Muumini wa shetani

Wa Nyumbani

JF-Expert Member
Mar 31, 2011
438
65
Waamini walikuwa kanisani, mara shetani akaingia ghafla na kusimama mbele altareni. Mlango ukawa mdogo! watu walitoka nje wakipiga makelele! Baada ya dakika 2 hivi watu wote walikuwa wametoka nje isipokuwa mwenyekiti wa kanisa hilo. Shetani akamuuliza mwenyekiti,

shetani: wewe ndio huniogopi sio?
Mwenyekiti: ndio sikuogopi.
shetani: unasema huniogopi mimi? shetani akasema kwa ukali zaidi.
Mwenyekiti: ndiyo sikuogopi

Hapo shetani lilishangaa.

shetani: kwa nini huniogopi
Mwenyekiti: wewe ni shemeji yangu nitakuogopa kwa sababu gani?
shetani: ehe, mimi shemeji yako kwa vipi?
Mwenyekiti: nimemuoa dada yako na wote tuna tabia zinazofanana.

Shetani akatingisha kichwa, akaondoka.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom