Mungu husema na Watu

Mungu husema na Watu

Ameen mkuu...kuna orphanage centre IPO jirani hapa...itabid niitembelee hata kwa kutoa kidogo nilichonacho
Ameeen na utaongezewa pale ulipopunguza, wakati wa Toba na kusaidia wenye uhitaji huu TOA kwa wenye uhitaji ubarikiwe, wakisema 'Asante' na kufurahia ulichowapatia wewe tayari ushapokea Baraka hadi hapo
 
Ameeen na utaongezewa pale ulipopunguza, wakati wa Toba na kusaidia wenye uhitaji huu TOA kwa wenye uhitaji ubarikiwe, wakisema 'Asante' na kufurahia ulichowapatia wewe tayari ushapokea Baraka hadi hapo
Amen...nmedhamiria kabisa mkuu ...Kuna vitu unafanya unaona haviend kumbe vimekosa baraka kutoka kwa Mungu....nitajitahid sanaa kufanya Toba na kujipatanisha na Mungu
 
Tafadhari waone Wataalamu Wa Magonjwa ya Akili haraka...!

Kuna Kitu Wanakiita 'Hallucinations'...

Unaweza Kuona au kusikia vitu ambavyo havipo.....!

Wakikuona jinsi ulivyo halafu wakapata historia ya yanayokusibu,bila shaka Watapata ugonjwa wako,niamini Mimi Watakuanzishia dawa..!
Hata wavuta bangi upata hallucinations
Kwaiyo Mtoa mada asijione special Sana
 
Huu mwaka nmechelewa sanaa....ila kuanzia mwez huu nimeamua kufanya Toba na kumrudia Mungu kwani nmejiona kama nmejiweka mbali nae...Kuna mambo yangu naona kabisa hayaendi kwa sababu ya kutokumshirikisha Mungu....hakika naona atanionekania na kunifanya kuwa mpya
Mungu akubariki kwa uamuzi huo. Ila kwenye safari yako ya marejeo, ukitaka umwone Mungu, wala usilenge kwamba umrudie ili mambo yako yawe bora, material things kwa Mungu wetu ni sawa na kachumbari au pilipili ya kuweka kwenye chakula tu, yaani ni kitu cha ziada ila chakula halisi kipo. Bali utafuteni kwanza Ufalme wake na haki yake na mengine yote mtazidishiwa.

nakuomba, lenga kutakaswa roho yako na kukaa katika uwepo wa Mungu moyoni mwako, yaani Mungu akae ndani yako, akishafika tu, hayo mengine ni marupurupu tu atakupa hata yale usiyoyaomba kwasababu anajua tunayohitaji. sawa na mtoto anaomba umpe pipi kumbe wewe ulipanga umnunulie baiskeli, mtoto wako yupo shule anaomba umpe elfu kumbi wakati wewe unaona uhitaji wakeni zaidi na ulipanga umpe laki moja. Mungu akiwa ndani yako hayo mengine ni ziada tu na tutapata na kusaza.

uwepo wa Mungu utakujaje kwako? ni kwa kusoma sana Neno la Mungu, tenga muda wa kusoma sana, pili, kwa kufanya maombi na kama umebahatika kujazwa Roho Mtakatifu, maombi ya Roho na kushiriki ibada.
 
That's the communication between mind (brain) and heart (soul), hayo ni mawasiliano baina ya Nafsi na Roho, like what do you feel? What do you experience? The eyes, after all, are the mirrors of the soul,
sisi wenzio tunatumia Neno la Mungu, upo ushahidi wa Neno la Mungu kua Mungu ameongea na watu, pia hata sisi wenyewe tulishawahi kuongea na Mungu, tunajua nini ni mawasiliano ya brain na soul yako tu, na tunajua nini ni mawasiliano ya Mungu. hayo ya Mungu ni halisi, na yale yasiyo ya Mungu ni halisi pia, vimejitofautisha na yule mwenye Mungu moyoni analijua hili. wale wasio na Mungu hawawezi kabisa kujua tunaongea nini hapa.
 
Back
Top Bottom