kwamtoro
JF-Expert Member
- Nov 15, 2010
- 4,922
- 3,244
Hapo ndipo ninapowashangaa CCM jinsi timu yao ya kampeni ilivyo. CCM kwa asili ina watu wazuri na wenye hekima ilikuwaje wakatuwekee watu aina ya vibajaji. Hivi hao vibajaji wana hekima na busara kuliko akina Chiligati Mkuchika, Salim, Makinda, Jenister, Anna Abdallah, Asharose, Kinana. Wana watu wengi sana wazuri, wenye hekima na busara lakini sijui ni kwa nini wakawachukua vibajaji. Wanatukatisha tamaa maana ukiangalia vizuri unaona kabisa Magufuli yuko peke yake kwa sababu wengi wa wale 32 waliochaguliwa hawamsaidii. Magufuli atashinda lakini hakika ni kwa juhudi zake mwenyewe na wala si wale wanaoitwa timu ya ushindi ya CCM.
BRADHAA!Mimi dereva wa magari makubwa, natembea sana. Magufuli awezi kushinda hata iweje. Binafsi nampa 30% hapo atakuwa amejitaidi sana. By saa nne Lowassa atakuwa ameshinda.