Muongo Vs. Mengi. Kimenuka !

Sishangai lions viongozi wa serikali iliyopo madarakani kulinda maslahi ya wageni na hasa weupe,nijuavyo mimi wanajua wazi wakiwapa wageni watapata ten percent.inashangaza eti waziri anasema ni aghali sana kuwekeza kwenye utafiti wa gas, kisima kimoja kinakaribia 100 billion,nani aliiyemwambia watanzania hawana hizo pesa kama ni swala la wataalam si wanaweza kuajiriwa tu,kwani shida iko wapi?nakumbuka wakati wa utawala wa mkapa bwana Mengi alinyimwa kuwekeza Kilimanjaro hoteli na akapewa mwarabu.Hii ndio Tanzania,viongozi vichaa
 
Huyu Mengi alishawahi kuibuka na issue ya mafisadi papa!Jiulize iliishaje?

Wewe ndiye Kilaza kweli sasa ulitaka Mengi awakamate? Yeye alitoa taarifa kwa umma kam ingekuwa siyo kweli si wangemshitaki kwa kuwadhalilisha? Mbona husemi kashifa ya Kamanda Nzow kutaka kumbambikizia madawa ya kulevya mtoto wake mbona serikali na waliotajwa hadharani hawakuchukua hatua yoyote kama walisingiziwa? I think you have personal conflict with mzee Mengi! Siyo bure, utakuwa unakula kwa akina Yusuf Manji!
 

Moja za athari tunazopata kwa kuwategemea foreign investors ni suala la ajira. Hawa jamaa huwa wanaajiri karibu nyanja zote muhimu watu wao wanaokuja nao. Nafasi za chini ndio wenyeji wanaachiwa. Ingekuwa busara na jambo la msingi kama tungekuwa tunawapa kipaumbele wazawa katika uwekezaji. Hii ingesaidia sana kuongeza nafasi za ajira. Na mawazo ya kwamba wenyeji hawawezi mimi nadhani ni mawazo ya kizamani. Tukiendelea na fikra za namna hii tutabakia kuendeshewa miradi yetu na wageni na kuendelea kuibiwa. Kina BAKHRESA, MENGI and the like wamelifanyia taifa makubwa sana katika kutengeneza ajira. Ni vyema kuthamini mchango wao sasa.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo la watanzania tunapenda sana kupakwa mafuta ili hali kweli hatuwezi.Kila sehemu tunapenda usanii.Prof aliona billioner wa bongo amewekeza sana kwenye viwanda vya vyakula ndio maana akasema ukweli gasi hatuwezi.uwekezaji katika Gas si mchezo.hata maofisini mbogo akikosea anataka aambiwe kwa kubembelezwa,ndio maana hatufiki.
 


Mkuu Zinedine

Shukran sana,Fikra zako ni pevu sana,
Nimekusoma kwa utuvu wa hali ya juu.
 
Last edited by a moderator:

Msidhani Mengi anawatetea watanzania kwa hili. Anatetea maslahi yake binafsi. Kila uwekezaji akikosa lazima apige kelele. Kilimanjaro Hotel ilikuwa hivyo hivyo. Hivi tujiuliza uwekezaji ule ulifanikiwa au la? Je Mengi angeweza kuwekeza pesa aliyowekekeza mwarabu?
 

Meningitis huwa naheshimu sana comments zako lkn kwa hapa tupingane bila kupigana. Aliyekudanganya watz hatuna uwezo ni nani?
Mimi ninao. Ninawafahamu wengi tu walio na uwezo. Tatizo ni kukariri kama baba wa taifa alivyokwisha sema, viongozi wengi (kama siyo wote) tulionao leo wanaamini mawazo yao ndiyo mawazo ya watanzania na mitizamo yao(hofu zao) ndiyo mitizamo ya watz.
Hii siyo kweli...its kind of a brainwash technique our leaders are happily nurturing oblivious of the deadly consequences.

HAKUNA TAIFA LOLOTE DUNIANI LILILOJENGWA NA WAWEKEZAJI WA NJE HUKU WA NDANI WAKIWA WATAZAMAJI. HAKUNA. PERIOD
 
Huyu ni Professor wakuteuliwa, Mbunge wa kuteuliwa, Waziri wa kuteuliwa. Hiyo ndio output ya kuteuliwa kwa kila kitu....
 
Tanzania shamba la bibi
 
krap kabisa hii

You cant let outsiders run these shows, it is the responsibility of the government to build local ownership na sio kusema sisi hatuwezi.... if that is the case what is the use of his education??

Imbechili at work
Eyes can not see if the mind does not know!
 
Mkuu usipende kuamini ngonjera za kina Mengi!
Niambie ni mtanzania au kampuni ya kitanzania gani aliyewekeza katika tafiti za rasilimali zetu hasa hayo mafuta na gesi?
Kina mengi wabakie kuuza soda na juisi tu,wasijidai na kujikweza kwa vitu wasivyoviweza.
Watanzania hatujawekeza katika utaalamu vya kutosha!tunatakiwa kufanya hivyo sasa...
 

mkuu kwani Muhongo alichaguliwa na nani hadi awajali walalahoi ? Si inasemekana alipigiwa simu ya uteuzi akiwa anakula bata mahali ! Aogope nini tena mjomba !
 
Muhongo ni tapeli. Huyu jamaa muulizeni nani alimvunja mguu.....

Ana roho mbaya hadi kumuua mkewe, nyang'au
 
Ugomvi wangu na Mengi ni mmoja tu!
Ni mzee mnafiki sana ....hasimami na wanaharakati wa kweli,ni mtu wa kuangalia maslahi yake akifanikiwa anawaacha kwenye mataa.Kumbuka Mengi ni mwanaccm na inayofanya hayo mnayoyalalamikia ni ccm.kwa nini asitumie influance yake kushawishi chama chake katika hili na mengine mengi?
By the way nasubiri ile hospitali ya magonjwa ya moyo aliyotuahidi kuijenga.

Mengi ni mfanya biashara na sio mwekezaji ...bado sana kuwa mwekezaji hasa hasa unapoongelea uwekezaji katika mafuta au gesi!
Ukimsikia Mengi analaumu ujue hilo jambo limathiri maslahi yake binafsi na si watanzania kwa ujumla.
 

Kumbe kuna tofauti Kati ya kuwekeza na kufanya biashara?? Mwekezaji hafanyi biashara?? Wasomi nyie muna taabu sana mlisoma ili mtumikie wazungu Nadhani...🙄🙄
 
Eti nani...Profesa Muongo au Profesa Muhogo au Profesa Muhongo?
Lakini anaweza asiwe mbali na ukweli. Kama vitalu vya wanyama pori watanzania tunashindwa kuwinda ipasavyo badala yake tunavifanyia udalali sembuse vitalu vya mafuta na gesi vinavyo hitaji uwekezaji wa madola mamilioni! Huyo Mengi anao ubavu wa kuwekeza katika vitalu vya mafuta? I think labda anataka vitalu ili afanye udalali au aalike makampuni ya nje ili agawiwe hisa vinginevyo atauza IPP yake mpaka mbwa wa nyumbani kwake! ndio udalali kwa kila kitu tulionao watanzania...udali wa vyumba, udalali wa nyumba, udalalai wa viwanja, udalali wa mashamba, udalali wa magari....mpaka udalali wa wanawake (super stars wa kibongo)! Hey guys let's be serious when it comes to the matter of heavy investiments!
 
Kumbe kuna tofauti Kati ya kuwekeza na kufanya biashara?? Mwekezaji hafanyi biashara?? Wasomi nyie muna taabu sana mlisoma ili mtumikie wazungu Nadhani...🙄🙄

In business, to make money you need two critical assets: Customers and Employees. While in Investments, to make money you need two different kinds of assets: Money and Experience.

wewe bwana chesco endelea kufanya biashara ya maparachichi lakini kamwe usijidai una uwezo wa uwekezaji...labda baadae sana tena sio kwenye field ya mafuta.
 
Sasa Kwani bank zimeenda wapi kwasababu unaweza kopa hizo pesa kwa banks ilimradi uwathibitishie kuwa unachofanya kitawarudishia pesa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…