Mume kuitwa daddy na daddy aitweje?

Mume kuitwa daddy na daddy aitweje?

shansarie

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2013
Posts
5,690
Reaction score
3,370
Wapendwa nisaidieni hili eti ni sahihi kumuita mpenzi wako au mume wako daddy?
Inamaana gani? angali daddy ni baba yako mzazi au ndo kumkabidhi majukumu ya mzazi wako.
 
Wapendwa nisaidieni hili eti ni sahihi kumuita mpenzi wako au mume wako daddy?
Inamaana gani? angali daddy ni baba yako mzazi au ndo kumkabidhi majukumu ya mzazi wako.

hizo ni tashtiti za mahabati acheni tu tuitwe daddy na isitoshe nimempiga gepu la 20 years khee khee..
 
Nimeshuhudia hilo, ila majibu nilopata yalikuwa kuwazoesha watoto kumwita daddy/mummy, badala ya kumwita mkeo Esther...

watoto nao wanaweza kuita kama mnavoitana.....baadae wakishakuwa wakubwa na nyie mshazoea kuitana daddy/mummy basi mazoea yanabakia ivo.
 
Mda mwingine tunawaita kina dady sbb mnafanya majukumu ya baba zetu! Mnatulea na kutusomesha.
 
Wengine wanafanya hivyo ili watoto wao wazoee kuwaita baba zao daddy coz wanackia vile mama zao wanavyowaita. Usikomae sana na sweetie ukashangaa siku mtoto anamuita baba sweetie. Ama 'we fulani!' then mtoto naye anamuita 'we fulani(jina la mume)'
 
mi binafsi naona ni sawa tu ikiwa hakuna anayekwazika kati yenu kuitwa daddy au mummy ni ishara ya mapenzi ya hali ya juu na kuonyesha unatambua jukumu lake kwa ukubwa upi.
 
mi binafsi naona ni sawa tu ikiwa hakuna anayekwazika kati yenu kuitwa daddy au mummy ni ishara ya mapenzi ya hali ya juu na kuonyesha unatambua jukumu lake kwa ukubwa upi.

Kuna mtu aliniambia eti wanaoitwa daddy ni wale wanaoudumia kila kitu mf kodi ya nyumba lunch saloon mafuta ya gari nk...
Nikashangaa nakuogopa maana kidogo nimwite wangu daddy asije kudhani nataka matumizi lol
 
Back
Top Bottom