Ukiongea na Mungu utakua ushakufa, huyo ni wewe alie ndani yako nazungumzia Roho, anaitwa 'spirit guide' wewe una timu ya Malaika na Mungu yupo pamoja nawe km Muumba wako, Ila anaeku-guide na kukuongoza hichi fanya na hichi usifanye ni 'spirit guide' namaanisha ni Roho, anakuongoza uweze kutofautisha kati ya nini unahitaji na nini unataka, yeye ndio anakuongoza pita huku na huku usipite au pita hivi kata hapa usikae pale kaa pale kule usiende nenda kule ondoka hapo usiondoke saa 2 ondoka saa 7 hizo zote anakulinda na kukuongoza kuelekea kumfikia huyo Mungu ambae ni muumba wako
Ndugu yangu, tunaongea na Mungu hivi hivi tukiwa hai, kabisa kabisa. Mungu huwa anaongea na watu, anaamua tu aina ya communication ipi atumie, wengine wanasikia sauti kabisa kama mimi na wewe tunapoongea na kujibizana kabisa, Mungu ni halisi, sio story. wengine Mungu anaongea nao kwa ndoto, wengine kwa sauti ya ndani, wengine kwa Neno la Mungu unasoma Biblia halafu mistari yote unaona ya kawaida ila upo mmoja tu ambao unachoma na kuongea na wewe na unajua kwamba ni Mungu anaongea, wengine Mungu anaongea nao kwa maono ya waziwazi au ya usingizini n.k,
wengine Mungu anawatumia malaika waje kukuambia wakiwa wamevaa aidha mwili wa mwanadamu au wakiwa vilevile kama malaika walivyo. Samweli alisikia sauti ya Mungu kabisa ikimuita, Yesu aliposhuka kubatizwa sauti ilitoka mbinguni ikisema Huyo ndiye mwanangu mpendwa msikieni yeye na wote waliokuwepo walisikia ile sauti, Yesu alipopanda mlimani na Petro yohana na yakobo kuomba akabadilika sura ikawa inamng'aa Musa na Eliya wakashuka kumhudumia sauti ilitoka na wanafunzi hao walisikia kabisa,
Petro alipokuwa gerezani malaika alienda kumtoa gerezani akamwambia aelekee wapi hadi nje, mambo mengi mengi. mimi binafsi Mungu ameongea na mimi mara nyingi sana hadi huwa naogopa.
Juzi wakati natype hapahapa JF Mungu aliongea nami kwa sauti ya ndani kwamba "MUNGU ANAPENDA SANA KUWA NA UHUSIANO WA KARIBU NA WANADAMU", yaani kama uhusiano wa baba na mtoto, umwabudu, umsifu, umheshimu, umsikilize, umuombe mahitaji mbalimbali n.k, Mungu anapenda hivyo, ameongea na mimi. sijui nikuelezeje?