tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mwibara kupitia ACT Wazalendo Cyprian Musiba ameahidi kuzilinda kura zote atakazopigiwa na wananchi katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Musiba amesema hayo Agosti 31, 2025 akizungumza na waandishi wa habari wilayani Bunda akiwaomba wananchi kumpigia kura kwa wingi na kumsaidia kuzilinda.
Soma pia: Musiba: Mimi nilikuwa na ndoto ya kuwasidia wananchi Mwibara lakini naona inapotea
"wananchi nendeni mkanipigie kura mimi nitadhibiti hizo kura kuliko mnavyofikiria" Musiba
Ameongeza kuwa ataweza kudhibiti mianya yoyote ya wizi wa kura kutoka kwa mpinzani wake.
"huyo mpinzani wangu mkuu huyo Mzee hatoniibia kura na nitalinda kura zangu vibaya sana wananchi wenzangu tutalinda kura kwa kushirikiana na nyie".
Aidha amesisitiza mwaka huu atapata ushindi wa kishindo na kihistoria.
"kwa sababu ushindi sio asilimia sabini (70%) mimi nataka nimshinde mpinzani wangu kwa asilimia tisini na nane (98%)" amesema Musiba.
Musiba amesema hayo Agosti 31, 2025 akizungumza na waandishi wa habari wilayani Bunda akiwaomba wananchi kumpigia kura kwa wingi na kumsaidia kuzilinda.
Soma pia: Musiba: Mimi nilikuwa na ndoto ya kuwasidia wananchi Mwibara lakini naona inapotea
"wananchi nendeni mkanipigie kura mimi nitadhibiti hizo kura kuliko mnavyofikiria" Musiba
Ameongeza kuwa ataweza kudhibiti mianya yoyote ya wizi wa kura kutoka kwa mpinzani wake.
"huyo mpinzani wangu mkuu huyo Mzee hatoniibia kura na nitalinda kura zangu vibaya sana wananchi wenzangu tutalinda kura kwa kushirikiana na nyie".
Aidha amesisitiza mwaka huu atapata ushindi wa kishindo na kihistoria.
"kwa sababu ushindi sio asilimia sabini (70%) mimi nataka nimshinde mpinzani wangu kwa asilimia tisini na nane (98%)" amesema Musiba.