Muungano wa Serikali 3 ni bora Sana

Muungano wa Serikali 3 ni bora Sana

Kwa msingi huo kwanini sisi Tanganyika tunaumizwa kuyabeba maZNZ yasiyobebeka?. Faida gani mTANGANYIKA anapata toka muunganoni?.
Hujajibu swali na kama umejibu basi kuna vitu huvijui.

Moja ya mambo ya muungano ni ushirikiano wa kimataifa. Sasa ZNZ inataka kiti UN, hilo unasemaje nalo ni la muungano tena ikifika hapo.

Ulinzi na usalama: Gharama za jeshi zinalipwa na Tanganyika 100, bajeti ya jeshi ni zaidi ya bajeti ya ZNZ, sasa ZNZ itachangia nini?

Hilo la wabunge ni dogo sana, angalia mambo kwa upana. Bajeti ya ZNZ ni bilioni 600, pungufu kuliko bajeti ya afya ya muungano. ZNZ ikitaka muungano huo haitakuwa na cha kuchangia kwasababu bajeti yake hairuhusu kutoa hata senti tano, infact haina bajeti yake ina bajeti kutokana hazina Dar! kuanzia msihahara ya wafanyakazi hadi vibili vya umeme.

Fikiria kidogo, bilioni 50 ZNZ haiwezi kulipa, itapata wapi bilioni 400 za ulinzi na usalama! c'mon think about it.
Hii thread yako nakushauri uifunge, ni too low ndugu yangu! ninakusaidia sikukashifu.
 
Mkuu TAYADI naunga mkono hoja,mimi mpaka sasa sijaona role ya wabunge wa Zanzibar kwenye serikali inayoitwa ya muungano ilhali na wao kwao wana serikali yao!Huu ni moja ya ufisadi tu unaofanywa na serikali ya CCM.
 
Hakuna faida hata moja ya serikali tatu! Je ni kitu gani ambacho Tanzania itafaidika na serikali tatu!. Kwasasa Zanzibar ina baraza lake la mawaziri, mawaziri walio kwenye serikali ya Tanzania wakilishi kwenye bunge la Zanzibar, wana bunge lao , makamu wa raisi katokea Zanzibar sasa je kama kwasasa wanasema wanaonewa na walivyonavyo havitoshi srikali tatu itatoa nini cha kuwatosheleza? Zanzibar ni alisimia 10% tu ya Watanzania je ni kwanini wawe na haki tofauti na Watanzania wengine na waseme wanaonewa. Solution ya muungano ni mbili tu (1) Serilaki moja tu ya Tanzania na Watanzania wasio na mipaka (2) Serikali mbili zinazo jitegemea ambazo zina mahusiano ya kijeshi na kiusalama. Hizi serikali tatu nne, mbili hazitasaidia maana Wanzanzibar hawatafikia sehemu ya kuacha kulalamika kuhusu muungano yakiisha haya yatakuja mengine!
 
Kujitegemea namaana nchi mbili tofauti lakini Jeshi ni lazima ziwe na uhusiano kwasababu ya usalama kwa wote
 
uchu wa madaraka tu

kwa pesa ipi, bajeti yenyewe hii ya kuomba omba kwa wafadhili??
 
wakati Tanganyika na Zanziba zinaungana watanganyika tulikuwa 12,000,000 na wazenji 300,000. Mwl.Nyerere alikataa serikali tatu(3) kwa kuwa watanganyika wangekuwa na Mzigo wa Kuendesha serikali ya Tanganyika ya watu 12m na ya TZ yenye 12.3 wangechangia proportionally! Hivyo wa Danganyika wangekuwa na Mzigo wa almost 2 governments na wazenji wangechangia kidogo. Nadhani Mazingira hayo bado ni yaleyale nashauri kama kweli tuko serious na muungano tuainishe Kero very realistically and Objectively tuzi solve na tuwe na serikali moja(1) kama nia ya Wazanzibari ni kama za wachache niliowahoji na kusema:
1.Tunataka nchi huru(Sovereign State).
2.Tunataka kiti chetu UN
3.Tunataka kila kitu chetu wenyewe!
4.Urais wa kupokezana
5.Tunataka Kiti FIFA, CAF, SECAFA etc, Timu ya Taifa Zenji: Tanganyika 1:1(not proportinally ila cost ziwe proportinaly)
Kuwa na serikali tatu(3) si suruhu(Mwarobaini) wa kero za Muungano. Nashauri tujadili wazi tuwe na Muungano wa wananchi na si viongozi. Tuwe tayari kwa Maamuzi ya wananchi. Quote me Surely baadya ya serikali tatu(3) Zanzibaris of the types above will start other claims.
Serikali 3 ni bora sana kwa sababu zifuatazo:
(i) Ni muarobaini wa malalamiko ya kuonewa au kumezwa;
(ii) Ni balance nzuri ya uwiano serikalini - 50 kwa 50 katika uwakilishi na gharama;
(iii) Hujuma za kuingiliana ktk chaguzi na kulazimisha chama kimoja kiongoze pande zote mbili zitadhibitiwa kirahisi;
(iv) Hoja ya muunda wa serikali kuwa sera za vyama tutakuwa tumeimaliza;
(v) Gharama za uendeshaji zitapungua kwa zaidi ya 50%. Mfano mmoja, serikali ya Muungano (serikali 2) kwa sasa (siyo SMZ) inalipa wabunge zaidi ya 80 wa Zanzibar (yenye wapigakura pungufu ya laki 4 na 50 na ukubwa sawa na wilaya ya Sengerema). Kila mbunge akilipwa milioni 11 kwa mwezi (11x80) sawasawa na milioni mia 8 na 80. Muundo wa serikali 3 tutakuwa na wabunge 30 au 40 (15 au 20 toka kila upande kufanya kazi za muungano wakigharamiwa na pande zote 2) na wabunge Serikali ya Tanganyika wapatao 150. Huu ni mzigo mwepesi kwa walipa kodi wote. SERIKALI MBILI NI MZIGO!!!!!
 
we ni mjinga tanganyika tuko mil zaidi ya 40 zanzibar wapo zaiidi ya mil 3 sasa ukisema tugawane 50/50 ni sawa......

Ni sawa, si ujinga. Na ndivyo wazanzibari wanavyotaka, serikali ya tatu (ya Muungano) kwa mambo yale tu ya Muungano, iwe 50/50 kwenye uwakilishi, expenses na income, hata Bunge la Muungano liwe dogo, 50/50 na kwa yale tu mambo machache, 11? ya muungano.
BTW wazanzibar wapo mil 1 tu na ushei na sio mil 3 lakini wacha tusubiri census.
 
Kwa mara ya kwanza nakuunga mkono. Muungano ulioshinikizwa na Nyerere na Karume usio na faida kwa pande zote, sioni sababu ya kuwepo.

Kabisa Mkuu. Utatupunguzia karibu wabunge 80 waliokuwa wanaingia Bungeni kwa sababu tu ya dini yao. Uwiano wa kidini tunaoutaka kila mahali utakuwa imara sana katika jumba letu la kutunga sheria.
 
Kabisa Mkuu. Utatupunguzia karibu wabunge 80 waliokuwa wanaingia Bungeni kwa sababu tu ya dini yao. Uwiano wa kidini tunaoutaka kila mahali utakuwa imara sana katika jumba letu la kutunga sheria.

Hilo la uwiano linashughulikiwa ipasavyo kwa sasa, na ndio linawauma wengi sana. Hawana njia tu.
 
Serikali 3 ni bora sana kwa sababu zifuatazo:
(i) Ni muarobaini wa malalamiko ya kuonewa au kumezwa;
(ii) Ni balance nzuri ya uwiano serikalini - 50 kwa 50 katika uwakilishi na gharama;
(iii) Hujuma za kuingiliana ktk chaguzi na kulazimisha chama kimoja kiongoze pande zote mbili zitadhibitiwa kirahisi;
(iv) Hoja ya muunda wa serikali kuwa sera za vyama tutakuwa tumeimaliza;
(v) Gharama za uendeshaji zitapungua kwa zaidi ya 50%. Mfano mmoja, serikali ya Muungano (serikali 2) kwa sasa (siyo SMZ) inalipa wabunge zaidi ya 80 wa Zanzibar (yenye wapigakura pungufu ya laki 4 na 50 na ukubwa sawa na wilaya ya Sengerema). Kila mbunge akilipwa milioni 11 kwa mwezi (11x80) sawasawa na milioni mia 8 na 80. Muundo wa serikali 3 tutakuwa na wabunge 30 au 40 (15 au 20 toka kila upande kufanya kazi za muungano wakigharamiwa na pande zote 2) na wabunge Serikali ya Tanganyika wapatao 150. Huu ni mzigo mwepesi kwa walipa kodi wote. SERIKALI MBILI NI MZIGO!!!!!
hayo mambo ya serikali tatu .,nne,moja au mbili sasa tumeshayachoka na hayatuhusu.
 
enyi wajinga na wapumbavu msituletee serikali tatu mpango mzima ni serikali moja. Waachieni wale wanaojifanya waarab nchi yao tuone kama itakuwa kama Peponi.
 
50% kwa 50% ktk muungano wa Serikali tatu ndo sahihi kwa7bu itatupunguzia gharama bara na itaongeza Uhuru wa Znz kujiendesha na kujiamulia mambo yake yenyewe hivyo kupunguza hasira za makundi kama uamsho.
Bajeti ya ZNZ ni bilioni 600, ni ndogo kuliko bajeti ya elimu ya Tanganyika. Sasa 50/50 hawa watatoa nini?

Bajeti ya usalama na ulinzi ya ZNZ hakuna ndio maana wanang'angania serikali 3 au mkataba. Kama ingekuwepo 50/50 ya bajeti ya ulinzi maana yake ni kuwa ZNZ ingetoa bilioni 400 na kubaki na bilioni 200 kama bajeti.

Msisahau kuwa hawa WZNZ wanachukua mishahara kutoka hazina Dar, hawalipi wabunge, BLW ua viongozi wastaafu. Wote wanalipiwa na Tanganyika, sasa ukisema 50/50 itoke wapi? hawana 50 hawa, wanakinga mkono.

Jiulize kwanini wameacha hoja ya kuvunja muungano wamekomalia serikali 3 au mkataba, wanajua kuwa asilimia 60 ya shuguli za serikali yao zinatoka Tanganyika. Fungueni macho Watanganyika, hapa ni kuliwa tu halafu mnatukanwa na kuchomwa moto.

Jiulize, hivi wewe Mtanganyika unataka muungano wa nini, ukusaidie nini? Hawa wanapenda pesa yako wewe kwao ni Kafir tu.
Waacheni waende zao, kwanini hamuioni mbali zaidi ya pua zenu Watanganyika?
 
Bajeti ya ZNZ ni bilioni 600, ni ndogo kuliko bajeti ya elimu ya Tanganyika. Sasa 50/50 hawa watatoa nini?

Jiulize kwanini wameacha hoja ya kuvunja muungano wamekomalia serikali 3 au mkataba, wanajua kuwa asilimia 60 ya shuguli za serikali yao zinatoka Tanganyika. Fungueni macho Watanganyika, hapa ni kuliwa tu halafu mnatukanwa na kuchomwa moto.

Jiulize, hivi wewe Mtanganyika unataka muungano wa nini, ukusaidie nini? Hawa wanapenda pesa yako wewe kwao ni Kafir tu.
Waacheni waende zao, kwanini hamuioni mbali zaidi ya pua zenu Watanganyika?

Mkuu Nguruvi3

Niseme kuwa navutika na baadhi ya michango yako katika kuwapa UAMSHO/ kuwaamsha watanganyika, lakini ungefanikiwa zaidi kama ungeacha kuibua hamasa zao kupitia ,vijineno kama kuchomwa moto, kafir au washirazi ,watwana. Unasahau kuwa Katika Tanganyika kuna wanaofanya swaumu? Au watanganyika sote ni makafir?

Hata makafiri wa hapa Bongo wanafutarisha na kufutari siku hizi. https://www.jamiiforums.com/jamii-photos/306885-picha-iliyonivutia-leo-hii.html

Lakini Mukuu Nguruvi3,

Jana nilitoa rai ya Mwalimu Nyerere kama njia moja inayoweza kutumika kutatua kero za Muungano. Wewe naona unarudia rudia, mke,mume, kafir,mtwana, chogo,urojo...kweli tutafika mahali kupata njia ya kuepusha chuki ya muungano huu?

Mimi naamini kwa jinsi ulivyo na weledi wa kuandika mistari, tuichukue rai hii ya Mwalimu, tuipigie debe. Wale wasioona mbali zaidi ya pua pia wataongeza upeo.

Lakini pia ,njia ya kusema Znz ndio wajitoe au watangaze kujitoa itachukua muda mrefu.Njia rahisi ni ile waliyotumia Malaysia kuifukuza Singapore kutoka Muunganoni.
Njia hii si Nguruvi3, MMJ au yeyote mwengine aliyeiona kama ni njia moja wapo inayoweza kutumika.
Je, wewe pia huoni mbali zaidi ya pua yako?

Hoja zako ni nzuri tu za matumizi, bajeti, mishahara, waznz wanahitaji soko bara lakini unazitumia kuzielekeza kwenda kombo.

Muungano huu hausaidii wananchi/ walalahoi wa Tanganyika wala wa Zanzibar. Ni kiini macho/ mazingaombwe yanayotumika kutugawia umaskini tu na kulinda ufisadi.

Tanganyika tunasema imekufa, Tanganyika tunasema haipo....kuna msemo wa kiswahili usemao, asiyekuwepo na lake.....

Hapa ni lazima turejeshe jina la eneo letu( territory) Tanganyika pia kushawishi umma kuwa saa na wakati umefika wa kuwa na Tanzania yenye serikali mbili , ya Tanganyika na ya Zanzibar ili kujinasua na mazingaombwe ya Muungano.

Kama hatutaki kurejesha serikali ya Tanganyika na jina Tanganyika basi ziwa Tanganyika pia tuliite, ziwa bara au ziwa Tzbara.:redface:

Bado inaonekana hujaweza kutegua kitendawili cha rai ya Mwalimu. Ukiweza,utaniunga mkono katika kampeni ya Tanzania yenye serikali ya Tanganyika na ya Zanzibar.
 
enyi wajinga na wapumbavu msituletee serikali tatu mpango mzima ni serikali moja. Waachieni wale wanaojifanya waarab nchi yao tuone kama itakuwa kama Peponi.
Mkuu wa chuo.

Tulipomtoa Jumbe katika madaraka na siasa tulipoteza nafasi na uhalali wa mpango mzima wa serikali moja.
Na kwa hapa ilipofikia hilo haliwezekani tena, ama itapasa Tanganyika iimeze Zanzibar kama UK ilivyojitwalia Northern Ireland.

Kwa nini haiwezekani kuleta Serikali moja?

...Znz wamepata umoja ambao hapo siku za nyuma haukuweza kufikirika kuwa unawezekana. Serikali ya umoja wa kitaifa.

...Kuwepo kwa makundi yanayotoa elimu ya uraia kama jukwaa la katiba la Zanzibar, UAMSHO,na asasi za kiraia zenye lengo la kuwahamasisha wazanzibari kupigania taifa,utaifa wao na maslahi yao ndani ya muungano au kuuvunja Muungano.

....Katiba iliyofanyiwa marekebisho ya Znz.

....Kuwepo kwa umasikini,ukosefu wa ajira ambao wanasiasa huutumia kueleza wananchi kuwa uduni na umasikini huo unasababishwa na Muungano(hata kama sio kweli)

...kuwepo kwa kero za Muungano ambazo hazitatuliwi,wala hazitatuki pasi na kuirejesha serikali ya Tanganyika au kuuvunja muungano.

Lakini kubwa zaidi ni kuwa serikali moja Tz si sera rasmi ya Chama chochote cha siasa, ingawaje CCM walishajiropokea kuwa wanaazimia kutoka serikali mbili kwenda moja.

Pia kuna usanii wa Katiba Mpya ya Muungano, kama unafuatilia wazenj wanataka serikali2,3.Ni wazi rasimu ya katiba mpya itakayopendekeza serikali moja kwa Tz haitopitishwa na CCM wataendelea kutangazwa washindi kama kawaida kwa kukosekana katiba mpya.

Kama ni mpenda mabadiliko, ni vyema ushajihishe wana Tanganyika kudai serikali ya Tanganyika na mengine yata.jiset yenyewe(fall into place) tukiwa na wawakilishi wazalendo wa Tanganyika.

Nguruvi3 ameshatuasa tujitahidi kuona mbali zaidi ya pua zetu. Chukua hatua.

Serikali moja si jambo litakaloinufaisha Tanganyika na watanganyika ni kuzalisha tatizo jipya/ au kuchelewesha tu mripuko wa bomu tulilojitegea. Kuelewa hilo soma hii makala. Link Raia Mwema - Tusipoujadili muungano kwa makini, utavunjika II
 
Nonda, mimi ni mpenzi wa Pan Africanism nikiamini kuwa mpaka wa Kenya na Tanzania ni hypothetical kwasababu hakuna alama.

Niliwahi kuishi maeneo ya Tarakea na Mjasani Tanga, sikuwahi kuona tofauti yoyote nikiwa upande mwingine
serikali 3 mimi nilimuunga mkono kwa wakati huo na mazingira ya nayakati zile.
Hoja ya Nyerere niliikubali kwa wakati ule na mazingira yale.

Kutokana na mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi na kiutamadni duniani, sioni sababu ya muhimu ya kuwa na muungano unakuwa mateso na adha kwa pande zote. Lakini kinachonisukuma sana kuona kuwa hatuna sababu ya kuwa na muungano na ZNZ ni ukweli kuwa wenzetu wamejenga chuki ya dhati dhidi yetu. Kule sisi twajulikana kama makafir, machogo na washenzi wa tabia. Chukia iliyofikia mahali wenzetu wanachoma moto Watanganyika, wala si wakongo, Wazaire, wakenya au Waganda.

Pili, Chuki inayojengwa na WZNZ bila sababu, chuki iliyojaa uongo usioweza kubweba na ndimi nadhifu ya muumini.
Chuki ya ubinafsi wa kujiona wao ni bora na wanatahili hata wasichostahili, kuzua uongo ili kupata hata wanachotakiwa kuomba. Ukiweka kwenye mizani ZNZ inanufaika na muungano kuliko Tanganyika hata kwa hesabu za Darasa la 3B.
Wenzetu hawalioni hilo na hakuna sababu ya kuwaonyesha kwasababu wamegoma.

Ni kwa mantiki hiyo, natoka mbele na kusema ZNZ iondoke zake kwa amani. Iondoke kwanza ili watu wake wapatao 350,000 wahamishe rasilimali zao na tuachane kwa wema. Kinyume cha hivyo chuki iliyopandwa na WZNZ itawalazimisha wanafunzi wawaone wznz kama wanyonyaji, wafanyakazi waone WZNZ kama majahilia, Wamachinga waone muda wa kuchukua biashara umefika. Hapo hakuna heri ni shari kama ile shari tuliyoiona wakafinyiwa Watanganyika.


Watanganyika wanajiuliza, hawa wenzetu wanasoma bure kwa gharama zetu, wazazi wao wanalala na taa za bure, wafanyakazi wao wanalipwa kwa kodi zetu, viongozi wao wanatibiwa kwa kodi zetu, dhidi ya hayo fadhila wanazotupa ni matusi na kejeli, yahusu nini?

Ninachosema hapa ni kuwa wenzetu walisema hawataki, nasi tunasema hewala. Hatuwezi kuishi tena kama watu wa taifa moja kutokana na chuki kubwa ya WZNZ dhdi ya Mtanganyika. Chuki hii sasa imekuwa replicated na ni kubwa kwa Watanganyika at the same magnitude. Kabala hatujaanza kuchinjana tusioane haya, wala tusione haya kusema ukweli kuwa sasa basi, tuvunje jahazi tugawane mbao kama zipo.

Tukuatane UN, EAC, SADC, FIFA, IOLYMP, WBO, n.k. Huko tutakuwa na misimamo ya pamoja kwasababu tunatoka kanda moja na tunaweza kuongea kiswali kuwazuga wasiojua. Tukitoka nje, kila mtu na lake.

Usinilaumu mimi kusema ukweli,walaumu WZNZ waliojenga chuki ya dhati mioyoni mwao dhidi ya Mtanganyika hadi kufikia mahali pa kuona ya kuwa kumtoa roho Mtanganyika ni rahisi kuliko kupata dumu la petroli.
Ya kwamba huyu ni Mtanganyika, kafir, malaya, jambazi ambaye hafai kuishi ZNZ. Hii ndiyo imetufikisha hapa.
Fikiria chuki hiyo itakapokuwa reciprocated nini kitatokea? kabla haijatokea LET ZNZ GO PEACEFULLY

Mkataba au serikali 3 ni kutapa tapa tu kikubwa ni kuondoa CHUKI iliyojengwa na Wznz dhidi ya Mtanganyika. Sheria zote za ZNZ zinatungwa ili kumzuia au kumnyima fursa Mtanganyika, siyo mzimbabwe au mmalawi.
Hatuwezi tena kuwa wamoja kwasababu ishatumbukia nyongo ya chuki na heri ni moja tu kuvunja muungano
 
Upeo wako mdogo sana. Ama unamtazamo wa Kiccm zaidi kuliko kitaifa. Soma post mstari kwa mstari na pia pitia kwa umakini comments zangu hapo juu.
Hakuna faida hata moja ya serikali tatu! Je ni kitu gani ambacho Tanzania itafaidika na serikali tatu!. Kwasasa Zanzibar ina baraza lake la mawaziri, mawaziri walio kwenye serikali ya Tanzania wakilishi kwenye bunge la Zanzibar, wana bunge lao , makamu wa raisi katokea Zanzibar sasa je kama kwasasa wanasema wanaonewa na walivyonavyo havitoshi srikali tatu itatoa nini cha kuwatosheleza? Zanzibar ni alisimia 10% tu ya Watanzania je ni kwanini wawe na haki tofauti na Watanzania wengine na waseme wanaonewa. Solution ya muungano ni mbili tu (1) Serilaki moja tu ya Tanzania na Watanzania wasio na mipaka (2) Serikali mbili zinazo jitegemea ambazo zina mahusiano ya kijeshi na kiusalama. Hizi serikali tatu nne, mbili hazitasaidia maana Wanzanzibar hawatafikia sehemu ya kuacha kulalamika kuhusu muungano yakiisha haya yatakuja mengine!
 
Back
Top Bottom