Mwaisela, Tambaza, Sewa Haji et al...ni kina nani hawa?

Jamani,

Kadri ninavyofahamu mimi kuhusu historia ya Tanzania, ambayo sisi vijana wengi siku hizi tunaipuuuza, MWAISELA na SEWA HAJI, walikuwa ni madaktari bingwa wa mwanzo wenye asili ya Kiafrika nchini mwetu. Hospitali ya kwanza kubwa katika Tanzania, ilikuwa inaitwa kwa jina la “Sewa Haji”, ambayo ilikuwepo kabla ya uhuru katika eneo kati ya Kituo cha sasa cha Kati cha Polisi na Ofisi ya Kituo Kikuu cha Usalama Barabarani, jijini Dar es Salaam. Baadaye wakati uhuru unapatikana, Sewa Haji, ikahamishiwa pale ambako sasa ni Muhimbili, lakini wakati huo ilikuwa inajulikana kuwa “Princes Margaret Hospital”, kwa heshima ya Malkia wa Uingereza wakati huo. Ndiyo maana Wodi moja muhimu Muhimbili, inaitwa “Sewa Haji”. Hospitali nyingine kubwa ni ile ambayo sasa ni Ocean Road, lakini ilikuwa inaitwa “European Hospital”, kwa ajili ya Wazungu tu!

TAMBAZA, alikuwa kiongozi wa Kizaramo, aliyeitwa Jumbe Tambaza. Jumbe kilikuwa ni cheo ambacho baadhi ya Waafrika walipewa tangu utawala wa Kijerumani nchini. Yeye ndiye aliyekuwa anamiliki eneo lote la kuanzia Ikulu hadi Muhimbili (Upanga Mashariki na Magharibi). Ndiyo maana shule ya “H.H. The Agakhan” iliyokuwa inamilikiwa na Waislamu wa Dhehebu la Ismailia, ikataifishwa na kuitwa jina la Tambaza. Jumbe Tambaza aliyagawa maeneo hayo bure kwa ajili ya maendeleo na hakuwa na uchoyo na uroho ulioletwa na Wazungu wa kuhodhi na kulangua ardhi! Yeye mwenyewe akabaki na kieneo kidogo kwenye msikiti uliopo Barabara ya Umoja wa Mataifa na eneo ambalo sasa linatumika kuvizika vitoto vichanga vilivyofia Muhimbili!

KIBASILA ni Chifu wa Kizaramo, ambaye alinyongwa na Wajerumani kutokana na msimamo wake wa kukaidi kutawaliwa na Wazungu hao! Alinyongwa kwa kamba kwenye mti wa mwembe katika eneo ambalo sasa kinajengwa Kituo cha Mabasi yaendayo kasi, (Kamata, karibu na duka kubwa la Shoprite, barabara ya Nyerere). Tusisahau historia hii muhimu! Kwa kuisahau ndiyo maana hatujiamini na sasa tunatawaliwa tena kiuchumi na hawa Wazungu!

Bwassa

interesting....
 
sewa haji alikuwa ni mfanyabiashara mkubwa na mwanzilishi wa hospitali ya muhimbili.
tambaza alikuwa ni mmoja ya wazee kongwe akiishi upanga pia hata shule ya Tambaza ni jina lake..
cc Mohamed Said FaizaFoxy
 
Last edited by a moderator:
Ningependa pia kuijua historia ya Gwamahala ambaye jina lake linatumika katika mabweni ya shule za Feza Boys na St. Patric Schools.

Karibuni.
 
Last edited by a moderator:
Sawa, rekodi zako ni sahihi kwa sababu umesoma Rungwe. Na zangu ni sahihi pia kwa sababu nimesoma Malangali Sekondari, mkoa wa Iringa ambako kuna mabweni yenye majina hayo.
Mambweni yenye majina hayo yapo pia katika shule ya sekondari ya Malangali, iliyo katika kata ya Malangali, wilaya ya Mufindi mkoa wa Iringa. Kwa hiyo hawa celebrities wamekuwa maarufu maeneo yote hayo! Muulize Mwaipopo aliyesoma Malangali, alikuwa analala bweni la Mwaisela! Tupo pamoja hapo?

Nami nilisoma hapo, nililala mwaisela ya chini. Pia nakumbuka vyema bweni lililoitwa Bango likitumika kumuenzi mkuu wa shule na msomi maarufu uko mufindi. Nakumbuka maeneo ya ibangi, itengule, isimikinyi, ihowanza na tambala ng'ombe!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom