Mume Akupende!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,144
[h=3]Mume Akupende![/h]

[h=3]Mume Akupende![/h]

Haijalishi ni kazi gani mume anafanya anastahili kupewa appreciation!
Wanaume wakikutana wenyewe kwa wenyewe kama hawafahamiani swali la kwanza kuulizana ni “unafanya kazi gani
Sababu ya msingi ni kwamba wanaume wengi suala la kazi ni kitambulisho (identity)
Ndivyo walivyoumbwa na Mungu na hiki ni kitu wanachozaliwa nacho kujikuta ni mtu wa kwenda kuwinda, kulima, kufanya kazi kwa ajili ya familia yake.
Kufanya kazi ni jambo la msingi kwake.
Akipata ugonjwa anaweza kupigana na kuhimili kila aina ya msongo wa mawazo au mgandamizo wa damu hata hivyo linapokuja suala la kazi kwake huwa maumivu ni makubwa kiasi cha kuwa na stress au depression.
Mwanaume anaweza kusimama imara hata katika ugonjwa unaoleta mauti kama cancer lakini si suala la kupoteza kazi au business.
Mwanaume mmoja baada ya kufanya deal la uhakika kwa kutengeneza Mamilioni ya pesa, kwa furaha akaenda nyumbani kwa mke wake kumwambia hizo habari njema na mke wake akamjibu kwa mkato “sawa nimekusikia” then akaendelea na kazi zake pale nyumbani.
Mume alikatishwa tamaa na kuvunjwa moyo kiasi cha kutoa maamuzi kwamba kuanzia hapo hatamshirikisha mke wake jambo lolote au maamuzi yoyote kwani hakutegemea kama mke wake angejibu kwa mkato vile na kuonekana alichofanya hakina maana.
Wanawake wengi hawafahamu umuhimu ambao wanaume wameuweka katika kazi zao na kwamba ukimshukuru kwa kazi anayofanya basi anaweza kukuonesha upendo wa ajabu.
Fikiria wewe ni mwanamke sasa umegundua kwamba ni mjamzito na unaenda kumweleza mume wako naye anakujibu “sawa” then anaendelea kuangalia TV utajisikiaje?
Basi ndivyo mume wako hujisikia pale Unapokuwa hutambua kazi yake hata kama wewe unafanya kazi na kupata fedha kubwa zaidi.
Mwanamke anaweza kuamua au kuchagua kufanya kazi au kuwa nyumbani na kulea watoto, hata hivyo mwanaume anaweza kuchagua kufanya kazi au kwenda jela.
Ni kweli mwanaume mwema huolewa kwa sababu ya UPENDO na si FEDHA, hata hivyo mwanamke huyu mwema huwa na hekima na maarifa ya kufahamu sifa ya ndani ya huyu mwanaume kama anaweza kujenga kiota na kuhudumia vifaranga kwa chakula, mavazi na malazi maisha yao yote.
Je umewahi kumshukuru Mume wako kwa kazi anayofanya?
Kwa mwanamke ambaye anataka kuonesha respect kwa mume wake anaweza kujaribu kuandika hata message au note na kuiweka hata kwenye Lunch box yake na kumwambia “ mpenzi mume wangu nashukuru sana kwa namna unajituma kufanya hiyo kazi kwa ajili ya familia” au vyovyote unavyotaka wewe.
Pia unaweza kumshukuru kwa uhuru aliokupa wewe mwanamke kufanya kazi au kukaa nyumbani na yeye kufanya kazi.
Wapo wanawake ambao huwaza mara kwa mara kwamba wangewashukuru waume zao kwa kufanya kazi, hata hivyo kuwaza peke yake si lolote unachotakiwa kufanya ni kumshukuru au kumwambia.
Je, utajisikiaje mume ambaye anasema kwamba huwa anafikiri mara kwa mara kukwambia anakupenda na hajawahi kukwambia anakupenda!
Ukweli mahusiano ni two way street, mume anatakiwa kukwambia “ANAKUPENDA” na wewe unatakiwa siku moja kumwambia mumeo “Asante sana nashukuru kwa kazi unayofanya ambayo inatupa fedha na maisha”
Nakuahidi atafanya mambo ya ajabu sana kuhusiana na kukupenda wewe kwa sababu ataamini wewe ni mwanamke ambaye unaamini katika yeye.
Mume wako anajiona unamshukuru kwa kazi anayofanya pale tu
Pale unapomwambia kwa maneno au maandishi kwamba kile anafanya kina maana kwako na familia.
Unaelezea imani yako katika taaluma yake.
Unasikiliza stories mbalimbali kuhusu kazi zake na taaluma yake, inaweza kuwa ni magari, ualimu, Computer, forestry, nk.
Kumsaidie kukamilisha ndoto zake kama wakati ule wa kuchumbiana.
Hulalamika kuhusiana na kazi zake

 
asee mkuu kweli kazi ni sensitive issue sana kwa wanaume..ila hawa dada zetu huwa hawajui si kazi tu na mengine mengi...
 
Back
Top Bottom