Mungu hana sifa tatu, tu!

Mungu hana sifa tatu, tu!

Umesema si mtaalamu, chukua somo la bure leo. Hata hydrogen inaweza kupatikana kama kimiminika, si gesi tu.


Mwalimu anaweka chaguzi kwa sababu hana uwezo wa kuingia kichwani kwako na kukupima unajua nini na hujui nini.

Mungu anayejua kila kitu na kuweza kila kitu anaweka uchaguzi ili iweje?

Kwa nini asingeweka mazuri matupu mabaya yasiwepo?

Angefanya hivyo angepungukiwa nini?
Mkuu
Nashukuru kwa somo, japokuwa naona umerudia tu nilichoandika kwenye post namba #36 kwa maneno tofauti.

Sasa umeanza kuuliza maswali yenye maana, na tunaweza kufikia hitimisho vizuri. Tunapouliza maswali ya 'Kwa Nini' Mungu amefanya hivi ama vile na si hivi ama vile, tunajaribu kujua Nia ya Mungu. Na kama tukiweza kujua kwa ufasaha (kwa kutumia akili zetu wenyewe), tutakuwa tunajua sawa na Mungu ( Ujuzi wote) kitu ambacho haiyamkiniki kikawa.

Inaonesha mkuu Kiranga ungependa sana Mungu angeumba ulimwengu ambao kuna mema tu, hakuna mabaya. Nafikiri kwako, kuumba ulimwengu wa namna hiyo ni kuthibitisha kwamba Mungu anaweza yote. Lakini habari njema kwako na kwa wengine ni kwamba ulimwengu huo ulikwisha kuumbwa na Mungu zamani kabisa, na hata ukitaka kwenda huko inawezekana.

Ulimwengu huu tuliopo umeumbwa kwa namna ambayo mema na mabaya yanaweza kutokea. Kuna ulimwengu unaoitwa Mbingu, huo ni mahali ambapo mema tu yanaweza kuwepo, mabaya yote hayako/hayatakuwepo huko. Kuna ulimwengu unaoitwa Kuzimu/Jehanamu, huko kuna mabaya tu, mema hayatakuwepo huko. Tumepewa uhuru wa kuchagua tutapenda kwenda kwenye ulimwengu upi kati ya hizo.
 
Kitendo tu cha wewe kusema ukristo ndio Dini pekee ya kweli najiuliza una ushahidi gani? What about Buddha,Hindus, Islam?
 
Mkuu
Kuna sifa tatu za Mungu (Upendo, Uwezo na Ujuzi) ambazo zinatumiwa na baadhi ya watu kwamba zinajipinga/zinapingana na uhalisia wa ulimwengu huu. Ninachomaanisha ni kwamba Mungu ana sifa nyingi zaidi ya hizo, ambazo ni muhimu tunapojaribu kuelezea jambo lolote katika ulimwengu huu.
Kwanini Mungu anaruhusu matetemeko ya ardhi? Vimbunga? Mafuriko? Still ana uwezo wa kuzuia yote haya yasitokee
 
Unajiita big mind halafu unaandika utumbo? shame on u.!
Wewe ndiyo fala kabisa unayetaka kumpangia Mungu ni wakati na mida gani aruhusu watu wafe..!

Mimi ni bigmind kweli, maana ulivyofala huwezi jua nini kitakutokea dakika mbili zijazo, iweje atuhumiwe Mungu eti anaua wake? Wewe ukichinja kuku wako unakuwa na kosa? Au hao kuku unakuwa huwapendi??

Only God created us and He is only who known our beginning and end in this world. Stop pretending to know one destiny's...! Haya twambie nini kilitakiwa kuwa kifo chao na mpaka useme walikufa kimakosa??
 
Hivi huyo Mungu wenu inamana alishindwa kumwinua nabii/mtume katikati ya waAfrika hadi tumjue kupitia watu wa mbali????
Inamana kwa kufanya ivyo hakujua kwamba kutatokea watu ambao hawataamini uwepo wake??
Mkuu ukristo na uislam hivi vitu sio kwaajili yetu cc waafrika just think about this mitume yote ya kwao vitabu vya kwao munngu wa kwao baraka zote ktk kwamungu za kwao pamoja na kugeuzana na kulalana wanaume kwa wanaume still mungu akawapa nchi ya ahadi akawapendelea wakawa taifa teule duuh
 
Kitendo tu cha wewe kusema ukristo ndio Dini pekee ya kweli najiuliza una ushahidi gani? What about Buddha,Hindus, Islam?
Mkuu
Nimeeleza hapo juu kwa nini nimeandika hivyo, ili kurahisisha kunielewa kwenye baadhi ya hoja nitakazotoa. Si kusudi la uzi huu kuthibitisha hilo. Tujikite na kusudi la uzi huu.
 
Kwanini Mungu anaruhusu matetemeko ya ardhi? Vimbunga? Mafuriko? Still ana uwezo wa kuzuia yote haya yasitokee
Mkuu
Maswali uliyouliza ndiyo hasa ninachokueleza tangu mwanzo, zifahamu sifa zingine za Mungu na utajua kwa nini vitu hivyo hutokea. Mungu hatendi jambo ati kwa sababu tu anaweza kulitenda. Hata wewe unaweza mambo mengi tu ambayo huyatendi,...
Nimeeleza zaidi hapo #41
 
Tusianzishe nyuzi ili tu tuonekane tumeandika. Sielewi lengo hasa la mwanzisha uzi huu zaidi ya kutaka ukristo utukanwe humu. Hebu jaribu kutoa pointi za kutetea ulichoandika..... sio uboronge wengine watukanwe!
 
Idea ya Mungu mmoja mwenye sifa zote asiyekuwa na mapungufu hata siku moja haiwezi kuwa na mantiki katika ulimwengu wetu.

Hata siku moja watu wa dini wanaoamini Mungu mmoja hawataweza kuthibitisha kimantiki.. Narudia tena ni kuthibitisha kimantiki bila ya contradiction ya aina yoyote ile Idea ya Mungu mmoja.

Wagiriki waliona hizi shida za kusema kuna Mungu mmoja ambaye ndo sababu ya kila jambo linalotokea ulimwenguni ni idea ngumu mno, wakaamua kuanzisha imani ya kuwa na Miungu mingi.

Wagiriki wana Mungu wa upendo, Mungu wa uponyaji, Mungu wa uzazi, Mungu wa njaa, Mungu wa mvua na radi, mungu wa baharini, Mungu wa kila aina ya jambo nk!

Ina maana ukisema kwanini watu wanakufa kwa magonjwa, wao watakumabia Mungu wa uponyaji asa hivi amekasirika na jambo fulani ndo maana tunakufa kwa magonjwa... Ukisema kwanini mvua hazinyeshi mazao hakuna njaa watasema kuna Mungu wa mavuno na mvua ametuaksirikia.

Ila tukisema Mungu mmoja awe na upendo at the same time mjuzi wa kila kitu kilichopita, kijacho na cha sasa ana kila aina ya utimilifu alafu anaruhusu baadhi ya mambo ambayo yanawatesa wenye hatia na wasiokuwa na hatia ni ngumu sana kumeza hii... Hii idea ni ngumu kufafanuliwa ndo maana itabaki kuwa ni IMANI na tutaendelea kuiheshimu ila kuithibitisha kimantiki haitakuja kuwezekana.
 
huwezi kumshinda alieumba hakuna kisicho na sababu huu ni mtihani kwetu uovu upo kwasababu mtu anachagua mwenyewe na kila elimu imetoka kwake utajiuliza kwann kaumba uchawi? kuna alipo paumba hakuna bugudha ya aina yoyote ile ambapo ni peponi........

mwalimu anapotoa mtihani anakujalibu pale anapohisi ulipasahau ili kupima kumbukumbu zako ni sawa tunavyoribiwa sisi na uovu je tutatiii au tutakengeuka
Umejibu vizuri sana.

Kama ambavyomchanganyiko wa kuweka maji na Pepsi hauondoi ubaya wa mkojo, hivyo hivyo, unaposema "Mungu hana sifa tatu tu" sifa zake nyingine haziondoi sifa zake tatu.

Ni hivi.

Sifa yoyote utakayompa Mungu haiwezi kuondoa contradiction ya "the problem of evil" bila kuzaa contradiction nyingine.

Jaribu kufanya "thought experiemnt" hapa umpe Mungu sifa yoyote uone kama itaondoa "the problem of evil" bila kuleta contradiction nyingine.

Sababu hiyo hiyo iliyokufanya ukatae mchanganyiko wenye mkojo, ilitakiwa ikifanye umkatae Mungu mwenye uwezo wa kuzuia maovu ambaye anayaruhusu, kuruhusu maovu ni mkojo nao.

Sasa unachofanya kwa huyo Mungu unasema "Huyu Mungu si mkojo tu, kuna maji na Pepsi vimechanganywa, nakunywa, kwa sababu si mkojo tu"

Mbona pale juu umekataa kunywa maji yaliyochanganywa na mkojo na Pepsi, halafu kwa huyu Mungu unakubali kunywa maji yaliyochanganywa na mkojo na Pepsi?

Umeelewa unapojichanganya?
 
Idea ya Mungu mmoja mwenye sifa zote asiyekuwa na mapungufu hata siku moja haiwezi kuwa na mantiki katika ulimwengu wetu.

Hata siku moja watu wa dini wanaoamini Mungu mmoja hawataweza kuthibitisha kimantiki.. Narudia tena ni kuthibitisha kimantiki bila ya contradiction ya aina yoyote ile Idea ya Mungu mmoja.

Wagiriki waliona hizi shida za kusema kuna Mungu mmoja ambaye ndo sababu ya kila jambo linalotokea ulimwenguni ni idea ngumu mno, wakaamua kuanzisha imani ya kuwa na Miungu mingi.

Wagiriki wana Mungu wa upendo, Mungu wa uponyaji, Mungu wa uzazi, Mungu wa njaa, Mungu wa mvua na radi, mungu wa baharini, Mungu wa kila aina ya jambo nk!

Ina maana ukisema kwanini watu wanakufa kwa magonjwa, wao watakumabia Mungu wa uponyaji asa hivi amekasirika na jambo fulani ndo maana tunakufa kwa magonjwa... Ukisema kwanini mvua hazinyeshi mazao hakuna njaa watasema kuna Mungu wa mavuno na mvua ametuaksirikia.

Ila tukisema Mungu mmoja awe na upendo at the same time mjuzi wa kila kitu kilichopita, kijacho na cha sasa ana kila aina ya utimilifu alafu anaruhusu baadhi ya mambo ambayo yanawatesa wenye hatia na wasiokuwa na hatia ni ngumu sana kumeza hii... Hii idea ni ngumu kufafanuliwa ndo maana itabaki kuwa ni IMANI na tutaendelea kuiheshimu ila kuithibitisha kimantiki haitakuja kuwezekana.
Unataka uthibitishiwe uwepo wa Mungu au unataka upate maelezo ya kuhusu Mungu na hekima zake?
 
Tatizo la wafia dini hawajui kwamba huyo Mungu anaepewa sifa zote izo alishindwa kuzuia biashara ya utumwa Africa
Watu waliuliwa/kulazimishwa kufuata hizi dini. Lakini bado mnaendelea kumtetea kwamba yupo
*smfh*
huko mbali " saudi arabia wameacha juzi tu kumfurumushia mabomu Yemen ''
kuna watoto " kuna wajane kuna lakini hilo mungu wala halioni na hana mpango nalo " Anawaacha tu wananchi wa Yemen wauwawe "...

halafu anatokea mtu ana sema Mungu ni mwenye upendo kwa watu wote
 
huko mbali " saudi arabia wameacha juzi tu kumfurumushia mabomu Yemen ''
kuna watoto " kuna wajane kuna lakini hilo mungu wala halioni na hana mpango nalo " Anawaacha tu wananchi wa Yemen wauwawe "...

halafu anatokea mtu ana sema Mungu ni mwenye upendo kwa watu wote
Mkuu
Kwa jinsi Mungu alivyo Mtakatifu, akichunguza maisha yako (na yangu) atatukuta na dhambi nyingi tu, kwa kifupi hatutakuwa tofauti na hao 'waarabu' unaowataja. Na kwa kuwahukumu hao, unapalia makaa kichwani pako mwenyewe. Lakini ikiwa humkumbushi Mungu kuhusu makosa yako mwenyewe, mbona unayataja ya wengine?

Watu wengi wanapenda kuona Mungu anaadhibu wakosaji, halafu wanasahau kwamba wao wenyewe ni miongoni mwa hao wakosaji. Kwa hiyo, ijapokuwa ni kweli kwamba Mungu ana upendo wote, lakini pia ana huruma yote. Hivi anaweza kumwonea huruma yule anayetenda kosa kama vile anavyomwonea huruma yule anayetendewa. Kisha anataja siku ambayo mambo hayo yote yatakomeshwa, Siku ya Hukumu. Tufanye juhudi kujiandaa kwa ajili ya siku hiyo.
 
huwezi kumshinda alieumba hakuna kisicho na sababu huu ni mtihani kwetu uovu upo kwasababu mtu anachagua mwenyewe na kila elimu imetoka kwake utajiuliza kwann kaumba uchawi? kuna alipo paumba hakuna bugudha ya aina yoyote ile ambapo ni peponi........

mwalimu anapotoa mtihani anakujalibu pale anapohisi ulipasahau ili kupima kumbukumbu zako ni sawa tunavyoribiwa sisi na uovu je tutatiii au tutakengeuka
Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?

Kama hakuna kisicho na sababu, Mungu sababu yake nini?

Mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao uovu hauwezekani kuwepo?

Tsunami linapopiga na kuua watu, watu wamechagua lipige?
 
Mkuu
Nashukuru kwa somo, japokuwa naona umerudia tu nilichoandika kwenye post namba #36 kwa maneno tofauti.

Kwako nikirudia siwezi kushangaa, you seem dense.

Sasa umeanza kuuliza maswali yenye maana,

Tuheshimiane tafadhali. Maswali yenye maana ukiyaona utayajua?

na tunaweza kufikia hitimisho vizuri.

Nani kakupa mamlaka ya kuhukumu hili kabla ya wakati?

Tunapouliza maswali ya 'Kwa Nini' Mungu amefanya hivi ama vile na si hivi ama vile, tunajaribu kujua Nia ya Mungu. Na kama tukiweza kujua kwa ufasaha (kwa kutumia akili zetu wenyewe), tutakuwa tunajua sawa na Mungu ( Ujuzi wote) kitu ambacho haiyamkiniki kikawa.

This is a priori fallacy. Umeanza kwa kusema Mungu hajulikani na kumficha Mungu wako wa uongo awe kapita uchunguzi.

Unamficha kwa sababu hayupo, huwezi kuthibitisha kwamba hayupo.

Naweza kukwambia chumbani kwako kuna tembo wa dhahabu ambaye haonekani kwa macho wala kugusika, hapigiki picha wala kunusika, hasikiki wala kujulikana kwa akili zetu.

Utanihakikishiaje kwamba huyu tembo hayupo?

Inaonesha mkuu Kiranga ungependa sana Mungu angeumba ulimwengu ambao kuna mema tu,

Hjaelewa ninachoandika, hujaelewa hujaelewa hujaelewa.

Kwa sababu akili yako ndogo.

Ushaelewa hilo? Akili yako ndogo hujui kusoma kwa comprehension.

Noinapohoji ulimwengu wenye mabaya kuumbwa na Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, hilo si kwa sababu mimi napenda ulimwengu usio na mabaya, ni kwa sababu ulimwengu ulio na mabaya hauko logically consistent na Mungu huyo.

Umeelewa hilo somo?

Unaelewa "logically consistent" maana yake ni nini?

hakuna mabaya. Nafikiri kwako, kuumba ulimwengu wa namna hiyo ni kuthibitisha kwamba Mungu anaweza yote. Lakini habari njema kwako na kwa wengine ni kwamba ulimwengu huo ulikwisha kuumbwa na Mungu zamani kabisa, na hata ukitaka kwenda huko inawezekana.

Thibitisha, usilete hadithi. Unaeweza kuthibitisha?

Ulimwengu huu tuliopo umeumbwa kwa namna ambayo mema na mabaya yanaweza kutokea. Kuna ulimwengu unaoitwa Mbingu, huo ni mahali ambapo mema tu yanaweza kuwepo, mabaya yote hayako/hayatakuwepo huko. Kuna ulimwengu unaoitwa Kuzimu/Jehanamu, huko kuna mabaya tu, mema hayatakuwepo huko. Tumepewa uhuru wa kuchagua tutapenda kwenda kwenye ulimwengu upi kati ya hizo.

Hujaelewa swali, hivyo huwezi kulijibu.

Swali si "kwa nini Mungu hakuumba ulimwengu ambao hauna mabaya popote", swali ni "kwa nini Mungu hakuumba ulimwengu ambao hauwezi kuwa na mabaya sehemu yoyote, wakati wowote".

Hujaelewa swali.

Sitegemei uweze kulijibu.

Si kwa ubongo huu wa kuparamia mambo usiyoyaelewa bila hata kuuliza.

Kwa sababu hata cha kuuliza hujui.

Hujui hata maana ya "logically consistent".

Hujui hata kama kuna liquid hydrogen.

Kabla ya kujitutumua sana, futa ujinga basic kwanza.
 
peponi hakuna tsunami wala bugudha alishapaumba so alishaumba vyote hivyo uthibitisho wangu ni wew kuwepo hapa lazima kuna source aliyeumba mtu wa kwanza ni nani? au alizuka
Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?

Kama hakuna kisicho na sababu, Mungu sababu yake nini?

Mungu alishindwa kuumba ulimwengu ambao uovu hauwezekani kuwepo?

Tsunami linapopiga na kuua watu, watu wamechagua lipige?
 
peponi hakuna tsunami wala bugudha alishapaumba so alishaumba vyote hivyo uthibitisho wangu ni wew kuwepo hapa lazima kuna source aliyeumba mtu wa kwanza ni nani? au alizuka
Sijauliza kama peponi kuna tsunami au hakuna. Na wewe huwezi kunithibitishia kwamba kuna pepo, na hizo habari za peponi si stories tu.

Kama unaweza thibitisha.

Nimeuliza kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kaachia tsunami liweze kupiga na kuua watu hapa duniani?

Nakuuliza habari za duniani, unanijibu za peponi.

Una akili wewe?

Kama kitu kuwepo lazima kuna source kwa nini unasema source yangu lazima iwe Mungu?

Na Mungu naye source yake nani?

Unaelewa ukisema kila kilichopo kina source unamaanisha Mungu hayupo, kwa sababu unayemuita Mungu naye atakuwa na source na akiwa na source si Mungu tena?

Unaelewa hoja yako inaonesha Mungu hawezi kuwepo?
 
Back
Top Bottom