Eneo la Unguja na Pemba kama ilivyo Mafia kijiografia ni sehemu ya ardhi ya iliyokua Tanganyika...
"nafikiri sahihi kusema eneo lote la Tanganyika lilikuwa ni ardhi ya Zanzibar. sijui wajua kama dola ya Zanzibar ipo kabla ya hiyo yenye kuitwa Tanganyika?"
Pili, asilimia zaidi ya 50 ya wakazi wa Pemba na Unguja asili yao ni kutoka kwa mikoa ya iliyokua Tanganyika, tofauti ya tamaduni imetokana na tawala za kikoloni zilizokuwepo visiwani na bara.
"tupo wenye asili ya kutoka bara, lakini si kwa asilimia kama hiyo usemayo wewe. sijajua hili la utamaduni, nijualo kwa kweli utamaduni wetu ni tofauti kabisa na wa huko Tanganyika, lafudhi, chakula, tabia, nk. wapo waZenji wenye asili ya Tanganyika na bado wanaendelea na mila zao"
Hivi ushawahi jiuliza kabla ya uvamizi wa Waarabu ni kina nani walikua wakiishi katika visiwa vya Pemba na Unguja?
" ulipokuja huo uvamizi wa waarabu uuitao wewe, tayari Waarabu walikuwepo miaka mingi nyuma, tokea asili visiwa hivi ni mchanganyiko wa watu wa makabila mbali mbali tabu kusema nani kaja mwanzo. unajua nani kaupa jina mji wa Dar es Salaam? na ni neno la lugha gani na lina maana gani?"