Mzee Wa Republican
JF-Expert Member
- Jul 20, 2013
- 1,663
- 840
Ndugu wananchi, wanabodi na great thinkers wa humu JF Salaam !!
Tayari mwaka 2023 umeanza kwa kasi na kama ilivyo ada tumeendelea na pilika pilika za kusaka maisha kona mbali mbali.
Katika harakati za kujikwamua kiuchumi nimefikiria kufanya biashara ya kukopesha pesa (Microfinance). Kiufupi ni biashara ambayo kwa sasa ina sheria nyingi kali na hata leseni yake kwa sasa hutolewa na benki kuu wenyewe (BOT).
Moja ya masharti yake makali ni kwamba ni lazima uwe na mtaji usiopungua milioni 20, na pesa hiyo isiwe ya kukopa.
Kibongo bongo kwa sharti hili wengi ni ngumu kuanzisha biashara hii (labda uwe mfanyabiashara) au kama ni mtumishi basi ni lazima uwe umefanya saving kwa muda mrefu sana au uuze asset yako mf kiwanja na kadhalika.
Sanjari na hayo masharti yake, nimekuja mbele zenu kuomba ushauri na uzoefu kuhusu biashara husika kwani humu ndani naamini kuna watu wenye uzoefu wa biashara mbali mbali ikiwemo na hii.
Nitafurahi kama nitapata mrejesho kuhusu changamoto za biashara hii, fursa zake, namna ya kuiendesha, tabia za wakopaji na mazingira mengine anuai yanayoizunguka sekta hii kwa sasa.
Ni imani yangu ya kwamba nitapata mwangaza zaidi baada ya kuleta wazo langu mbele yenu.
Uchumi wa Tanzania utajengwa na watanzania wenyewe.
Naomba kuwasilisha mbele zenu wakuu . . . . . .!
Tayari mwaka 2023 umeanza kwa kasi na kama ilivyo ada tumeendelea na pilika pilika za kusaka maisha kona mbali mbali.
Katika harakati za kujikwamua kiuchumi nimefikiria kufanya biashara ya kukopesha pesa (Microfinance). Kiufupi ni biashara ambayo kwa sasa ina sheria nyingi kali na hata leseni yake kwa sasa hutolewa na benki kuu wenyewe (BOT).
Moja ya masharti yake makali ni kwamba ni lazima uwe na mtaji usiopungua milioni 20, na pesa hiyo isiwe ya kukopa.
Kibongo bongo kwa sharti hili wengi ni ngumu kuanzisha biashara hii (labda uwe mfanyabiashara) au kama ni mtumishi basi ni lazima uwe umefanya saving kwa muda mrefu sana au uuze asset yako mf kiwanja na kadhalika.
Sanjari na hayo masharti yake, nimekuja mbele zenu kuomba ushauri na uzoefu kuhusu biashara husika kwani humu ndani naamini kuna watu wenye uzoefu wa biashara mbali mbali ikiwemo na hii.
Nitafurahi kama nitapata mrejesho kuhusu changamoto za biashara hii, fursa zake, namna ya kuiendesha, tabia za wakopaji na mazingira mengine anuai yanayoizunguka sekta hii kwa sasa.
Ni imani yangu ya kwamba nitapata mwangaza zaidi baada ya kuleta wazo langu mbele yenu.
Uchumi wa Tanzania utajengwa na watanzania wenyewe.
Naomba kuwasilisha mbele zenu wakuu . . . . . .!