- Thread starter
- #41
MkuuUmesema si mtaalamu, chukua somo la bure leo. Hata hydrogen inaweza kupatikana kama kimiminika, si gesi tu.
Mwalimu anaweka chaguzi kwa sababu hana uwezo wa kuingia kichwani kwako na kukupima unajua nini na hujui nini.
Mungu anayejua kila kitu na kuweza kila kitu anaweka uchaguzi ili iweje?
Kwa nini asingeweka mazuri matupu mabaya yasiwepo?
Angefanya hivyo angepungukiwa nini?
Nashukuru kwa somo, japokuwa naona umerudia tu nilichoandika kwenye post namba #36 kwa maneno tofauti.
Sasa umeanza kuuliza maswali yenye maana, na tunaweza kufikia hitimisho vizuri. Tunapouliza maswali ya 'Kwa Nini' Mungu amefanya hivi ama vile na si hivi ama vile, tunajaribu kujua Nia ya Mungu. Na kama tukiweza kujua kwa ufasaha (kwa kutumia akili zetu wenyewe), tutakuwa tunajua sawa na Mungu ( Ujuzi wote) kitu ambacho haiyamkiniki kikawa.
Inaonesha mkuu Kiranga ungependa sana Mungu angeumba ulimwengu ambao kuna mema tu, hakuna mabaya. Nafikiri kwako, kuumba ulimwengu wa namna hiyo ni kuthibitisha kwamba Mungu anaweza yote. Lakini habari njema kwako na kwa wengine ni kwamba ulimwengu huo ulikwisha kuumbwa na Mungu zamani kabisa, na hata ukitaka kwenda huko inawezekana.
Ulimwengu huu tuliopo umeumbwa kwa namna ambayo mema na mabaya yanaweza kutokea. Kuna ulimwengu unaoitwa Mbingu, huo ni mahali ambapo mema tu yanaweza kuwepo, mabaya yote hayako/hayatakuwepo huko. Kuna ulimwengu unaoitwa Kuzimu/Jehanamu, huko kuna mabaya tu, mema hayatakuwepo huko. Tumepewa uhuru wa kuchagua tutapenda kwenda kwenye ulimwengu upi kati ya hizo.