Mume kuitwa daddy na daddy aitweje?

Mume kuitwa daddy na daddy aitweje?

haileti mantiki hata kidogo kwangu!

kuna swaga nyingine ni wastage of time and money.
 
Haya ni mazoea kati ya mzazi na mtoto wake, ingawa muda mwingine ni makosa kuiga! mi nilizoeshwa na wadogo zake mama yaani Wajomba zangu kumwita MAMA sister mpka sasa nina 25, Nae mama anaona kawaida tu.
 
Wapendwa nisaidieni hili eti ni sahihi kumuita mpenzi wako au mume wako daddy?
Inamaana gani? angali daddy ni baba yako mzazi au ndo kumkabidhi majukumu ya mzazi wako.


nje ya mapenzi yenu , mwanaume anapaswa kukulinda , kukupenda , kukujali , kukuheshimu , kukusaidia , kukuongoza , kukutunza kiuchumi , jamii ,ikiwezekana na kisiasa............. hapo naona majukumu ya udaddy yameingia , ukichukulia pia huwa tunawazidi umri kwenye mahusiano.
 
siku hizi "helo baba au mamy/mama unasemaje......nyumbani wote neno linalitumika ni baba/mama
 
Back
Top Bottom