Mume Mwema Anapatikanaje?

Mume Mwema Anapatikanaje?

ladyfurahia

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2011
Posts
14,758
Reaction score
9,589
Habarini bandugu marafiki zangu wote na wasio marafiki pia.

Naingia kwa ujio kama alivyokuja Raisi Obama kimkuku kuku na wakiana kwa leo wapendwa wangu
marafiki zangu ninaingia kiimani zaidi na ni vyema muelewe nilichoamua kukizungumzia hapa na sio
kufakamia bila hata kuelewa topic hii yasemaje: Kabla sijaenda mbele zaidi tazama picha hii hapa:

man in suit.jpg na hii man ni suit2.jpg hapa tena man2.jpg mwisho man 1.jpg


Kila mmoja wetu anajua kua Maandiko matakatifu yanavyosema sana jinsi ya kupata Mke kuliko Mume na maandiko maarufu ni kama-‘’Mithali18:22-‘’Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa Bwana’’ na Mithali.31:10-’’Mke mwema( Kiswahili imetumia neno moja tu .’’Mwema’’ lakini Kiingerea ktk Bible mbalimbali imetumia maneno mengi yenye nguvu ya ajabu na kushangaza kujua kumbe Mwanamke mtarajiwa kuwa Mke ni kitu kizuri na cha ajabu sana hasa aliyetoka kwa Bwana. Maneno yaliyotumika ni kama.’’ wife of noble character’’, ‘’capable’’, ‘’intelligent’’ ‘’virtuous woman’’, ‘a competent wife’’, ‘’worthy woman’’), ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani. Tena Biblia ya King James na New King James ndizo zimetumia neno ‘’Virtuous woman’’ ( notice: Ni woman!) na maana ya neno ‘’Virtuous’’ ni ‘’good’’, ‘’moral’’, ‘’ethical’’, ‘’upright’’, ‘’honourable’’, ‘’excellent’’, ‘’pure’’, ‘’worthy’’, ‘’honest’, ‘’righteous’’, ‘’exemplary’’, ‘’squeaky clean’’, ’’blameless’’, ’’praiseworthy’’, ‘’incorruptible’’, ’’high-principled’’), pia Mwanzo.24:1-67.

Katika Agano Jipya, tunakutana na neno kuchumbia au Mchumba wazi wazi ktk Luka.2:5 ingawa hatuambiwi Joseph (yusufu) alimpataje mdada Mary (Maria mama wa Yesu) Kwakua ni ivyo kwamba Bible imeongelea sana kuchumbia au Mchumba wazi wazi ktk Luka.2:5 ingawa hatuambiwi Joseph alimpataje mdada Mary. Kwakuwa ni ivyo kwamba Bible imeongelea sana kupata Mke mwema ambaye anapatikana tu kwa Bwana, mchumba bora je? anayepelekea mke mwema, tunampataje? kwa kizazi chetu cha leo cha DOT .COM ambapo hatuchanguliwi Wachumba/Wake zetu na wapendwa marafiki zetu, Viongozi wa Kanisa. Maparoko au Wazazi kama zamani, tunafanyaje kuwa salama?

Tutafanyaje kumpata mchumba mwema (mume) kwa kizazi hichi jamani na je kwanini haya maneno hayakuandikwa kwenye Bible? kwani sisi madada tunachanganyikiwa nami pia yameniconfuse mwenzenu kabisa wala sijaelewa, kwani Mume (Mwanaume) mwema hapatikani kwa Bwana? au ni versa vesa tu hapa.ambayo imewekwa, kwani hakuna wanaume wema wa kuolewa nao.? Ndo mana nimependa niwashirikishe jambo hili la kiimani tuchambue kidogo. kwani huwa nikisoma vifungu hivi vinanitatiza sana. Nakuwa sielewi kabisa my frendo. HAKUNA MWANAUME MWEMA TOKA KWA MUNGU?
Karibuni mabestito kwa uchambuzi zaidi hapa.


cc: Nicas Mtei, Ruttashobolwa, Erickb52, Mr. Rocky, Arushaone, Mtambuzi, Mamndenyi, lara 1,
stevoh, jouneGwalu, Kipaji Halisi, Jiwe Linaloishi, Filipo, Liverpool, Passion Lady, charminglady, Paloma, Mentor, Heaven on earth, everln salt, gfsonwin, Lady doctor, Asprin, Madame B, Lucas, @Rular Swaga, Lyagwa, Ben Saanane, mimisa, na marafiki zangu wote jongeeni
 
Last edited by a moderator:
Fanya maombi,tena kama ni yakufunga itakuwa bora halaf uwe na imani hasa kwa yule unayedhani unampenda,Mungu atakujibu ama kwa ndoto,maono na hata uhalisia,kisha muahidi Mungu kwamba "unipe mume wa namna .....ukinipa nitatoa.... "halaf changanya na sadaka.
 
Habarini bandugu marafiki zangu wote na wasio marafiki pia.

Tutafanyaje kumpata mchumba mwema (mume) kwa kizazi hichi jamani na je kwanini haya maneno hayakuandikwa kwenye Bible? kwani sisi madada tunachanganyikiwa nami pia yameniconfuse mwenzenu kabisa wala sijaelewa, kwani Mume (Mwanaume) mwema hapatikani kwa Bwana? au ni versa vesa tu hapa.ambayo imewekwa, kwani hakuna wanaume wema wa kuolewa nao.? Ndo mana nimependa niwashirikishe jambo hili la kiimani tuchambue kidogo. kwani huwa nikisoma vifungu hivi vinanitatiza sana. Nakuwa sielewi kabisa my frendo. HAKUNA MWANAUME MWEMA TOKA KWA MUNGU?
Karibuni mabestito kwa uchambuzi zaidi hapa.
Just to quote few;
ladyfurahia kwa asili ilikua wanaume (mume mwenyewe, baba wa mume au baba wa mke) ndio wakitafuta wake wa kuoa. Kwa sasa labda tuseme wote wake kwa waume wanatafutana! Hakuna shida yeyote katika maandishi, kwa vile hizo tabia haziko "explicit" bado nguvu ya Mungu iko pale pale.. Unatakiwa umuombe Mungu akuonyeshe mume wa kweli mwenye sifa unazozitaka wewe, au Yeye Mungu amlete kwako mwanaume mwenye sifa hizo tu si mwenginewe.. very simple..!!
 
Mi nahisi maandiko yametutenga wanawake mana wanaume tu ndo wameelekezwa kwe2 ila sisi twapataje waume wema haijasema ! Ila kwa akili zangu mi nahisi maandiko yameona jinsi gani wanawake 2livyo MUHIMU sana katika jamii,kanisani,shuleni,nyumbani na kwengineko that y wanaume wameelekezwa kuchagua MKE MWEMA ili asikosee kujenga ama kuendeleza FAMILIA iliyonjema mana mwanaume anapoteleza tuu! Ndo hayo unaskia mara mwanamke kaomba talaka,mara mke haelewani na mama mkwe,mala kafumaniwa full vurugu! All in all mamaa Lady MUME WAKUFANANA NAWE anapatikana kulingana na INTEREST ZAKO,TABIA ZAKO, + MAOMBI YA KUKUTANISHWA NA HUYO MUMEO MTARAJIWA baasi! Ni hayo tu my dia!
 
Mi nahisi maandiko yametutenga wanawake mana wanaume tu ndo wameelekezwa kwe2 ila sisi twapataje waume wema haijasema ! Ila kwa akili zangu mi nahisi maandiko yameona jinsi gani wanawake 2livyo MUHIMU sana katika jamii,kanisani,shuleni,nyumbani na kwengineko that y wanaume wameelekezwa kuchagua MKE MWEMA ili asikosee kujenga ama kuendeleza FAMILIA iliyonjema mana mwanaume anapoteleza tuu! Ndo hayo unaskia mara mwanamke kaomba talaka,mara mke haelewani na mama mkwe,mala kafumaniwa full vurugu! All in all mamaa Lady MUME WAKUFANANA NAWE anapatikana kulingana na INTEREST ZAKO,TABIA ZAKO, + MAOMBI YA KUKUTANISHWA NA HUYO MUMEO MTARAJIWA baasi! Ni hayo tu my dia!
hahahahahahaha...umesahau mungu alimuumba ADAM na 'HAWA' sasa hapo kwenye "hawa"..ndio tunatakiwa....kuwachagua nyie akina hawa maana mko wengi
 
Muombe mungu atakupa mume mwema. Usiaangalie material tu!
 

nimekuelewa my cousin
ukimuomba mungu akupe mume
mwema inakua kama ulivyoomba!!
 
Kwa ujumla vijana wa kike na kiume wana wakati mgumu sana wakati wa kumpata mwenzi wa maisha. Inakua rahisi kwa mwanaume cse yy ndo mfanya maamuzi japo nao wana wakati mgumu cse mapenzi ni. Vise versa : vile unavyo mpenda mwenzako sivyo atakavyo kupenda.

Kikubwa ni kumuomba Mungu tukiamini mume na mke mwema anatoka kwa Lkn tunapaswa kua na subira ktk kusubiri majibu. Usilazimishe tamaa zako kua majibu.
 
Tatuzo lenu mnatumika sna , afu mtataka tuwaowe. Pia mnaleta mapenzi ya kwenye tamthilia sna.

wee Kaka Jambazi utafungwa ujue! 2natumika wap viwandani au? Na watumiaji ni akina nani kama siyo nyie akina Kaka? Je unakipimio cha kumpima aliye2mika? Aaah bana wee! Em zama tena uibuke!
 
Kwa ujumla vijana wa kike na kiume wana wakati mgumu sana wakati wa kumpata mwenzi wa maisha. Inakua rahisi kwa mwanaume cse yy ndo mfanya maamuzi japo nao wana wakati mgumu cse mapenzi ni. Vise versa : vile unavyo mpenda mwenzako sivyo atakavyo kupenda.

Kikubwa ni kumuomba Mungu tukiamini mume na mke mwema anatoka kwa Lkn tunapaswa kua na subira ktk kusubiri majibu. Usilazimishe tamaa zako kua majibu.

yaaap! Upo ryti kabisa bdaye ntakupa like!
 
Back
Top Bottom