Mume kama huyu je ni Mume bora

Kalaudi

Senior Member
Apr 16, 2017
112
100
Mambo vipi

Mume kama huyu anae amka asubuhi kutaarisha watoto na kupika chai kupiga pasi nguo za watoto kuwaandaa kwenda Shule .
Wife kalala

Mume kama huyu je ni Mume bora au wewe kwa mtazamo wako unamuweka katika Group lipi ?
 
Wanawake ndo wanapenda wa hivyo, halafu akienda kusukwa anamuona boya.
 
Zoba na mwanaume halelewi ivo jamani mwanaume kumfanya km houseboy, mume ana heshima yake kumbuka mwanaume aliumbwa kwa mfano wa Mungu na sisi tuliumbwa kwa ubavu wa mwanaume sasa dume kulifanya ivo ukweli ni kumtukana Mungu na utalipia dhambi hiyo
 
Mzee usipanic kila mtu anaishi maisha anayoyataka yeye na familia yake wengine ni siri yao sasa kama wewe maisha yako umeyafafanua hapa tulia sindano zikuingie hakuna aliekutaka uhadithie unavyoishi na mkeo.
poa mkuu sasa ubwege umetoka wapi
 
Ikiwa mwanamke atampata mume kama huyo ajitahidi asimuache, kwani ni katika waume wachache wenye kumudu mambo hayo.
 
poa mkuu sasa ubwege umetoka wapi
Ahahaha kama nilivyosema kuna mtu anaweza kuona kama unakosea ndo yanapokuja majibu ya hivi ila hata yeye mwenyewe kuna vitu mkewe anaweza kuwa anamfanyisha akivisema hapa wewe mwenyewe utaweza kumwita hivyohivyo bwege so tuvumiliane tu kaka.
 
Zoba na mwanaume halelewi ivo jamani mwanaume kumfanya km houseboy, mume ana heshima yake kumbuka mwanaume aliumbwa kwa mfano wa Mungu na sisi tuliumbwa kwa ubavu wa mwanaume sasa dume kulifanya ivo ukweli ni kumtukana Mungu na utalipia dhambi hiyo
Umenikosha kweli kweli sijajua kwa nn mm nisingekuoa ww malkia wa nguvu nilichelewa wapi mm jaman
 
Back
Top Bottom