HOMOSAPIEN
JF-Expert Member
- Mar 31, 2011
- 745
- 271
Nauliza hivi huu uonevu tunaofanyiwa watanzania utaisha lini?.Hali ngumu ya maisha,bidhaa juu,bado na kodi tena imepanda!bidhaa muhimu zinaonekana ni anasa,mshahara ndiyo hivyo kwa wastani kima cha chini ni kidogo sana.
Hivi mungu haoni huu uonevu,mbona anawasaidia wengi hata waisraeli kule misri aliwatoa utumwani na kuwapeleka katika nchi ya ahadi.Je sisi watanzania hatuko katika mpango wa mungu?mbona wengine wanafanya maombi yanakubaliwa?vipi viongozi wetu wa dini wanashindwa kuomba maombi ya kweli kujinasua na haya matatizo?badala yake wanatishiwa eti waheshimu sheria au wale walioko madarakani!.siasa za hovyo hovyo kila anayepata nafasi anakula tu tena bila kupangusa mdomo.
Imefikia wakati sasa wanaweka wanawe marafiki katika nyazifa kubwa kama vile mungu haoni,kama kweli mungu anaona basi tunaomba atende miujiza yake hata leo niko tayari kufunga nac kuomba isifike 2015.
Nakumbuka rais wa iliyokuwa inaitwa Romania au Yugoslavia jina Chesescu aliuwawa na wananchi wake baada ya wananchi kuchoka na manyanyaso na maisha magumu wakati viongozi wao wanaishi maisha ya kutumbua wakiwadanganya wananchi wao hii ikasababisha mpaka nchi yenyewe ikasambaratika.
Angalia hapo Misri wananchi wanaandamana wanataka Mubarak ahukumiwe kifo badala ya maisha.
Viongozi wetu hawajifunzi haya wakafanya marekebisho kidogo au ni mpaka yatokee?.
Tunaomba yasitokee kwetu tuendelee kuwa wamoja ila yanayojiri sasa yanaweza kutufikisha huko tulikozungumzia hapo juu.
Karibu watanzania wataamka katika lidi la usingizi wa kusema hewalahewala kila jambo hata liwe baya.
Hivi mungu haoni huu uonevu,mbona anawasaidia wengi hata waisraeli kule misri aliwatoa utumwani na kuwapeleka katika nchi ya ahadi.Je sisi watanzania hatuko katika mpango wa mungu?mbona wengine wanafanya maombi yanakubaliwa?vipi viongozi wetu wa dini wanashindwa kuomba maombi ya kweli kujinasua na haya matatizo?badala yake wanatishiwa eti waheshimu sheria au wale walioko madarakani!.siasa za hovyo hovyo kila anayepata nafasi anakula tu tena bila kupangusa mdomo.
Imefikia wakati sasa wanaweka wanawe marafiki katika nyazifa kubwa kama vile mungu haoni,kama kweli mungu anaona basi tunaomba atende miujiza yake hata leo niko tayari kufunga nac kuomba isifike 2015.
Nakumbuka rais wa iliyokuwa inaitwa Romania au Yugoslavia jina Chesescu aliuwawa na wananchi wake baada ya wananchi kuchoka na manyanyaso na maisha magumu wakati viongozi wao wanaishi maisha ya kutumbua wakiwadanganya wananchi wao hii ikasababisha mpaka nchi yenyewe ikasambaratika.
Angalia hapo Misri wananchi wanaandamana wanataka Mubarak ahukumiwe kifo badala ya maisha.
Viongozi wetu hawajifunzi haya wakafanya marekebisho kidogo au ni mpaka yatokee?.
Tunaomba yasitokee kwetu tuendelee kuwa wamoja ila yanayojiri sasa yanaweza kutufikisha huko tulikozungumzia hapo juu.
Karibu watanzania wataamka katika lidi la usingizi wa kusema hewalahewala kila jambo hata liwe baya.