Wakuu!
Nimeanzisha uzi huu kujaribu kutoa utetezi kinyume na hoja inayopinga uwepo wa Mungu kwa hoja kwamba ulimwengu huu unathibitisha kwamba 'Mungu mwenye upendo wote, uwezo wote na ujuzi wote' hayupo. Kwa wasiofahamu sana hoja hii ni maarufu pengine kuliko hoja zote zinazopinga uwepo wa Mungu, hivi kwamba imekuwa ikikimbiliwa na wengi wasioamini uwepo wa Mungu kama hoja yao ya msingi.
Kwa utambulisho mfupi mimi ninaamini kwamba Mungu yupo, na kwamba pia ninaamini Ukristo ndiyo dini ya kweli pekee. Haya nimeyatamka ili iwe rahisi kuelewa mtazamo wangu kuhusu hili swala, lakini nisingependa iwe msingi wa mjadala, natamani tujadili kulingana na kichwa cha uzi huu.
Ninataka kukiri kwamba ikiwa tunaoamini uwepo wa Mungu tutalazimishwa kuelezea mambo yote yanayotokea katika ulimwengu huu kwa kutumia sifa tatu tu za Mungu (Upendo, Uwezo na Ujuzi) tutababaika kujibu; tutaweza kutoa majibu kwa baadhi ya mambo, lakini si yote. Yamkini hili limejionesha mara kadhaa watu wanapoulizwa hilo swali.
Lakini hoja yangu ni kuwa tatizo liko kwenye swali lenyewe na si kwa wanaojibu. Ikiwa tutataka kujiburudisha tu kwa mdahalo, tunaweza kuweka swali la Mungu mwenye sifa tatu tu lielezee ulimwengu halisi tunaoishi. Lakini ikiwa tutataka kudadisi kwa undani uwepo wa Mungu aliyeuumba na anayeuongoza ulimwengu huu, lazima tutumie mjumuisho wa sifa zake zote (Mungu halisi) kuelezea mjumuisho wa mambo yote ya ulimwengu huu (ulimwengu halisi)
Mungu halisi ana sifa nyingi mbalimbali, na hizi zote zinahusika wakati wowote anapojihusisha na ulimwengu. Baadhi ni hizi Upendo, Uwezo, Ujuzi, Wema, Utakatifu, Utukufu, Hekima, Wivu, Haki, Mamlaka, Uamuzi Binafsi, Uwepo mahali pote, Maarifa na kadhalika.
Mfano: Tukitaka kujiuliza kwa nini Mungu ameumba jua na kuliweka umbali huo alioliweka, na kulazimisha kutumia sifa tatu tu za Mungu kuelezea, hatutapata jibu (la kuridhisha). Lakini tukiruhusu sifa zaidi, ile kujua kuwa ana 'Hekima na Maarifa' vitatupa jibu.
Jambo hili tunapaswa kulitumia tunapoelezea mambo mengine ya ulimwengu huu kama vile kwa nini kuna magonjwa, maafa na kadhalika ilhali Mungu ni mwenye upendo, uwezo na ujuzi wote. Ni kwa sababu hekima, haki, Uamuzi binafsi na kadhalika vinahusika pia.
Nimeanzisha uzi huu kujaribu kutoa utetezi kinyume na hoja inayopinga uwepo wa Mungu kwa hoja kwamba ulimwengu huu unathibitisha kwamba 'Mungu mwenye upendo wote, uwezo wote na ujuzi wote' hayupo. Kwa wasiofahamu sana hoja hii ni maarufu pengine kuliko hoja zote zinazopinga uwepo wa Mungu, hivi kwamba imekuwa ikikimbiliwa na wengi wasioamini uwepo wa Mungu kama hoja yao ya msingi.
Kwa utambulisho mfupi mimi ninaamini kwamba Mungu yupo, na kwamba pia ninaamini Ukristo ndiyo dini ya kweli pekee. Haya nimeyatamka ili iwe rahisi kuelewa mtazamo wangu kuhusu hili swala, lakini nisingependa iwe msingi wa mjadala, natamani tujadili kulingana na kichwa cha uzi huu.
Ninataka kukiri kwamba ikiwa tunaoamini uwepo wa Mungu tutalazimishwa kuelezea mambo yote yanayotokea katika ulimwengu huu kwa kutumia sifa tatu tu za Mungu (Upendo, Uwezo na Ujuzi) tutababaika kujibu; tutaweza kutoa majibu kwa baadhi ya mambo, lakini si yote. Yamkini hili limejionesha mara kadhaa watu wanapoulizwa hilo swali.
Lakini hoja yangu ni kuwa tatizo liko kwenye swali lenyewe na si kwa wanaojibu. Ikiwa tutataka kujiburudisha tu kwa mdahalo, tunaweza kuweka swali la Mungu mwenye sifa tatu tu lielezee ulimwengu halisi tunaoishi. Lakini ikiwa tutataka kudadisi kwa undani uwepo wa Mungu aliyeuumba na anayeuongoza ulimwengu huu, lazima tutumie mjumuisho wa sifa zake zote (Mungu halisi) kuelezea mjumuisho wa mambo yote ya ulimwengu huu (ulimwengu halisi)
Mungu halisi ana sifa nyingi mbalimbali, na hizi zote zinahusika wakati wowote anapojihusisha na ulimwengu. Baadhi ni hizi Upendo, Uwezo, Ujuzi, Wema, Utakatifu, Utukufu, Hekima, Wivu, Haki, Mamlaka, Uamuzi Binafsi, Uwepo mahali pote, Maarifa na kadhalika.
Mfano: Tukitaka kujiuliza kwa nini Mungu ameumba jua na kuliweka umbali huo alioliweka, na kulazimisha kutumia sifa tatu tu za Mungu kuelezea, hatutapata jibu (la kuridhisha). Lakini tukiruhusu sifa zaidi, ile kujua kuwa ana 'Hekima na Maarifa' vitatupa jibu.
Jambo hili tunapaswa kulitumia tunapoelezea mambo mengine ya ulimwengu huu kama vile kwa nini kuna magonjwa, maafa na kadhalika ilhali Mungu ni mwenye upendo, uwezo na ujuzi wote. Ni kwa sababu hekima, haki, Uamuzi binafsi na kadhalika vinahusika pia.