Dhambi wanazofanya viongozi wa CCM na ufirauni walioifanyia nchi hii hata shetani angeambiwa afanye hizo dhambi angeogopa, zinatisha, sidhani kama sala yako itasikilizwa na Mungu....
CCM ni sawa na sikio la kufa halisikii dawa, uthibitisho ni kitendo cha mtu ambaye angekinusuru chama wakati huu mgumu kaenda zake Malawi baada ya kurejea toka kwa Maximo
Na mapinduzi yameanza mwezi huu na CCM itakufa mwezi huu.
hata mwalimu alishasema mwisho wa ccm,ni utengano ndani ya chama,so now iz timd 2separate completily.
Na hasalimiki mtu
Twasubiri miujiza ya mwenyezi mungu ili tupate okoka katika lundo la kashfa na tuhuma mitaani na bungeni. Mie leo nimepata taabu kusikiliza mazungumzo ndani ya daladala toka Gongo la Mboto hadi Posta;
njia yote ni kukisema vibaya chama chetu tukipendacho CCM.
Ilikuwa ni kushindana kutoa msururu wa kashfa dhidi ya CCM kana kwamba chama chetu hakijafanya jambo lolote la maana kwa watanzania.
Ilibidi Tazara nishuke katika lile daladala nichukue bodaboda kwani uvumilivu ulikuwa mdogo, wasafiri hawana na neno zuri kwa CCM niipendayo.
Mungu toa nguvu kwa viongozi wetu waamuke na kufanya mageuzi ndani ya CCM ilu mvuto urudi kama enzi za mwalimu.
MUNGU SAIDIA CCM ili WATZ wafunguke warudi tena chamani