Mume wangu mvivu!

Mume wangu mvivu!

magori81

Member
Joined
Oct 11, 2011
Posts
22
Reaction score
11
Habari zenu wana janvi,yamenifika shingoni mwenzenu ndio maana nimeamua kuomba msaada wa mawazo yenu.
Nina umri wa miaka 30 na mume wangu ana miaka 38 tunapendana sana na tumeoana miaka sita iliyopita.tumebahatika kupata watoto 2.Wakati wa uchumba wetu uliodumu kwa miaka 2 mchumba wangu alikuwa very active katika suala la tendo la ndoa.Baada ya kuoana mambo yalibadilika kabisa kwani mume wangu amekuwa hajisikii kabisa kufanya tendo hilo ambapo yaweza pita wiki tatu hata mwezi mzima bila kufanya chochote na akibahatika kufanya basi ni round moja tena isiyozidi hata dakika 3.Nimejaribu kufanya kila niwezalo ikiwa ni pamoja na kuongea naye lakini yeye anadai kuwa yuko sawa ila hapendi tu kufanya mapenzi mara kwa mara kwani mara nyingi anachoka na majukumu ya kazi!Binafsi sioni dalili kama ananisaliti nje ya ndoa,ila nshindwa kupata jibu je hali hii ni kawaida? au pengine Kanichoka?
 
Hiyo hali ni ya muda gani? yaani ameanza kubadirika toka muda gani?
 
la mgambo limelia huku maujuzi yenu yanahitajika ktk hili
copy;Mzizimkavu,Mtambuzi,The Boss,Madame B,Kongosho,nivea na ..................
mumshauri vizuri eeh.
 
Sasa unapotea hutaki kuja kujibia hoja ndo nini? Si unaulizwa hapo juu na wadau ili wakusaidie?
 
Je ulivyokuwa nae kwenye uchumba ulikuwa mwembamba ila kwa sasa umenenepa ovyo? Jibu kwanza hili swala ili nitiririke mafacts.
 
Pole. Kabla hujamhisi na kumhisi, hebu jitafakari wewe mwenyewe, go back to the manuals ...the basics.

Umesema umefanya kila uwezalo, unaweza kusema ni yapi umeshafanya ...ili nasi tujue pa kuanzia?
 
Upunguze kuvaa mavitenge ovyo.....mtege kidogo,vile ulivyokua unafanya wakati wa uchumba,uendelee navyo....na usishangae huyo mumeo akienda game za mchangani anapiga goli nne tena hachoki.....!!!!
 
Hiyo hali ni ya muda gani? yaani ameanza kubadirika toka muda gani?

Hali hii ilianza muda mfupi tu baada ya kufunga ndoa,kwa kweli nimejaribu kila ninaloliweza lakini hali haibadiliki.ninahisi uvumilivu umeanza kupungua ndio maana ninaomba ushauri wa ziada.
 
Pole... Unamtunza Mme wako vizuri na wewe kujitunza kama mwanamke na yeye kukuthamini kama Mke.. Mnaishi kwa Mawazo na kusononeka... Mnashughuli inayowaingizia kipato... Jichunguzeni kama hampo katika hali ya kukata tamaa inayotokana na Majukumu ya familia, kwani mambo haya hukatisha tamaa katika Maisha ya Ndoa.
 
wakati mwingine mwanamke anaweza akawa ndio chanzo cha matatizo.
embu tuchukulie zamani ulikuwa na tabia ambayo mumeo aliipenda sana, pengine ulimpendeza zaidi unapojipigilia manukato mazuri lakini tangu uolewe sasa umejihakikishia kuwa mume unae ndani na hatoenda kwingine so unaanza kupunguza baadhi ya mambo muhimu ambayo mumeo aliyapenda

wakati mwingine mnajisahau na kushindwa kutambua kuwa mapenzi ni utoto baadhi yenu huwa mnafikia hatua ya kuwaona wapenzi wenu kuwa wanafanya mambo ya kitoto mfano; mwenza wako anaweza kukufanyia suprise afu wewe ukampa discourage words ......kama hivi wewe baba nanihiii lini utaacha utoto???? mh kwa maneno kama hayo sizani kama kuna mwanaume atakuwa na hamu tena na tendo la ndoa.
 
Yah.enzi za uchumba nilikuwa mwembamba lakini hii hali ilianza kabla hata sijaanza kugain ingawa hata yeye amegain sana,tulijaribu kuliona hili kama tatizo tukajaribu hata kufanya mazoezi ya viungo na diet pamoja lakini haijabadilisha situation.
 
Upunguze kuvaa mavitenge ovyo.....mtege kidogo,vile ulivyokua unafanya wakati wa uchumba,uendelee navyo....na usishangae huyo mumeo akienda game za mchangani anapiga goli nne tena hachoki.....!!!!

Anavaa suti ya kuzaliwa licha ya vidress vya mitego. Mume mchovu au malaya full stop. Si kosa la mkewe wala nini; bidada, piga magoti kwa Mungu huenda akanrudishia nguvu za kiume kama devil ameikwapua ili kuharibu ndoa yako, hata kama anamwaga nje basi Mungu amuoneshe uovu wake na arudi kundini!
 
Hali hii ilianza muda mfupi tu baada ya kufunga ndoa,kwa kweli nimejaribu kila ninaloliweza lakini hali haibadiliki.ninahisi uvumilivu umeanza kupungua ndio maana ninaomba ushauri wa ziada.
Kwa maana hiyo umeishi na hilo tatizo kwa zaidi ya miaka 5? Hadi sasa umechukua hatua gani katika kumsaidia mwenzio?
 
Back
Top Bottom