Mungu anafaidika/anafurahia nini vitu hivi kutoka kwa binadam?

Mukulu wa Bakulu

JF-Expert Member
Aug 12, 2014
4,052
12,906
Miaka ile bado nasali/naamini uwepo wa personal God au Mungu anaehusika moja kwa moja na maisha ya binadam nilikua najiuliza baadhi ya maswali ila sikuwahi kupata majibu yake. Kwa kua imani inakufundisha kuamini kila kitu bila kuhoji ikanibidi niwe nakubali tu au naamini tu.

Baada ya kuachana na mambo ya kuamini uwepo wa mungu anaehusika na maisha ya binadam moja kwa moja, bado nimekua najiuliza, Mungu anafaidika nini na vitu vifuatavyo toka kwa binadam.

1. Kuomba. Mungu anafaidika nini na watu kumuomba wakati anajua maisha yao na anajua shida zao. Hii ni sawa na mzazi kujua kabisa mwanao hajala siku mbili na ana njaa na chakula unacho ila tu unangoja uombwe, je huu ni uwajibikaji au uzembe?

2. Kufunga. Mungu anafaidika nini na kuona watu wanashinda njaa au kushinda bila kula. Furaha yake ni nini watu wasipokula?

3. Sadaka/Zaka. Mungu ambae anadai yeye ni tajiri bado anataka pesa za watu eti wamtolee, mungu anafurahia nini kuomba watu hela zao tena watu choka mbaya lakini bado anakomaa umpelekee hela, ili iweje?

Mnaweza kunisaidia mungu anafurahia au anafaidika na nini na hivi vitu?
 
Acha kuamini vitu vya kipumbavu mkuu!
Elewa kwamba walioanzisha maswala ya uwepo wa Mungu ni wanasiasa.
Haiwezekani kuwepo na Mungu muumbaji wa vyote, muweza wa yote, mwenye upendo, mjuzi wa yote alafu kuwepo na mapungufu mengi namna hii ambayo sisi wanadamu tunapambana usiku na mchana kuyapunguza.

Hakuna cha Mungu wala mamaake na Mungu.
Pambana ukijua kuna kupata na kukosa, kuanguka na kusimama, shida na raha, masikini na matajiri, kuzaliwa na kufa.

Kuamini kuna Mungu ni sawa na kuweka akili yako rehani/bond
 
Acha kuamini vitu vya kipumbavu mkuu!
Elewa kwamba walioanzisha maswala ya uwepo wa Mungu ni wanasiasa.
Haiwezekani kuwepo na Mungu muumbaji wa vyote, muweza wa yote, mwenye upendo, mjuzi wa yote alafu kuwepo na mapungufu mengi namna hii ambayo sisi wanadamu tunapambana usiku na mchana kuyapunguza.

Hakuna cha Mungu wala mamaake na Mungu.
Pambana ukijua kuna kupata na kukosa, kuanguka na kusimama, shida na raha, masikini na matajiri, kuzaliwa na kufa.

Kuamini kuna Mungu ni sawa na kuweka akili yako rehani/bond
Yaaani Hawa Jamaa wamewageuza binaadamu wenzao "" wajinga ndio waliwao
 
Miaka ile bado nasali/naamini uwepo wa personal God au Mungu anaehusika moja kwa moja na maisha ya binadam nilikua najiuliza baadhi ya maswali ila sikuwahi kupata majibu yake. Kwa kua imani inakufundisha kuamini kila kitu bila kuhoji ikanibidi niwe nakubali tu au naamini tu.

Baada ya kuachana na mambo ya kuamini uwepo wa mungu anaehusika na maisha ya binadam moja kwa moja, bado nimekua najiuliza, Mungu anafaidika nini na vitu vifuatavyo toka kwa binadam.

1. Kuomba. Mungu anafaidika nini na watu kumuomba wakati anajua maisha yao na anajua shida zao. Hii ni sawa na mzazi kujua kabisa mwanao hajala siku mbili na ana njaa na chakula unacho ila tu unangoja uombwe, je huu ni uwajibikaji au uzembe?

2. Kufunga. Mungu anafaidika nini na kuona watu wanashinda njaa au kushinda bila kula. Furaha yake ni nini watu wasipokula?

3. Sadaka/Zaka. Mungu ambae anadai yeye ni tajiri bado anataka pesa za watu eti wamtolee, mungu anafurahia nini kuomba watu hela zao tena watu choka mbaya lakini bado anakomaa umpelekee hela, ili iweje?

Mnaweza kunisaidia mungu anafurahia au anafaidika na nini na hivi vitu?
Isaya : Mlango 40

28 Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, BWANA, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki.
 
Ukiona upo kitandani hoi unajinyea hapo hapo uje tena uulize haya maswali yako.
Hivi hujui kuwa hata akina baba parocko, mashehe, mapadri, wachungaji wa kondoo na waumini wao wanaumwa hadi kufa?

Endelea kuabudu uoga na hofu zako ambazo msingi wazo ni maandishi uliyoletewa na wazungu na waarabu.
 
Back
Top Bottom