Muuguzi adaiwa kuua mjamzito, mapacha

Muuguzi adaiwa kuua mjamzito, mapacha

Mpendwa Mwanawao, fuatilia vizuri maelezo ya Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Fredrick Mlekwa, akizungumza kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Mkoa alikanusha vifo vya mapacha hao kusababishwa na uzembe wa muuguzi na kwamba mimba hiyo ilikuwa haijatimiza muda wake wa miezi tisa hivyo kitaalam watoto hao wasingeweza kuishi kwa vile hawajakamilika. Dkt. Mlekwa aliendelea kufafanua kuwa pamoja na maelezo ya mzazi mwenyewe kukiri umri wa ujauzito wake (miezi sita) walichunguza miili ya watoto waliozaliwa na kuipima ambapo mmoja alikuwa na uzito wa gramu 500 na mwingine gramu 700, hivyo kitaalamu walikuwa hawajakamilika kuitwa binadamu."Binafsi baada ya kupata taarifa hizo nilikwenda katika wodi hiyo na tulipofuatilia tulibaini kuwa mimba ya mjamzito huyo ilikuwa haijafikisha umri wa kujifungua kwani ilikuwa na umri wa miezi sita... mzazi mwenyewe alikiri muda huo na kitaalamu isingekuwa rahisi kwa watoto hao kuishi," alifafanua Dkt. Mlekwa.
watoto ni sawa wasingeweza kuishi, vipi kuhusu huyo mjamzito? walishindwa pia kuokoa uhai wake?
 
watz mnaboa sana! wengi mnaposikia vifo vya watoto na wajawazito mnadhani vinatokea mawinguni! hii ndo tz nchi masikini iliyokithiri kwa rushwa! kuweni wapole tu acheni kutoa mapovu! kuna watz wangapi wamepoteza maisha kwenye ajali mbalimbali kwa uzembe wa viongozi kutowajibika? mbona hamkutoa povu! acheni hizo !! hapa mmeambiwa katiba iliyotengenezwa ni fake lakin utaona wajinga wachache wanaiunga.mkono! ! !h Hii ndo tz bwana! inalaumu mtu kwa kosa moja inaacha mema yoote aliyowahi kuyafanya! acheni unafiki wa kuona vibanzi kwenye macho ya wengine hali mna maboriti ndani yenu!! wangapi mnaboronga maofisini kwenu hamtolewi mapovu! au kwavile mnatibu mifugo inapozidiwa mnachinja! majengo yanaporomoka, mabasi yanaanguka barabara mbovu! meli zinazama! watu wanafungwa bila hatia! tunaletewa madawa fake! majambaz yanaua na kuiba! katiba inachakachuliwa! watu mmekaa kimya tu! leo nurse! nurse! MMEROGWA NINI!
 
watz mnaboa sana! wengi mnaposikia vifo vya watoto na wajawazito mnadhani vinatokea mawinguni! hii ndo tz nchi masikini iliyokithiri kwa rushwa! kuweni wapole tu acheni kutoa mapovu! kuna watz wangapi wamepoteza maisha kwenye ajali mbalimbali kwa uzembe wa viongozi kutowajibika? mbona hamkutoa povu! acheni hizo !! hapa mmeambiwa katiba iliyotengenezwa ni fake lakin utaona wajinga wachache wanaiunga.mkono! ! !h Hii ndo tz bwana! inalaumu mtu kwa kosa moja inaacha mema yoote aliyowahi kuyafanya! acheni unafiki wa kuona vibanzi kwenye macho ya wengine hali mna maboriti ndani yenu!! wangapi mnaboronga maofisini kwenu hamtolewi mapovu! au kwavile mnatibu mifugo inapozidiwa mnachinja! majengo yanaporomoka, mabasi yanaanguka barabara mbovu! meli zinazama! watu wanafungwa bila hatia! tunaletewa madawa fake! majambaz yanaua na kuiba! katiba inachakachuliwa! watu mmekaa kimya tu! leo nurse! nurse! MMEROGWA NINI!

ilishawahi kuletwa habari ya ajali hapa halafu watu wakaisifia? habari hii inahusu wauguzi unataka tukae kimya? au labda kuna watu wanashangilia wakisikia habari za majambazi na hayo madawa feki?

wewe pia umekurupuka kwa sababu tunajadili juu ya muuguzi kudharau hali ya mgonjwa hata kama huyo mgonjwa angekuwa na miaka 60 kama hajapewa huduma angekufa tu.... hiyo habari ya kihere here hata kama ni kweli haihusiki hapa, na kwanza hatujui hiyo mimba aliipata katika mazingira gani......
 
watoto ni sawa wasingeweza kuishi, vipi kuhusu huyo mjamzito? walishindwa pia kuokoa uhai wake?

Nafikiri kulikuwa na complication nyingine ambayo nurse asingeweza kuhandle, ndiyo maana Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Fredrick Mlekwa, akizungumza kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Mkoa alisema "Ni kweli tumefuatilia kuhusu suala la muuguzi wa zamu kuongea na simu, tumemuhoji amekiri muda huo alikuwa akiongea na simu na kufafanua kuwa alikuwa akiwasiliana na daktari wa zamu kwa ajili ya kuomba msaada zaidi wa kumsaidia mzazi huyo,"alisema na kuongeza kwamba suala hilo watazidi kulichunguza. Dkt. Mlekwa amerejea kutoa wito kwa wakazi wa Shinyanga kuwa na tabia ya kuheshimu taratibu za hospitali zilizopo na kueleza kuwa ni kosa la kisheria kwa wananchi wa kawaida kuingia ndani ya wodi ya wazazi, hali ambayo inaweza kusababisha maambukizo mbalimbali kwa watoto wanaozaliwa kwa vile wanakuwa hawapatiwa chanjo za kinga.
 
Nafikiri kulikuwa na complication nyingine ambayo nurse asingeweza kuhandle, ndiyo maana Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Fredrick Mlekwa, akizungumza kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Mkoa alisema "Ni kweli tumefuatilia kuhusu suala la muuguzi wa zamu kuongea na simu, tumemuhoji amekiri muda huo alikuwa akiongea na simu na kufafanua kuwa alikuwa akiwasiliana na daktari wa zamu kwa ajili ya kuomba msaada zaidi wa kumsaidia mzazi huyo,"alisema na kuongeza kwamba suala hilo watazidi kulichunguza. Dkt. Mlekwa amerejea kutoa wito kwa wakazi wa Shinyanga kuwa na tabia ya kuheshimu taratibu za hospitali zilizopo na kueleza kuwa ni kosa la kisheria kwa wananchi wa kawaida kuingia ndani ya wodi ya wazazi, hali ambayo inaweza kusababisha maambukizo mbalimbali kwa watoto wanaozaliwa kwa vile wanakuwa hawapatiwa chanjo za kinga.

Ahsante kwa kunielewesha, lakini nadhani muuguzi huyu alivyoona usumbufu wa wazazi unazidi angewaambia tu kuwa anawasiliana na mganga wa zamu.

all in all tuwaachie wanaoendelea na uchunguzi
 
DAKTA AJIBU HAYA. 1.Anauhakika Gani Kama Sm Hy Ilikuwa Kwa Ajiri Ya Kuomba Maelekezo Ya Daktari Bila Ya Kuhakiki Kwenye Ofisi Za Kampuni La Sm Kuangalia Kama Kweli Muda Huo Huyo Nesi Alikuwa Anaongea Na Daktari?Je Mazungumzo Yao Yalihusu Huyo Mgonjwa?2.Mgonjwa Huyo Walimpokea Mapema,wakampima Wakajua Mimba Yake Siyo Ya Kawaida Na Kwa Kuzingatia Umri Wa Binti Anaejifungua Kwanini Hawakuchukua Tahadhari Tangu Mapema Na Kama Hayo Maelekezo Kwanini Hayakutolewa Tangu Awali Na Huku Walijua Tatizo Lake Mapema? Huu Siyo Uzembe?3.Daktari Kupigiwa Sm Inaonesha Hakuwepo Kituo Cha Kazi,kwanini Hakuwepo Mbona Hajaeleza Daktari Muda Huo Alikuwa Wapi?4.Na Kama Tatizo Lilihitaji Daktari,ilikuwaje Nesi Wa Wodi Ya Jirani Akatoka Akaenda Kumhudumia Na Huyo Nesi Akaendelea Kuongea Na Sm Tu?Si Na Yeye Angesema Siwezi Kwa Sababu Tatizo Hl Linahitaji Hadi Daktari?5.Hv Hospitali Nzima Huwa Na Daktari Mmoja Tu?6.Kwanini Hakuwasikiliza Upande Wa Wafiwa Nao Watoe Yao Moyoni?7Kwanini Ametumia Nguvu Kubwa Sana Kumlinda Huyo Nesi?
 
Ukweli hospital za serikali tanzania ukienda kutibiwa jiandae kwa mambo mawili, KUPOTEZA MAISHA au kupata ULEMAVU. wauguzi wote na madaktari hawajari always ni watu wenye dharau na kurahisisha jambo. gram 500 kweli watoto walikuwa bado sana, ila je ilishindikana kuokoa maisha ya mama?

poleni sana wanafamilia.
 
Inaumiza sana kuona vifo vinavyosababishwa na uzazi!

Lakini hata hivyo hawa manesi humu mahospitali wapo wachache sana na wagonjwa ni wengi sana inakuwa vigumu sana kutoa huduma kwa wagonjwa wote kwa wakati mmoja.

Serikali inapaswa kuboresha huduma za Afya ili kuondoa matatizo kama haya.
 
Inasikitisha sana. Huu ni ukatili kama inawezekana afukuzwe kazi na kupelekwa mahakanani iwe fundisho kwa wengine.

Kwa nini watu wanakuwa hawana hata chembe ya huruma na uhai wa wenzao. Kitakachoshangaza ni.kuwa hamna hatua yoyote ya kinidhamu itakayochukuliwa kuhusu huu ukatili.
afukuzwe kazi kwa lipi,mganga mkuu kaeleza mimba ilikuwa na miezi sita,sasa watoto wangesurvive vp
 
Back
Top Bottom