Mungu hakupi unachotaka

Mkuu kwa mtazamo HALISI Mungu mnaye mtaja kutoka kwenye vitabu vyenu ni JITU MOJA KATILI SANA

Anawezaje kuruhusu mtoto mchanga asiye jua lolote azaliwe na saratani mbaya kabisa itakayo mtesa maisha yake yote na akaacha wahalifu wakubwa wanao “mkufuru” wanakula bata kama wapo “peponi”?

Hakuna Mungu mwenye sifa mnasema anazo anaweza kuwa na njia za kikatili namna hii wakati uwezo anao
Unapewa unacho stahili
 
Huyo Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Hakuna Mungu anayetoa chochote kwa binadamu.

Mungu ni fiction character.

Hayupo katika uhalisia ila katika mawazo ya kufikirika tu, Imaginations just an illusion.
Sijui umeshiba maharage ya wapi!
 
Nakwambia hivi huyo Mungu hayupo.

Anashindwa kuwapa hata hayo maharage watoto wadogo wanaokufa kwa njaa maeneo mbalimbali duniani halafu aje anishibishe mimi?
Ndo shida ya sisi wanadamu matokeo mabaya ya matendo yetu tunatafuta pakutupia lawama ulitaka chakula kishuke kutoka mbinguni hizo akili na utashi uliopewa nizakazi gani sasa
 
Hakuna mtu alie pangiwa chochote kwenye maisha , maumuzi yako na mipango yako bahati , na mazingira ndio yataamua hali yako ya maisha
 
Ndo shida ya sisi wanadamu matokeo mabaya ya matendo yetu tunatafuta pakutupia lawama ulitaka chakula kishuke kutoka mbinguni hizo akili na utashi uliopewa nizakazi gani sasa
Kwanza hiyo mbingu haipo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Nakwambia hivi 👇

Sijapewa akili na huyo Mungu.

Huyo Mungu anaye toa akili hayupo.
 
maisha ya mwanadamu ni kama maua huchanua na kusinyaa, wengi wetu tumezaliwa tukiwa na ndoto kibao za mafanikio katika maisha yetu , hakuna mtu asiye penda kuishi maisha mazuri, kila mtu anatamani awe na pesa, jumba, magari na miradi mbalimbali ya kutosha

Nadhani wengi wetu tulipo kuwa bado wadogo katika nyoyo zetu na nyuso zetu tulikuwa tumejenga picha ya maisha yetu ya badae kwamba tutakuwa na maisha mazuri tumejenga nyumba nzuri,tumenunua gari kali la bei mbaya alafu pembeni una mwanamke mzuri. Lakini vyote sivyo bado hatujafanikiwa na tunaendelea kusota na maisha

Siku zote Mungu huwa HAKUPI UNACHOTAKA na anakupa usichotaka ni watu wachache sana ambao wapo kwenye mpango wa Mungu na wakamuomba mahitaji yao wanayo yataka na wakapewa, wengi wetu ndoto zetu nyingi zimeishia njiani kwa sababu tumesha kata tamaa ya maisha.

Sababu maisha ni bahati, maisha ni nasibu mafanikio ya mtu huwa yanakuja automatiki na kila mwanadamu huwa ana road map ya maisha yake yaani mungu anakuwa amesha kuchorea kila kitu kuhusu maisha yako hata ufanye vipi utumie mbinu gani lakini Mungu akipanga amepanga kwamba huyu mtu maisha yake yatakuwa hivi

Embu fikiria una ndoto ya kuwa daktari ila unaishia kuwa mwalimu,
Unataka kuwa injinia unaishia kuwa polisi
Unataka kuwa mwanasheria unaishia kuwa bodaboda
Unataka kumuoa mwanamke fulani ila unaishia kuoa mwingine usiye mdhania
Unapanga nikifungua biashara fulani basi mambo yangu yatanyooka yatakuwa mazuri ila baada ya kufungua mambo yanaenda ndivyo sivyo unaishia kwenye limbi la mawazo kibao.

Lakini haya yote ndio maisha yetu sisi maskini, kwa maana maskini ni wengi kuliko matajiri na wenye mafanikio ni wachache sana tulio wengi ni maskini .

Na baada ya mahangaiko yetu yote duniani lakini mwisho tunaishia kaburini

Ndugu zangu tumtafute sana Mungu kwa bidii ili kila tunacho kitaka tuweze kukipata kwa muda na wakati sahihi

Lakini pia usisahau kuwa sio kila mtu anayepitia nyakati ngumu za kuwa na maisha magumu eti kwamba baadae atapata mafanikio baadae pia unaweza hata ukafa.
Kama Mungu hakupi unachotaka, huo ni uchoyo.

Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo wote hawezi kuwa mchoyo kiasi cha kushindwa kuwapa watu wanachokitaka.

That is a contradiction.

Mungu huyo hayupo katika uhalisia.
 
umeandika vitu kishabiki bila ya kuwa na facts na data

Mungu hana ubaguzi, huwapa mvua wema na wabaya

Bwana wetu Yesu Kristu alisema kabisa kwamba wenye afya hawaitaji tabibu bali wagonjwa na hakuja kwaajili ya wema bali waovu ili wapate kutubu (Kasome injili ya Mtakatifu LUKA 5:31-32)


Inapaswa ujue kwamba siyo vyema kujistahilisha neema za Mungu kwa kudhani kwamba kitendo fulani cha kiiimani kina kustahilisha zaidi kuliko watu wengine. Kwa maana, Mungu wetu anatujua kabla ya sisi kuzaliwa na walio wake anawajua pia.


Bwana wetu Yesu Kristu alisema hivi: (Kasome Mtakatifu LUKA 14:8-11)

8.Mtu akiku alika harusini, usikae kwenye kiti cha mgeni wa heshima. Inaweze kana kuwa amealika mheshimiwa akuzidiye, 9 na yule aliyewaalika ninyi wawili akaja kukuambia, ‘Tafadhali mpishe huyu bwana.’ Ndipo kwa aibu utalazimika kwenda kukaa katika kiti cha nyuma kabisa. 10. Badala yake, unapoalikwa, chagua kiti cha nyuma; na mwenyeji wako akikuona atakuja akuambie, ‘Rafiki yangu, njoo kwe nye nafasi ya mbele zaidi.’ Kwa jinsi hii utakuwa umepewa heshima mbele ya wageni wote. 11 Kwa maana kila mtu anayejitukuza atash ushwa naye ajishushaye atatukuzwa.


Pia nenda kasome Mathayo Mtakatifu 7:21

Kwamba siyo wote wasemao bwana bwana watauona ufalme wa mbingu bali wale tu wanaotimiza matakwa ya baba yake aliye mbinguni


Mwisho kabisa nakupiga na kitu kizito kabisa ili uache kujistahilisha uokovu

Yohana 10:14

Mimi ni Mchungaji Mwema: ninawafahamu kondoo wangu nao wananifahamu

Swali je Yesu anakufahamu?
Uhalali wa kutumia biblia unaletwa na nini? Yaani unapomwambia mtu soma kifungu flani ina akisi katika mambo yote?
 
Kwanza lazima uelewe kuna kitu kinaitwa fate (something which is destined to happen to you) yaani majaaliwa na kila mtu ana fate yake hapa duniani.

Sasa swali kwanini imekaa hivyo, majibu yake ni from the theological perspective kwamba Mungu alipo umba dunia akaona kila kitu kinafaa na ni chakupendeza kwa lugha laini kazi ya Mungu haina makosa.

Sasa basi, vitu vinavyozungumzwa hapa ni vile ambavyo wewe una viomba, na wengi wetu tunaomba vitu ambavyo pengine tunao wajibu wakuvitafuta kama vile mali, mke, usalama, amani, upendo na ata afya njema.

Sina nia ya kukufuru au kulaumu, matatizo mengi ya watoto wetu pengine yangeweza kuepukika kama tungezingatia kanunu za afya na kufuata maelekezo ya kitabibu. Magonjwa mengine yanayowapata watoto ni ya kurithi au yanatokana na uzembe wa wazazi katika kutunza na kufuata afya ya uzazi. Nakiri pia kwamba matatizo mengine pia yanatokea bila kuwa sababu yoyote na hakuna anayeweza kulaumiwa mfano organ failures and diseases kama cancers.

Ukiacha matatizo yanotokea kwa kujitakia wenyewe kama vile urahibu wa madawa ya kulevya, ngono na ajali kama za bodaboda na nyingine nyingi ambazo zinasababisha madhara makubwa, bado sehemu kubwa ya maisha yetu sisi wanadamu ni majaaliwa ya Mwenye -Enzi Mungu.

Bado naendelea kukusihi, tuendelee kumshukuru Mungu kwakua matendo yake ni makuu na ya ajabu
Nimependa namna ulivyotoa ufafanuzi wa kisayansi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom