Mwakalebela ashinda tena,Takukuru Waumbuka !

Rutunga M

JF-Expert Member
Mar 16, 2009
1,769
1,382
Chanzo blog ya Francis Godwin,Iringa

MAHAKAMA ya hakimu makazi mkoa wa Iringa kwa mara ya pili imemwachia huru aliyekuwa mshindi wa kura za maoni ndani ya chama cha mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 Frederick Mwakalebela na mkewe Celina baada ya kuonekana hawana kesi ya kujibu katika shitaka lililofunguliwa na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Iringa.


Mwakalebela na mkewe walifikishwa kwa mara ya pili mahakamani hapo na Takukuru baada ya kushinda kesi hiyo kwa mara ya kwanza miezi miwili iliyopita kabla ya Takukuru mkoa wa Iringa kuifungua upya kesi hiyo ya kuwakamata kwa mara ya pili watuhumiwa hao.



Hakimu wa mahakama hiyo Mary Senapee alisema kuwa mahakama hiyo inawaachia huru watuhumiwa hao kutokana na kutokuwa na kesi ya kujibu katika shitaka hilo la rushwa lililofunguliwa na Takukuru na kuitaka Takukuru kama haijaridhika kukata rufaa.



Mwakalebela na mkewe walifikishwa mahakamani hapo na Takukuru kwa kosa la kutoa rushwa ya shilingi 100,000 kinyume na sheria ya kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 kifungu cha 15(1)(b) kinachokwenda sambamba na sheria ya gharama za uchaguzi namba 6 ya mwaka mwaka 2010 kifungu namba 21 (1) (a) na kifungu cha 24(8).



Takukuru kupitia mwendesha mashtaka wake Imani Mizizi ilidai kuwa Juni 20, mwaka jana mshitakiwa Mwakalebela alidaiwa kutoa hongo ya sh. 100,000 kwa mwenyekiti wa kijiji cha Mkoga ,Hamis Luhanga ili awagawie wajumbe wa CCM 30 ambao waliitwa kwenye kikao hicho cha kujipanga kushinda kura za maoni CCM huku akitambua wazi kufanya hivyo ni kosa .


Hata hivyo kesi hiyo ambayo ilionyesha kuwa na mvuto zaidi kwa wakazi wa mkoa wa Iringa ambao walifika mahakamani hapo kutaka kujua hatma ya kesi hiyo ,imekuwa ni kesi ya aina yake na kupelelea ndugu kutoka kwa shangwe zaidi katika mahakama hiyo kutokana na TAKUKURU kuendelea kubwagwa mahakamani .



Mwandishi wa habari hizi alishuhudia ndugu na marafiki wa karibu wa Mwakalebela wakiondoka mahakamani hapo kwa furaha kubwa huku wakimpongeza Mwakalebela na mkewe kwa kushinda katika kesi hiyo tena.



Katika kesi hiyo Mwakalebela na mkewe Celina walikuwa wakitetewa na wakili wa Basil Mkwata ambaye aliwasilisha pingimizi la awali la kisheria ukiomba kesi hiyo iondolewe mahakamani kutokana na mapungufu ya kisheria yaliofanywa na upande wa mashitaka kabla ya Takukuru kuendelea kung’ang’ania kuendelea na kesi hiyo​
 
Rutunga

Sahihisha heading ya thread : BREAING NEWS.. Although hii pia ilishakuwa posted hapa JF kama NEWS!
 
Hivi alikuwa na kesi? haya ni mamichezo ya wanasiasa wanamaliza tu stationary za mahakama.
 
Kulikuwa hakuna kipya kwani tangu mwanzoni alikubali kuvunja makundi na kumuunga mkono aliyepitiswa na kina Magamba. Angelikuwa alikataa, angekiona cha moto, leo angekuwa ananyea debe. Kwa ujumla ukipata jibu la Swali kwanini hakuna yeyote aliyekamatwa kwa makosa ya rushwa baada ya mchakato wa kura za maoni ccm, wakati kura zilikuwa nje nje, basi utapata jibu kuwa hizi kesi zitakuwa na maana tu ya kuwakomoa wale waliokwenda nje na ccm baada ya kuenguliwa na kukataa kuwaunga mkono.
 
Acha kupoteza muda kufuatilia hizi kesi, hakuna kesi hata moja ambapo mgombea wa ccm aliyekamtwa anatoa rushwa na takukuru atayefungwa kwani hii ilikuwa set up tu ya takukuru lakini hamna lolote kwani takukuru ni taasisi yao wao ndio wanaicontrol. kesi hii ya uchaguzi ya iringa mjini mwakalebela hawezi kushinda endapo takukuru isingekubali kutumiwa kwani mwakalebela alikamatwa live na mkewe wakigawa rushwa mkutanoni na video zipo, mama sitta alikamatwa usiku wa manane akigawa rushwa tena mtego uliowekwa na takukuru wenyewe mpaka leo kimya jiulize why? na yule mama aliyekuwa mkuu wa wilaya kule moshi alikamatwa hotelini amejifungia na watu akiwagawia bahasha zenye pesa ndani lakini mpaka leo hii kimya. wahusika wote hawa rais akiwa ziarani mikoani mwao utawaona waki chat na rais. in my opinion takukuru should have been abolished longtime to save taxpayers money to be spent on failed institution like Takukuru.
 
Ukweli unapopita uongo hujitenga, Takukuru na ccm yao wameumbuka!
 
Kulikuwa hakuna kipya kwani tangu mwanzoni alikubali kuvunja makundi na kumuunga mkono aliyepitiswa na kina Magamba. Angelikuwa alikataa, angekiona cha moto, leo angekuwa ananyea debe. Kwa ujumla ukipata jibu la Swali kwanini hakuna yeyote aliyekamatwa kwa makosa ya rushwa baada ya mchakato wa kura za maoni ccm, wakati kura zilikuwa nje nje, basi utapata jibu kuwa hizi kesi zitakuwa na maana tu ya kuwakomoa wale waliokwenda nje na ccm baada ya kuenguliwa na kukataa kuwaunga mkono.

Mhhhhhm! A case of better devil you know................???????????:mod:
 
mbuzi nimbuzi hawezi kuwa simba!!!!!!!
Membe alisema, 'pesa hiyo ya FIDIA YA RADA KUTOKA( BAE )sio ya watanzania, ni ya tanzania.!!!'...........................Usually
when people are sad they don't do anything they just CRY over their
condition but when they gel Angry they bring about a change" (MALCOLM X)
.
 
Mtoto kaa hapa nikirudi nitakuletea pipi, umesikia. Haya baki!
Hizi kesi zinasikika kama uongo huo wa wazazi kwa watoto wao.
Wazazi ni serikari inayoongoza ya magamba, na watoto ni watanzania wenye taabu na shida nyingi, wakiahidiwa kila uchao na ahadi ambazo serikari ina uhakika 100% haitazitekeleza ng'o.
 
Chanzo blog ya Francis Godwin,Iringa

MAHAKAMA ya hakimu makazi mkoa wa Iringa kwa mara ya pili imemwachia huru aliyekuwa mshindi wa kura za maoni ndani ya chama cha mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 Frederick Mwakalebela na mkewe Celina baada ya kuonekana hawana kesi ya kujibu katika shitaka lililofunguliwa na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Iringa.


Mwakalebela na mkewe walifikishwa kwa mara ya pili mahakamani hapo na Takukuru baada ya kushinda kesi hiyo kwa mara ya kwanza miezi miwili iliyopita kabla ya Takukuru mkoa wa Iringa kuifungua upya kesi hiyo ya kuwakamata kwa mara ya pili watuhumiwa hao.



Hakimu wa mahakama hiyo Mary Senapee alisema kuwa mahakama hiyo inawaachia huru watuhumiwa hao kutokana na kutokuwa na kesi ya kujibu katika shitaka hilo la rushwa lililofunguliwa na Takukuru na kuitaka Takukuru kama haijaridhika kukata rufaa.



Mwakalebela na mkewe walifikishwa mahakamani hapo na Takukuru kwa kosa la kutoa rushwa ya shilingi 100,000 kinyume na sheria ya kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 kifungu cha 15(1)(b) kinachokwenda sambamba na sheria ya gharama za uchaguzi namba 6 ya mwaka mwaka 2010 kifungu namba 21 (1) (a) na kifungu cha 24(8).



Takukuru kupitia mwendesha mashtaka wake Imani Mizizi ilidai kuwa Juni 20, mwaka jana mshitakiwa Mwakalebela alidaiwa kutoa hongo ya sh. 100,000 kwa mwenyekiti wa kijiji cha Mkoga ,Hamis Luhanga ili awagawie wajumbe wa CCM 30 ambao waliitwa kwenye kikao hicho cha kujipanga kushinda kura za maoni CCM huku akitambua wazi kufanya hivyo ni kosa .


Hata hivyo kesi hiyo ambayo ilionyesha kuwa na mvuto zaidi kwa wakazi wa mkoa wa Iringa ambao walifika mahakamani hapo kutaka kujua hatma ya kesi hiyo ,imekuwa ni kesi ya aina yake na kupelelea ndugu kutoka kwa shangwe zaidi katika mahakama hiyo kutokana na TAKUKURU kuendelea kubwagwa mahakamani .



Mwandishi wa habari hizi alishuhudia ndugu na marafiki wa karibu wa Mwakalebela wakiondoka mahakamani hapo kwa furaha kubwa huku wakimpongeza Mwakalebela na mkewe kwa kushinda katika kesi hiyo tena.



Katika kesi hiyo Mwakalebela na mkewe Celina walikuwa wakitetewa na wakili wa Basil Mkwata ambaye aliwasilisha pingimizi la awali la kisheria ukiomba kesi hiyo iondolewe mahakamani kutokana na mapungufu ya kisheria yaliofanywa na upande wa mashitaka kabla ya Takukuru kuendelea kung'ang'ania kuendelea na kesi hiyo​

Kwani takukuru ni kitu gani, na inafanya nini, mbona immempeleka huyo mahakamani, hivi na yenyewe inaweza kumpakazia mtu? na yenyewe inakula rushuwa, nisaidieni wana JF.:smow:
 
Kwani takukuru ni kitu gani, na inafanya nini, mbona immempeleka huyo mahakamani, hivi na yenyewe inaweza kumpakazia mtu? na yenyewe inakula rushuwa, nisaidieni wana JF.:smow:

TAKUKURU inakula rushwa kama kawa. Hatua ya kuwabambikia watu kesi wakati wa uchaguzi ilikuwa ni sehemu ya rushwa ambazo TAKUKURU ilivuta ili kuwaharibia wengine na kuwaacha wengine wapete
 
Kwani hiyo ilikuwa kesi? hilo lilikuwa zengwe tu amekubali yaishe magamba baana

Pukudu@ Ilkiding'a, Arusha
 
Kwani takukuru ni kitu gani, na inafanya nini, mbona immempeleka huyo mahakamani, hivi na yenyewe inaweza kumpakazia mtu? na yenyewe inakula rushuwa, nisaidieni wana JF.:smow:

TAKUKURU inakula rushwa kama kawa. Hatua ya kuwabambikia watu kesi wakati wa uchaguzi ilikuwa ni sehemu ya rushwa ambazo TAKUKURU ilivuta ili kuwaharibia wengine na kuwaacha wengine wapete
 
Kwani takukuru ni kitu gani, na inafanya nini, mbona immempeleka huyo mahakamani, hivi na yenyewe inaweza kumpakazia mtu? na yenyewe inakula rushuwa, nisaidieni wana JF.:smow:

TAKUKURU inakula rushwa kama kawa. Hatua ya kuwabambikia watu kesi wakati wa uchaguzi ilikuwa ni sehemu ya rushwa ambazo TAKUKURU ilivuta ili kuwaharibia wengine na kuwaacha wengine wapete
 
Kesi ya rushwa ya uchaguzi wa kura za maoni ilikuwa set up ya ccm kwa ajili ya kupata watu wao waliowataka kushinda.
kwenye uchaguzi mkuu uliopita rushwa zilikuwa zinatolewa hadharani lakini takukuru hawakutaka kukamata mtu yeyote.
Mfano ilikuwa uchaguzi wa jimbo la Arusha, Batilda Buriani alikuwa anagawa fedha kwenye baa moja ... Garden, taarifa ilitolewa kwa takukuru saa 11 jioni ili wawahi pale, matokeo yake wao walifika pale saa 2 usiku, wakasema hakukuwa na dalili yoyote ya rushwa.

 
Back
Top Bottom