Mume na kuhudumia familia

Mume na kuhudumia familia

Wote yapasa wasaidiane ili mwanamke nae apate uzoefu,kuna msemo unasema"USILE SANA, KUNA NJAA"maana yake usiwe tegemezi sana,kuna kufa.
 
Wote yapasa wasaidiane ili mwanamke nae apate uzoefu,kuna msemo unasema"USILE SANA, KUNA NJAA"maana yake usiwe tegemezi sana,kuna kufa.
Kuna article moja ya New York Times la jana inasema ndoa za siku hizi watu wanaoana kwenye level moja, zamani ilikuwa bosi anamuoa sekretari halafu anamuachisha kazi awe mama wa nyumbani.

Siku hizi mkurugenzi anamuoa mkurugenzi.

Haya mambo hata kwetu yanakuja. Sasa ndoa ikishakuwa na power couples, mpango mzima ni kusaidiana kwa urari.

Equality in Marriages Grows, and So Does Class Divide http://nyti.ms/211JXyj
 
zamani wanaume wenye wake zaidi ya mmoja walikuwa wale wenye malinyingi tu kama ng'ombe,n.k kwani angeweza kuwatunza, ila sahivi kila mtu anamudu michepuko na wake kibao maana huwahudumii majumbani wanakulisha why usijisevieeee??

ila hawa wakuchagua kazi kama kwao wanamiliki viwanda, washinda kwa tv akiangalia Barcelona kipato cha mke kinamuumiza akili sana namna atavyokitafuna .
kila mtu aplay role yake anayezidiwa na wajibu wake baada yakujitahidi sana ndipo asaidiwe ndoa zitakuwa na heshima
 
Miaka 16 ina-qualify kweli kwenye ndoa zilizodumu? Sidhani. Kama ni futbol, hata kipindi cha kwanza hakijaisha.

Anyway, as a man, there's only one formula to getting along with us; DO NOT HURT A MAN'S PRIDE. And since we ain't all cut from the same piece of cloth, we don't share the same pride. So some may find theirs in providing, others may not. Just study the brotha.

these m.n of today na kauli mbiu "maisha ni kusaidiana" can't stand alone and do one thing effectively!! they must change
 
Hizi habari za suluhisho copy and paste unaweza kuambiwa niachie mke wako nilale naye ndiyo suluhisho hivi hivi.
Kwa upande wako utamwachia mkeo kufanya baadhi ya majukumu yanayopaswa kufanywa nawe?
 
Mfano kulipa bills,kulisha familia na mahitaji mengineyo hapo home...
Kuna thread humu inasema wanaume wanapungua sasa huyu sijui ni mme / ni Mme mtarajiwa hajui majukumu ya Mme ndani ya nyumba ni yepi!!!!!! Very interesting.
 
Kuna thread humu inasema wanaume wanapungua sasa huyu sijui ni mme / ni Mme mtarajiwa hajui majukumu ya Mme ndani ya nyumba ni yepi!!!!!! Very interesting.
Ha haa anajua ila kaamua tu kunifanyia kusudi....
 
  • Thanks
Reactions: nao
Kuna thread humu inasema wanaume wanapungua sasa huyu sijui ni mme / ni Mme mtarajiwa hajui majukumu ya Mme ndani ya nyumba ni yepi!!!!!! Very interesting.
Wapi nimesema sijui?

Unajua kusoma wewe?
 
Mfano kulipa bills,kulisha familia na mahitaji mengineyo hapo home...
Bills zote zipo automatically paid.

Kulisha familia tatizo language ni kununua vyakula zaidi ya vinavyohitajika, sina tatizo la kukosa kulisha, si familia tu.

Sasa hivi watu tunatafuta usuluhishi wa mambo ya juu kabisaaaa ya Maslow pyramid.

Hayo mambo ya bills sijui na kulisha familia ni habari za ujima.
 
Siwezi kumuegemea Mke hata siku moja.

Kwa upande wangu naona itakuwa najishusha mavyeo.

Ndio mke anajiweza sikatai, ila kuna baadhi ya mambo lazima yawe jukumu langu siwezi mwachia Mke
 
Wanawake wamekuwa shida sana siku hizi. Unakuta mtu yupo hapa JF anaponda kweli role ya mumewe ila kwakwe kainstall mahouse girl wawili wawili na house boy juu. Asilimia zaidi ya 70 ya wanawake wa siku hizi hawajui role yao kama wake lakini wanavyonyoosha midomo hapa kwenye role ya waume wao.
 
Naomba nijitahidi kuyajibu maswal yako kidogo kwa experience yangu. Kabla ya kuenda zaidi, ningeomba niseme kuwa ni mume wa mke mmoja, tupo pamoja bila kuachana hata kwa siku 1 akaenda kwao kwa sasa ni miaka 40+. Tumejaliwa watoto 8, kati ya hao 5 wapo hai. Nimebarikiwa kuwasomesha na wa mwisho yupo Chuo Kikuu. Hivyo wote walifikia huko.

1. Hili swala la wanawake kuingilia majukumu ya waume zao lina mchango kiasi gani katika familia zinazohudumiwa na wake hapa Tanzania ilihali waume zao wana vipato?

2. Kama wanaume hujisikia mashujaa/vizuri kwa kuhudumia familia, na kama hizi ni hisia za asili, hawa wanaume wanaonyang'anywa hizi hisia na wake zao huzifidia vipi?

3. Ni mara nyingi tumeona hapa jf wanandoa wa kiume wakilalamika kuwa wake zao wana vipato lakini hawachangii katika kuhudumia familia. Hili nalo liwekwe vizuri.

1. Kama kweli, mume ana kipato kizuri tu cha kuwezesha, akimruhusu mke wake awe ndiye mlishi wa nyumbani, huyo mwanamume nasema; Anatatizo kuubwa. Aliyetuumba tangu mwanzo alitutaka, Mwanamume atoke jasho ili mkewe ale. Itakuwa ni aibu iso kifani mke wangu anipakulie wali nyama na mchuzi mzito, halafu nikae mezani na watoto wangu tule tujilambe mikono. Najiuliza swali, nitamwambia aksante mama kwa chakula au nitatoka ka hotelini??
Hiyo nyama najua kafanyaje mpaka akainunua?? Nasema; Haikuji... Haiingii akilini. Mtoto asiposema aksante mama kwa chakula, ki kwetu anastahili vibao vya kumtosha. Sasa, miye ntalambwa fimbo au?? Haijiiiii.
2. Ukweli ni kwamba, hata ukifika pale buchani kununua nyama ya kupeleka home, wale wamama waliokaa pale hukuheshimu. Muuza bucha naye hukuita; Mzee nanihii nikate kilo ngapi. Hizo zote hukufanya ujisikie. Sasa, nikifika home, nkakuta nyama choma imeandaliwa kwa week end, nami sikuinunua, ntakulaje? Mama hastahili.
3. Mke kuwa na kipato chake, nitamkalisha chini, na kumsomesha hadi aujue wajibu wake. Kwa kuwa anataka kufanya kazi ofisini kwa sababu ya kisomo chake, sio vibaya. Lakini, akumbuke kuwa siku alipoondoka kwao, akaja kukaa kwangu, hata jina alibadilisha. Huyu ndiye mtoto wangu wa kwanza. Akaitwa binti MIMI yaani Mrs. MIMI. Kama mtoto wangu wa kwanza, jukumu lake ni kunitii, kuniheshimu. Ili jina langu limpendeze, kamshahara kake, akalete mezani tukapangie tufanye maendeleo. Najua wengi mtanipinga, lakini, kumbukeni kuwa kwenye mirathi anataka awe ndiye msimamizi wa mali (zangu) na wakati huo anadai tulichuma naye. Kama mshahara wake anautumbulia porini kusiko julikana, itakuwa ni dhambi kuthubutu kusema ati tulichuma naye. UAMINIFU ndio msingi wa haya yote. Mzee ukiisha ficha kipato na kuanzisha vijumba vijumba huko na huko, na beeer kwa wingi kwenye mabaa, hustahili hata kumuuliza anapata ngapi.
 
Back
Top Bottom