Mvua Kubwa Kunyesha

Mvua Kubwa Kunyesha

mbalila

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2013
Posts
825
Reaction score
161
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

Simu: 255 22 2460735/2460706 FAKSI: 255 22 2460735/2460700 S.L.P. 3056 Barua pepe: met@meteo.go.tz DAR ES SALAAM Tovuti: www.meteo.go.tz

Unapojibu tafadhali nakili: Kumb. Na.: TMA/1622 18 Februari, 2014

Taarifa kwa Umma: Vipindi vya mvua kubwa vinatarajiwa.

Taarifa Na. 201402-03

Muda wa Kutolewa Saa za Afrika Mashariki Saa 8:30 Mchana

Daraja la Taarifa: Tahadhari

Kuanzia: Tarehe 19 Februari, 2014

Mpaka: Tarehe 21 Februari, 2014

Aina ya Tukio Linalotarajiwa


Vipindi vya mvua kubwa (zaidi ya mm 50 ndani ya saa 24) kwa siku

Kiwango cha uhakika: Wastani (60%)

Maeneo yanayotarajiwa kuathirika Kanda ya kati (mikoa ya Singida na Dodoma), nyanda za juu kusini-magharibi (mikoa ya Iringa, Mbeya na Njombe) na maeneo ya kusini (Mikoa ya Ruvuma na Morogoro).

Maelezo: Hali hii inatokana na kuimarika kwa mfumo wa mgandamizo mdogo wa hewa katika rasi ya Msumbiji. Mfumo huu unatarajiwa kuvuta upepo kutoka misitu ya Congo kupitia maeneo tajwa hapo juu.

Angalizo: Idara zinazohusika na hali ya tahadhari pamoja na wakazi wa maeneo hatarishi wanashauriwa kuchukua tahadhari.

Maelezo ya Ziada

Mamlaka ya Hali ya Hewa inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa mrejeo kila itakapobidi.

Imetolewa na mamlaka ya hali ya hewa
 
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

Simu: 255 22 2460735/2460706 FAKSI: 255 22 2460735/2460700 S.L.P. 3056 Barua pepe: met@meteo.go.tz DAR ES SALAAM Tovuti: www.meteo.go.tz

Unapojibu tafadhali nakili: Kumb. Na.: TMA/1622 18 Februari, 2014

Taarifa kwa Umma: Vipindi vya mvua kubwa vinatarajiwa.

Taarifa Na. 201402-03

Muda wa Kutolewa Saa za Afrika Mashariki Saa 8:30 Mchana

Daraja la Taarifa: Tahadhari

Kuanzia: Tarehe 19 Februari, 2014

Mpaka: Tarehe 21 Februari, 2014

Aina ya Tukio Linalotarajiwa


Vipindi vya mvua kubwa (zaidi ya mm 50 ndani ya saa 24) kwa siku

Kiwango cha uhakika: Wastani (60%)

Maeneo yanayotarajiwa kuathirika Kanda ya kati (mikoa ya Singida na Dodoma), nyanda za juu kusini-magharibi (mikoa ya Iringa, Mbeya na Njombe) na maeneo ya kusini (Mikoa ya Ruvuma na Morogoro).

Maelezo: Hali hii inatokana na kuimarika kwa mfumo wa mgandamizo mdogo wa hewa katika rasi ya Msumbiji. Mfumo huu unatarajiwa kuvuta upepo kutoka misitu ya Congo kupitia maeneo tajwa hapo juu.

Angalizo: Idara zinazohusika na hali ya tahadhari pamoja na wakazi wa maeneo hatarishi wanashauriwa kuchukua tahadhari.

Maelezo ya Ziada

Mamlaka ya Hali ya Hewa inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa mrejeo kila itakapobidi.

Imetolewa na mamlaka ya hali ya hewa

Hawana Tofauti na Marehemu Sheikh Yahaya Hussein. Hawana Lolote bali Ni Longo Longo tu na Jua Linapiga na Kuchoma Kama Kawaida na Kuja Bonge La Joto Jijini Kwa Sasa.
 
Bora ukanda wa pwani haujajumuishwa maana hizi mvua za siku kadhaa zilizopita hiyo mifoleni yake barabarani khaaa!!
 
Thanks wahusika kwenye hiyo mikoa tajwa msipuuze chukueni tahadhari
 
Hawana Tofauti na Marehemu Sheikh Yahaya Hussein. Hawana Lolote bali Ni Longo Longo tu na Jua Linapiga na Kuchoma Kama Kawaida na Kuja Bonge La Joto Jijini Kwa Sasa.

Jijini? Ni wapi imetajwa jijini, mdau si ungetulia tu na kuelewa kuliko kukurupa.
 
shukrani kwa taarifa, ila wajitahidi kutoa updates kadri hali inavyobadilika.
 
Ahsante TMA Kwa Tahadhari Mliyotoa.Ni Kweli Dom Imeshaanza Kunyesha Ktk Baadhi ya maeneo ni kubwa kwa kweli
 
Hawana Tofauti na Marehemu Sheikh Yahaya Hussein. Hawana Lolote bali Ni Longo Longo tu na Jua Linapiga na Kuchoma Kama Kawaida na Kuja Bonge La Joto Jijini Kwa Sasa.
Unajua maana ya hii: 'Kiwango cha uhakika: Wastani (60%)'?
 
Halafu zinaweza pita siku thelathini hakuna mvua!

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Jijini? Ni wapi imetajwa jijini, mdau si ungetulia tu na kuelewa kuliko kukurupa.

Wewe ndiyo Bogus Wakati hata Juzi tu Dk. Agnes Kijazi Wa TMA Alifanya Press Conference na Hata ktk News Bulletins Zote Za ITV, TBC1 na Channel Ten Walitoa na Alitaja Mikoa 7 na Wa Dar es Salaam Ukiwepo na Kwa Kuongezea tu Alitoa Onyo Kali Sana Kwa Wakaazi wa Pembezoni Mwa Bahari Ya Hindi na Wavuvi Kuchukua Tahadhari. Sasa Mimi na Wewe Nani Amekurupuka? Mimi Najiamini Ndugu na Siweki Kitu hapa KIMBURULAMBURULA Kama Wewe na Moja Ya Jukumu La Profession Yangu Ni Kuwa Accurate na Factual. Jipange Upya Kaka na Kama Unamatatizo Basi Tumia Dawa Yenye Jina La ID Yangu hapo Juu na Utapona.
 
Halafu zinaweza pita siku thelathini hakuna mvua!

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

Halafu ikinyesha ikazoa ka'kibanda chako,utakuja kuwalaumu TMA....watanzania tukue basi.
 
Wewe ndiyo Bogus Wakati hata Juzi tu Dk. Agnes Kijazi Wa TMA Alifanya Press Conference na Hata ktk News Bulletins Zote Za ITV, TBC1 na Channel Ten Walitoa na Alitaja Mikoa 7 na Wa Dar es Salaam Ukiwepo na Kwa Kuongezea tu Alitoa Onyo Kali Sana Kwa Wakaazi wa Pembezoni Mwa Bahari Ya Hindi na Wavuvi Kuchukua Tahadhari. Sasa Mimi na Wewe Nani Amekurupuka? Mimi Najiamini Ndugu na Siweki Kitu hapa KIMBURULAMBURULA Kama Wewe na Moja Ya Jukumu La Profession Yangu Ni Kuwa Accurate na Factual. Jipange Upya Kaka na Kama Unamatatizo Basi Tumia Dawa Yenye Jina La ID Yangu hapo Juu na Utapona.

Kwa majibu yako tu...wewe ndiye unayestahili Dawa......
 
Wewe ndiyo Bogus Wakati hata Juzi tu Dk. Agnes Kijazi Wa TMA Alifanya Press Conference na Hata ktk News Bulletins Zote Za ITV, TBC1 na Channel Ten Walitoa na Alitaja Mikoa 7 na Wa Dar es Salaam Ukiwepo na Kwa Kuongezea tu Alitoa Onyo Kali Sana Kwa Wakaazi wa Pembezoni Mwa Bahari Ya Hindi na Wavuvi Kuchukua Tahadhari. Sasa Mimi na Wewe Nani Amekurupuka? Mimi Najiamini Ndugu na Siweki Kitu hapa KIMBURULAMBURULA Kama Wewe na Moja Ya Jukumu La Profession Yangu Ni Kuwa Accurate na Factual. Jipange Upya Kaka na Kama Unamatatizo Basi Tumia Dawa Yenye Jina La ID Yangu hapo Juu na Utapona.

Kweli wewe ni mgonjwa, unashindwa kuelewa kitu kidogo hivi? Mdau kakuuliza wapi hapo kwenye Tangazo hili Dar imetajwa? Wewe unaleta reference za kwenye TV. Nani kakwambia maeneo yaliyotolewa tahadhari kwenye TV hayawezi kubadilika? Ungejibu kulingana na what is provided kny barua iliyopo hapa. Halafu unajifanya nye nyee nyee profession yangu. Profession my foot.....
 
Kweli wewe ni mgonjwa, unashindwa kuelewa kitu kidogo hivi? Mdau kakuuliza wapi hapo kwenye Tangazo hili Dar imetajwa? Wewe unaleta reference za kwenye TV. Nani kakwambia maeneo yaliyotolewa tahadhari kwenye TV hayawezi kubadilika? Ungejibu kulingana na what is provided kny barua iliyopo hapa. Halafu unajifanya nye nyee nyee profession yangu. Profession my foot.....

Tumia GENTAMYCINE Itakusaidia na Shida za Uchi au Utupu wa Akili na Wa Kufikiri Kama Si Kupambanua Mambo Ulionao Ila Wenye Akili Zao Ambao ni Wengi Wamenielewa na Mmebaki Ninyi tu MAJUHA.
 
Mkoa wetu haukutajwa lakini leo imenyeesha kubwa tu
 
Halafu ikinyesha ikazoa ka'kibanda chako,utakuja kuwalaumu TMA....watanzania tukue basi.

Mara ngapi tumepewa hizi forecast na zikaenda ndivyo sivyo? Acha kutokwa mapovu kwa mambo yenye ukweli. Kama wewe hujakua kojoa kalale maana utakua tu!

Meantime respect others posts, and it is not a sin to differ in views and still be in the same boat!

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Mkoa wetu haukutajwa lakini leo imenyeesha kubwa tu

Ram this is what I am saying, we have authorities which, pamoja na kuwa katika century ya ICT na radar nzuri kunuliwa UK kwa mahela bwelelo bado hatupati precise info! Halafu tunajidai na kilimo kusaidia wananchi wetu!

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom