Msaada utakaothaminiwa na waTanzania

Msaada utakaothaminiwa na waTanzania

Kalamu

Platinum Member
Joined
Nov 26, 2006
Posts
21,836
Reaction score
30,912
Ni jambo linalotia matumaini kwamba hali duni inayolikabili taifa la Tanzania hatimaye imewagusa hata watu wa mataifa ya nje; si Ulaya Magharibi au Marekani pekee bali hata katika nchi za kiafrika na baadhi ya majirani zetu; hata kama baadhi yao hawsemi chochote hadharani kwa sababu zinazojulikana.

Kwa yale mataifa ambayo tayari wametoa misimamo yao kuhusu hali ya kisiasa hapa nchini kwetu, wengi wameonyesha kusikitishwa na hali ya ukandamizaji unaofanywa na watawala ambao wameshika madaraka bila ridhaa ya wananchi na hadi kutumia silaha kuua wananchi wao.

Juhudi za hadaa zinazotumika ili kuwasafisha hawa watawala, kazi hiyo inazidi kuwa ngumu kwao.
Juhudi hizo ni pamoja na kuwaajili kampuni maalum za kuwatetea katika baadhi ya nchi wafadhili. kama Marekani na Ulaya.
Kwa mfano, kampuni ya kimarekani (lobbyst) iliyopewa kazi ya kushawishi wawakilishi wa maseneta wa Marekani, kampuni ambayo walikubaliana malipo ya dola 45,000 kila mwezi kwa miezi sita.

Kutokana na taarifa za hivi karibuni toka huko Marekani, ni wazi kuwa kazi ya 'lobbyists' hao haikuzaa matunda bora yaliyotegemewa kama inavyoelezwa na mswada unaotengenezwa na maseneta wawili ili uwasilishwe kwenye seneti ya nchi hiyo..

Katika baadhi ya maprendekezo ya mswada huo ni kuwataja viongozi wote wanaojulikana kuhusika na mauaji/utekaji na mambo ya ukandamizaji kwa waTanzania; na hatimaye kuweka vikwazo vya kiuchumi.

Pamoja na kuwa na shukrani kwa nia hiyo nzuri ya kuwabana viongozi waovu; njia hiyo si suluhisho lenye msaada wa haraka kwa waTanzania wanaotafuta kujinasua toka kwenye hii hali mbovu haraka iwezekanavyo.
Vikwazo vya kiuchumi huchukua muda, na mara nyingi wanaoumizwa ni wananchi wenyewe; huku watawala waovu hao wakiendelea na uovu wao.

Msaada unaohitajika kwa waTanzania ni kuwawezesha wafanye wenyewe kazi hii muhimu ya kujiondoa kwenye manyanyaso ya hawa watawala.
Kwa kuwa uwepo wao madarakani unategemea ukandamizaji na mitutu ya bunduki kuua wote wanaojaribu kukataa kunyanyaswa, msaada mzuri zaidi na wa thamani kubwa ni kuhakikisjha kuwa hawaruhusiwi kuitumia mitutu ya bunduki tena bila ya wao kudhurika.

WaTanzania wakipewa msaada huo, kazi ya kurekebisha nchi yetu itakuwa rahisi kwetu wenyewe na njia za kuwawajibisha hawa waovu zitapatikana kwa haki, bila ya uonevu kwa yeyote.

Kwa hiyo, ombi kuu la waTanzania kwa mataifa yanayotaka kusaidia juhudi zetu, ni kuwanyima fursa ya kutumia bunduki wakati waTanzania wakitafuta njia za kurekebisha uongozi wa taifa lao.
 
Gentleman,
misimamo ya mataifa ya magharibi au Marekani dhidi ya taifa huru la Tanzania, kamwe haiwezi kudhoofisha wala kuathiri hata kidogo, jitihada kubwa na za makusudi zinazofanywa na serikali sikivu ya CCM chini ya Dr Samia Suluhu Hassan kipenzi cha waTanzania wote na kiongozi shupavu sana barani Africa, katika katika kuwatumikia wananchi na kuwaletea waTanzania wote maendeleo endelevu ya kiuchumi, kisiasa na na kijamii.

Mabadiliko tajika nchini, yataendelea kufanyiwa kazi kadiri itakavyonekana inafaa, ili kuendana na mabadiliko ya siasa na diplomasia ya ulimwengu mzima inavyokwenda.

hakuna haja ya porojo kwenye mambo haya.🐒

Mungu Ibariki Tanzania
 
Gentleman,
misimamo ya mataifa ya magharibi au Marekani dhidi ya taifa huru la Tanzania, kamwe haiwezi kudhoofisha wala kuathiri hata kidogo, jitihada kubwa na za makusudi zinazofanywa na serikali sikivu ya CCM chini ya Dr Samia Suluhu Hassan kipenzi cha waTanzania wote na kiongozi shupavu sana barani Africa, katika katika kuwatumikia wananchi na kuwaletea waTanzania wote maendeleo endelevu ya kiuchumi, kisiasa na na kijamii.

Mabadiliko tajika nchini, yataendelea kufanyiwa kazi kadiri itakavyonekana inafaa, ili kuendana na mabadiliko ya siasa na diplomasia ya ulimwengu mzima inavyokwenda.

hakuna haja ya porojo kwenye mambo haya.🐒

Mungu Ibariki Tanzania
Mzoga wa nguruwe unaooza sina muda wa kupoteza nao.
 
eleza tu wadau kwamba uko pointless na itapendeza zaidi,

huna haja ya visingizio useless 🐒
Wewe ni mzoga tena ulio karibu sana na Samia. Bila shaka uvundo wa mzoga ndio unaomzonga sana siku hizi za karibuni, maana hata zungumza yake imebadilika kabisa.
Na kichwani ndiyo kawa mtupu zaidi.

Halafu anategemea msaada toka kwa mzoga kama wewe?
Kila siku kunakucha unakimbilia JF kuweka mvundo kwenye kila mdda; hiyo itasaidia kitu gani?
 
Wewe ni mzoga tena ulio karibu sana na Samia. Bila shaka uvundo wa mzoga ndio unaomzonga sana siku hizi za karibuni, maana hata zungumza yake imebadilika kabisa.
Na kichwani ndiyo kawa mtupu zaidi.

Halafu anategemea msaada toka kwa mzoga kama wewe?
Kila siku kunakucha unakimbilia JF kuweka mvundo kwenye kila mdda; hiyo itasaidia kitu gani?
kukosa agenda au hoja ni umaskini mbaya sana na wafedheha kwa wafuata mkumbo 🤣
 
Serikali dhalimu iliyojaa damu, ni wazi kila taifa duniani linajua hii serikali haramu siyo chaguo la wananchi
 
Ni jambo linalotia matumaini kwamba hali duni inayolikabili taifa la Tanzania hatimaye imewagusa hata watu wa mataifa ya nje; si Ulaya Magharibi au Marekani pekee bali hata katika nchi za kiafrika na baadhi ya majirani zetu; hata kama baadhi yao hawsemi chochote hadharani kwa sababu zinazojulikana.

Kwa yale mataifa ambayo tayari wametoa misimamo yao kuhusu hali ya kisiasa hapa nchini kwetu, wengi wameonyesha kusikitishwa na hali ya ukandamizaji unaofanywa na watawala ambao wameshika madaraka bila ridhaa ya wananchi na hadi kutumia silaha kuua wananchi wao.

Juhudi za hadaa zinazotumika ili kuwasafisha hawa watawala, kazi hiyo inazidi kuwa ngumu kwao.
Juhudi hizo ni pamoja na kuwaajili kampuni maalum za kuwatetea katika baadhi ya nchi wafadhili. kama Marekani na Ulaya.
Kwa mfano, kampuni ya kimarekani (lobbyst) iliyopewa kazi ya kushawishi wawakilishi wa maseneta wa Marekani, kampuni ambayo walikubaliana malipo ya dola 45,000 kila mwezi kwa miezi sita.

Kutokana na taarifa za hivi karibuni toka huko Marekani, ni wazi kuwa kazi ya 'lobbyists' hao haikuzaa matunda bora yaliyotegemewa kama inavyoelezwa na mswada unaotengenezwa na maseneta wawili ili uwasilishwe kwenye seneti ya nchi hiyo..

Katika baadhi ya maprendekezo ya mswada huo ni kuwataja viongozi wote wanaojulikana kuhusika na mauaji/utekaji na mambo ya ukandamizaji kwa waTanzania; na hatimaye kuweka vikwazo vya kiuchumi.

Pamoja na kuwa na shukrani kwa nia hiyo nzuri ya kuwabana viongozi waovu; njia hiyo si suluhisho lenye msaada wa haraka kwa waTanzania wanaotafuta kujinasua toka kwenye hii hali mbovu haraka iwezekanavyo.
Vikwazo vya kiuchumi huchukua muda, na mara nyingi wanaoumizwa ni wananchi wenyewe; huku watawala waovu hao wakiendelea na uovu wao.

Msaada unaohitajika kwa waTanzania ni kuwawezesha wafanye wenyewe kazi hii muhimu ya kujiondoa kwenye manyanyaso ya hawa watawala.
Kwa kuwa uwepo wao madarakani unategemea ukandamizaji na mitutu ya bunduki kuua wote wanaojaribu kukataa kunyanyaswa, msaada mzuri zaidi na wa thamani kubwa ni kuhakikisjha kuwa hawaruhusiwi kuitumia mitutu ya bunduki tena bila ya wao kudhurika.

WaTanzania wakipewa msaada huo, kazi ya kurekebisha nchi yetu itakuwa rahisi kwetu wenyewe na njia za kuwawajibisha hawa waovu zitapatikana kwa haki, bila ya uonevu kwa yeyote.

Kwa hiyo, ombi kuu la waTanzania kwa mataifa yanayotaka kusaidia juhudi zetu, ni kuwanyima fursa ya kutumia bunduki wakati waTanzania wakitafuta njia za kurekebisha uongozi wa taifa lao.
Inawezekana vipi kuwanyima fursa ya kutumia silaha wakati zipo kwenye maghara yao mkuu. Au unataka wananchi nao wapewe silaha?
 
kukosa agenda au hoja ni umaskini mbaya sana na wafedheha kwa wafuata mkumbo 🤣
Kumbuka ulipoanzia kabla hujawa mzoga; unakumbuka?

Sasa jitazame ulivyoporomoka hadi kuwa umeoza namna hii. Kuna wakati ulidiriki kujifanya wewe ndiye Samia!!!

Nyinyi mizoga wote akiwemo na Samia mwenyewe mmeifikisha Tanzania mahali pabaya sana. Uzuri ni kwamba mizoga yote itaondolewa mitaani usafi utakapofanyika.
 
Inawezekana vipi kuwanyima fursa ya kutumia silaha wakati zipo kwenye maghara yao mkuu. Au unataka wananchi nao wapewe silaha?
Mbona watakuwa hawajipendi mkuu; au unadhani wao kufa hakuwahusu.

Hawa waovu sasa hivi haihitaji tena kutumia silaha.
Kule kuwamulika tu ni nani anafanya nini; uwezo ambao hao tunaowaomba wasaidie upande huo inatosha kabisa kuyafunga hayo maghala ya silaha unayoyazungumzia wewe.

Usifikiri kuwa pamoja na uovu walionao kuwa hawana akili tena za kujuwa hatari ikowapi kwao.

Kuna njia nyingi tu. Hebu fikiria wakiweka kimanowari kimoja tu pale langoni kwa wiki moja tu ili tumalize kazi yetu wenyewe; ni nani atakayethubutu kufungua hayo maghala?
 
Back
Top Bottom