Pukudu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 3,148
- 2,219
Leo katika mechi YA Ligi Kuu Kati YA Stand United chama la wana! Na Kagera Sugar limeshindwa kumalizka kutokana na mvua kubwa iliyonyesha katika Uwanja wa CCM Kambarage hadi Mpira unasimama Stand UTD Ilikuwa inaongoza goli MOJA lililofungwa na Striker machachari Toka Nigeria Chidi Obare .... Kesho asubuhi mechi hiyo itamaliziwa dakika kumi zilizobaki! iwapo matokeo yatabaki hivyo msahau Stand Utd CHAMA la wana!! Kushika daraja
Hii Ni kutoka official Facebook page YA Stand Utd CHAMA la Wana!
Shukrani za dhati sana kwa mashabiki wetu walioko Tanzania nzima na dunia kwa ujumla kwa kuendela kutuombea dua njema kwa mungu, na hasa walioko shinyanga na kanda ya ziwa kwa kujitokeza uwanjani siku ya jana na leo asubuhi katika Mchezo wetu wa ligi kuu soka Tanzania Bara dhidi ya Kagera Sugar katika uwanja wa Ccm Kambarage shinyanga.
Chama la Wana, Stand United imefainikiwa kulinda bao lake la jana na kuongeza jingine leo asubuhi katika kujihakikishia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Kagera Sugar FC.
Baada ya kuichapa Simba SC bao 1-0 Jumapili ya wiki iliyopita, Stand ilipata bao dakika ya 43 jana jioni kwa penalti kupitia kwa mshambuliaji Mnigeria Abasalim Chidiabele ambaye pia ndiye alifunga bao lao la ushindi dhidi ya Simba SC.
Mechi hiyo iliahirishwa dakika ya 80 na refa Hashim Abdallah kutoka Dar es Salaam baada ya kunyesha mvua kubwa ikiambatana na upepo mkali kiasi cha kuwa kiza uwanjani.
Katika kumalizia dakika 10 za mchezo huo leo kuanzia saa 2:30 asubuhi, Stand iliongeza bao la pili dakika ya nne na ya 84 ya mchezo wote kupitia kwa mshambuliaji Abasalim Chidiabele kwa mara nyingine tena baada ya kuwatoka mabeki wa Kagera na kufumua shuti kali lililotinga moja kwa moja nyavuni.
Chidiabele kwa hivi sasa amefikisha magoli 7 katika ligi kuu soka Tanzania Bara VPL.
Mola tuongoze STAND United FC (chama la wana)
Hii Ni kutoka official Facebook page YA Stand Utd CHAMA la Wana!
Shukrani za dhati sana kwa mashabiki wetu walioko Tanzania nzima na dunia kwa ujumla kwa kuendela kutuombea dua njema kwa mungu, na hasa walioko shinyanga na kanda ya ziwa kwa kujitokeza uwanjani siku ya jana na leo asubuhi katika Mchezo wetu wa ligi kuu soka Tanzania Bara dhidi ya Kagera Sugar katika uwanja wa Ccm Kambarage shinyanga.
Chama la Wana, Stand United imefainikiwa kulinda bao lake la jana na kuongeza jingine leo asubuhi katika kujihakikishia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Kagera Sugar FC.
Baada ya kuichapa Simba SC bao 1-0 Jumapili ya wiki iliyopita, Stand ilipata bao dakika ya 43 jana jioni kwa penalti kupitia kwa mshambuliaji Mnigeria Abasalim Chidiabele ambaye pia ndiye alifunga bao lao la ushindi dhidi ya Simba SC.
Mechi hiyo iliahirishwa dakika ya 80 na refa Hashim Abdallah kutoka Dar es Salaam baada ya kunyesha mvua kubwa ikiambatana na upepo mkali kiasi cha kuwa kiza uwanjani.
Katika kumalizia dakika 10 za mchezo huo leo kuanzia saa 2:30 asubuhi, Stand iliongeza bao la pili dakika ya nne na ya 84 ya mchezo wote kupitia kwa mshambuliaji Abasalim Chidiabele kwa mara nyingine tena baada ya kuwatoka mabeki wa Kagera na kufumua shuti kali lililotinga moja kwa moja nyavuni.
Chidiabele kwa hivi sasa amefikisha magoli 7 katika ligi kuu soka Tanzania Bara VPL.
Mola tuongoze STAND United FC (chama la wana)