kwamba waasi wa March 23 (M23) wameanza mashambulizi kukabiliana na majeshi ya Serikali ya DRC, wao hawajaanza kazi kwa kuwa hawajapewa amri kamili ya kupigana pamoja na kunyang'anya silaha.
Mwakibolwa ambaye ni mpiganaji kutoka Tanzania, alisema kuwa wanajeshi wote kutoka Tanzania wako salama na hakuna hata mmoja ambaye ametekwa wala kuumizwa na wanaendelea na mazoezi ya kivita pamoja na wenzao wa Afrika Kusini. Alisema Majeshi ya M23 yanapenda kuzusha mambo kuwateka kisaikolojia wapinzani, lakini wameshafahamu mbinu hizo.
UN imepanga kutumia vikosi vya askari 3,100 Mashariki mwa DRC katika mji wa Goma na vitongoji vyake kwa ajili ya kulinda amani.
Source; Mwananchi
Majeshi ya kulinda amani ya Tanzania tayari yako kwenye mji wa Goma, Mashariki mwa DRC pamoja yale ya Afrika Kusini. Majeshi ya Malawi bado hayajaingia DRC chini ya mpango huo wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa, Monusco.
"Bataliani zote ziko tayari kwa mapambano, tumeshajipanga, zana zote ziko tayari, bado tu silaha ndogondogo...wanajeshi wote wako tayari kuanza kazi. Tunachosubiri ni amri ya UN tuanze kukabiliana na waasi," alisema Mwakibolwa akizungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza, BBC.
Alisema kuwa pamoja na kwamba waasi wa March 23 (M23) wameanza mashambulizi kukabiliana na majeshi ya Serikali ya DRC, wao hawajaanza kazi kwa kuwa hawajapewa amri kamili ya kupigana pamoja na kunyang'anya silaha.
Mwakibolwa ambaye ni mpiganaji kutoka Tanzania, alisema kuwa wanajeshi wote kutoka Tanzania wako salama na hakuna hata mmoja ambaye ametekwa wala kuumizwa na wanaendelea na mazoezi ya kivita pamoja na wenzao wa Afrika Kusini. Alisema Majeshi ya M23 yanapenda kuzusha mambo kuwateka kisaikolojia wapinzani, lakini wameshafahamu mbinu hizo.
UN imepanga kutumia vikosi vya askari 3,100 Mashariki mwa DRC katika mji wa Goma na vitongoji vyake kwa ajili ya kulinda amani.
Source; Mwananchi