Muongozo Wa Biashara ya microfinance

Joined
Jun 28, 2018
Posts
11
Reaction score
11
Habari Zenu wakuu!!!!

Nataka anzisha biashara ya MICROFINANCE lakini Nimefanya utafiti nimeona lazima niwe na mtaji wa 20M ndo nipate kibali BOT , Sasa apa nikipiga hesabu kufikisha 20M ,Ni mpaka mwakani 2026, kwa savings zangu nazofanya kwa Sasa!

Swali Je, hii biashara huwezi kuiendesha bila leseni ??
Naheshimu mawazo yako!, karibu
 
Sheria ya Taasisi za Fedha za Microfinance ya mwaka 2018 (The Microfinance Act, 2018) na kanuni zake zimeweka bayana kuwa:

1. Ni kosa la jinai kuendesha biashara ya microfinance bila kusajiliwa au kupata leseni kutoka BoT.

Adhabu: Faini kubwa, kifungo au vyote kwa pamoja kwa mtu binafsi au kampuni.

2. BoT ndiyo msimamizi mkuu wa sekta ya microfinance.

Inasimamia masharti ya leseni, mitaji, ukaguzi wa fedha, na maadili ya uendeshaji wa taasisi hizo.
 
Unaweza kujilipua, ila ukitapeliwa hutokuwa na nguvu ya kuwashtaki.
 
  • Njia nyingine, unaweza kuanzisha mahusiano na mtumishi (mwalimu, nesi n.k) akukopee maisha yaendelee.
  • Au unaweza kumtafuta mshirika, ukampa wazo lako na akiliona lina faida , muunganishe mitaji.
  • Au tushawishi sisi wanabodi 1000 tununue hisa ya 20,000/= kazi ianze
 
Huu mchakato ulishawahi kuletwa humu 2011, Watu wakapita na fuko lote la hela 🤣
Nilipigwa 250,000 na aliyekuwa anajifanya kama ES wa huo mchakato
 
Huwezi kuendesha biashara bila liseni kwasababu hata wewe utataka uanao wakopesha wawe na liseni

Usipo fuata utaratibu wa uanzishaji biashara huko mbeleni kuna mtu anaweza kudai kwamba hiyo ni biashara yk kuna vitu ving hapa duniani i hakuna aijuae kesho
 
Huu mchakato ulishawahi kuletwa humu 2011, Watu wakapita na fuko lote la hela 🤣
Nilipigwa 250,000 na aliyekuwa anajifanya kama ES wa huo mchakato
Makosa yaliyopelekea kupigwa salio kipindi hicho, iwe funzo katika kurekebisha dili lijalo; baada ya kupata uzoefu, ili watu wasipigwe tena ni nini kifanyike?
 
Ili ufungue biashara ya kukopesha bila leseni labda uwe loan shark.

Unamkopesha mtu unakaa na ATM card yake, mshahara ukiingia unachomoa malipo yako unarudisha kadi.

Ukikuta kashatumia sim banking unamtumia kigang cha kumnyoosha. Yaani inabidi uwe loan shark haswa riba ya asilimia mpaka 40.

Kwa kifupi udaiji unakua mara mia ya model ya Oya Microfinance
 
Leseni Leseni Leseni kutoka BOT
 
Mipango ilikuwa kabambe Mkuu sema vidole hivi navyo vina shida sana 🤣
Sisi waafrika kwenye biashara ya ubia hatuko vizuri, mwanzo mtaanza vizuri ila mapato yakianza kuonekana, maigizo yanaanza kuwa mengi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…